Makapuku Forum

Makapuku Forum

.
Screenshot_20181030-181748.jpeg
 
Mvulana mmoja amekamatwa akifanya mtihani wa somo la muziki katika shule moja ya wasichana huko Magharibi mwa Kenya .

Mvulana huyo alikuwa amevalia sare ya shule ya upili ya wasichana ya Mukuyu na kusingizia kuwa mtahiniwa wa kike ambaye jina lake limebanwa.

Watahiniwa wenza waling’amua kitendawili hicho baada ya uweledi wake wa kucheza ala za muziki ambayo ni sehemu ya mtihani huo wa somo la Muziki kuwaduwaza .

Mvulana huyo hajatajwa kwa hofu kuwa hajatimiza miaka 18 hata hivyo yeye na mwalimu mkuu wa shule ya upili ya wasichana ya Mukuyu Kakamega wamekamatwa na polisi uchunguzi ukiendelea.
Screenshot_20181030-184139.jpeg
 
Jeshi la DRC limetoa Lori 300 Ndege 10 na Helikopta 10 kwa tume ya uchaguzi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kufanikisha uchukuzi wa vifaa vitakavyo tumika katika uchaguzi mkuu ujao.

Vyama vya upinzani viliandaa maandamano juma lililopita, kupinga matumizi ya mfumo wa kielektroniki wa kupigia kura.

Wanadai vitatumika kumsaidia mwandani wa rais anayeondoka Joseph Kabila kuiba kura. Tume ya uchaguzi imepinga madai hayo.
Screenshot_20181030-184332.jpeg
 
Mahamaka imemuachia huru mtangazaji maarufu wa runinga ya Citizentv bi Jacque Maribe kwa dhamana ya dola elfu 20,000. Mshtakiwa mwenza Joseph Irungu “Jowie” amenyimwa dhamana

Wawili hao wanakabiliwa na mashtaka ya mauaji ya mfanyabiashara Monica Kimani aliyepatikana amechinjwa nyumbani mwezi Septemba.
Screenshot_20181030-184457.jpeg
 
Samahani Ndugu, Baba, Waume na Shemeji kwa sababu hili linawahusu nyote!!

Utafiti umebaini kuwa kinamama wanastahili kusubiri kwa MWAKA MMOJA baada ya kujifungua kabla ya kupata ujauzito mwingine ili kupunguza hatari ya kumpoteza mama na mtoto
.
Muda mfupi kati ya mimba moja hadi nyingine humuweka mama katika hatari ya kuzaa mtoto ambaye hajatimiza wakati wa kuzaliwa,mtoto mdogo au kifo chake.

Eheee kwa hivyo vuteni pumzi jamani USIMHARAKISHIE MAUTI MPENZI WAKO
Screenshot_20181030-184643.jpeg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom