Utajiri na umasikini vipo kwaajiri yetu
Tajiri huonekana kwa kuwa masiki yupo
Masikini huonekana kwa sababu tajiri yupo
Maisha ni kutegemeana
Jifunze kusaidia wale wenye uhitaji pale unapo kuwa nacho
Jitahidi kuhimiza vijana wafanye kazi maana wakati ni sasa
Kazi za kufanya haziko ofisini tu
Unaweza kulima kufuga umachinga udobi genge zote ni kazi maana kujituma kwako ndio mafanikio yako
Jitahidi kusema ukweli daima
Ondoka sehemu iliyo fitinika
Simama kwa kuamini wewe ni mhimu kuliko yule anae kusema vibaya
Pokea ushauri hata kama unajua hauwezi kukusidia hii itakupa heshima mbele ya mtoa ushauri kuwa we we ni msikivu
Ogopa kuishi kwa dharura
Ishi kwa mipangilio unayo jiwekea
Tufanye kazi kwa bidii ili wanao kuja nyuma yetu wajifunze kwetu
Kumbuka ulipo wewe ni kioo cha mtu huwezi kujua maana uko bize na anae kuona kioo chake anakufuatilia kwa umakini mkubwa
TUWE NA MCHANA MWEMA