Makapuku Forum

Makapuku Forum


...ukijaribu kuutafuta ukweli kwa hapa kwetu utachoka kabisa, fikiria kijana amemaliza chuo na hajapata kazi (kwa mfumo wetu serikali ni mwajiri mkubwa) anakaa kupiga mishemishe siku ziende na kapanga chumba maana wadogo zake wanakua .

Tuna safari ndefu ya kufikia hatua ambapo kama huna ajira unalipwa kipato cha kutokuwa na ajira. Hakuna mtu asiyependa kuwa na kipato kwa kufanya kazi, kipato kinakusaidia kulipa mkopo wa shule (sijaulipa bado-ofisi ninayotumikia hailazimishwi kutoa taarifa za wafanyakazi wake) na kukamilisha masuala mengine ya kijamii. Tuna safari ndefu kama hakuna mipango sahihi ya kukabiliana na ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana wengi. FYI takwimu za mtandaoni zinasema karibu vijana laki 9 wanahitimu na katika hawa 300,000 ni wahitimu wa vyuo, jiongeze
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom