Makapuku Forum

Makapuku Forum

.
Screenshot_20181031-173532.jpeg
 
Maswali mengi yameibuka baada ya mabaki ya binadamu kupatikana katika ubalozi wa Vatican nchini Italia.

Taarifa kutoka Vatican inasema
kuwa polisi wanajitahidi kubaini umri na jinsia ya mwili wa mifupa hiyo, na siku ambayo kifo kilitokea.

Vyombo vya habari vya Italia vimesema kuwa mabaki hayo huenda ni ya msichana wa miaka 15 wa mfanyakazi wa Vatican aliyepotea mwaka 1983.
Screenshot_20181031-175254.jpeg
 
Wanafunzi Madrasa Zanzibar wafungiwa vijiwe shingoni ili wafuatilie masomo. Mwalimu Jecha Sule Mohamod kutoka chuo cha madrasatul-Qadiriya kisiwani Zanzibar, anasema mbinu hii imekuwa inatumika tangu zamani kuwafanya watoto watulie na kuzingatia kile wanachofundishwa
Screenshot_20181031-175407.jpeg
 
Mwanamuziki wa kufoka YE au kwa jina la zamani Kanye West ametangaza kujitenga na ushabiki wa siasa. West ameandika kwenye mtandao wake wa Twitter, “Nimefunguka macho sasa na nimegundua nimekuwa nikitumika kusambaza ujumbe wa kisiasa ninao tofautiana nao. Sasa natangaza kujitenga kabisa na siasa”
Screenshot_20181031-175508.jpeg
 
Hatimaye Marekani imetoa wito kwa Saudi Arabia na washirika wake kukomesha vita dhidi ya wapiganaji wa kihouthi wanaoungwa mkono na Iran nchini Yemen .

Yemen inahitaji msaada mkubwa wa kibinadam baada ya mapigano ya miaka minne kuharibu muundo msingi.

Mamilioni ya watu wananjaa na wengi wanaugua utapia mlo baada ya Saudi Arabia kuweka vizuizi kwa njia zote za ardhini angani na hata majini.
Screenshot_20181031-175611.jpeg
 
Wanasayansi nchini Uingereza na Gambia wanasema wana ushahidi wa awali unaoonesha kuwa mbwa wanaweza kunusa malaria .

Wanasayansi hao wamewafunza mbwa kutambua harufu ya malaria kwa kutumia nguo za watu walioambukizwa ugonjwa wa Malaria.

Kuna matumaini makubwa kuwa wanyama hao watatumika katika mapambano dhidi ya malaria na hatimaye kuutokomeza kabisa ugonjwa huo.
Screenshot_20181031-175724.jpeg
 
Mahakama ya juu zaidi nchini Pakistan imebatilisha hukumu ya kifo dhidi ya mwanamke mmoja mkristo, ambaye alikuwa amehukumiwa kinyonga kwa kosa la kukufuru.

Bi Asia anadaiwa kumkejeli mtume Mohammed katika kesi ambayo imeleta mgawanyiko mkubwa nchini Pakistan.
Majaji waliamua kwamba Asia Bibi, ambaye tayari amekuwa gerezani kwa takriban miaka 10 achiwe huru.

Polisi wa kupambana na ghasia wameshika doria mjini Lahore wakihofia huenda ghasia zikaibuka au maandamano ya kidini.
Screenshot_20181031-175834.jpeg
 
Idadi ya watu wanaotumia mtandao wa kijamii wa Facebook imepungua.
Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Facebook, watu bilioni 1.49 walitumia mtandao huo mwezi Septemba ikiwa ni chini ya idadi lengwa ya watu billioni 1.51 billioni.

Aidha kiwango cha ukuaji kilipungua katika mataifa ya Magharibi yaani Marekani, Canada na bara Ulaya.
Facebook hata hivyo imeshuhudia ukuaji wa mitandao yake ya WhatsApp na Instagram.

Screenshot_20181031-175952.jpeg
 
Marekani imetuma wanajeshi 5200 kwenye mpaka wake na Mexico ilikuzuia msafara wa maelfu ya wahamiaji kutoka mataifa ya Kusini mwa Marekani wasiingie nchini humo.

Jenerali Terrence O'Shaughnessy kutoka makao ya jeshi la Marekani Pentagon amesema Operesheni hiyo yenye jina “Faithful Patriot” inalenga majimbo ya Texas, Arizona na California.

Rais Donald Trump alionya wahamiaji hao, wawe tayari kukabiliana na jeshi kwani hatawaruhusu kukanyaga hata mguu mmoja ndani ya ardhi ya Marekani.
Screenshot_20181031-180148.jpeg
 
Muuguzi mmoja nchini Ujerumani amekiri kuua wagonjwa 100 aliokuwa akiwahudumia katika hospitali mbili tofauti ili ”aoneshe uhodari wake kuwafufua”

Niels Högel kwa mujibu wa upande wa mashtaka alikuwa akiwazidishia kipimo cha dawa na kusababisha wagonjwa wake kupatwa na mshtuko wa moyo. Alipoulizwa idadi ya wagonjwa aliowazidishia kipimo cha dawa akajibu “takriban 100 hivi”
Screenshot_20181031-180300.jpeg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom