3. Nimeshazeeka Siwezi kufanya hili/ Umri wangu Bado!
Kwa utafiti mdogo, Nimegundua kuwa waafrika wengi husubiri wafike miaka 30 ndipo waanze kuvaa majukumu mengi (mfano Kuwa na familia, kujenga, kununua ardhi, usafiri nk) Na je umegundua kwamba wakifika umri wa miaka 40 hujiona wazee na kukata tama na kutojihusisha na kujifunza vitu vipya? “mambo ya vijana hayo” Na watu wengi wenye miaka zaidi ya 50 hujiona wamechelewa na teknolojia imeshawapita, kumbe maisha yamerahisishwa! Kama uliweza kujifunza mambo mengi magumu ambayo mpaka unajisifu kwamba vijana wengi wa sasahivi hawayawezi, kwa nini uogope kujifunza kutumia kompyuta, mitandao au simu za kisasa? Hujachelewa anza sasa!