Makapuku Forum

Makapuku Forum

.
Screenshot_20181010-082559.jpeg
 
Habari zinazotufikia kutoka Magharibi mwa Kenya zinasema kuwa basi moja la uchukuzi wa umma limeanguka katika eneo la Fort Tenan lilipokuwa likielekea Kakamega.

Takriban watu 42 wamefariki.
Kilichosababisha ajali hii hakijabainika.
Screenshot_20181010-083200.jpeg
 
Rais wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli amekutana na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia nchini humo Bi Bella Bird kuzungumzia miradi inayofadhiliwa na benki ya dunia.

Hata hivyo, utata bado unaendelea kuhusu msaada wa dola 50 milioni za Marekani ambazo benki hiyo ilikuwa inatarajiwa kutoa kwa taifa hilo.
Screenshot_20181010-083338.jpeg
 
Balozi wa Marekani katika umoja wa mataifa UN Nikki Haley amejiuzulu takriban miaka miwili tangu achukue mikoba ya kumwakilisha rais Donald Trump na sera zake katika maswala ya kidiplomasia katika ulingo wa UN.

Trump amemsifu kwa ukakamavu wake na kumuahidi wadhfa wowote katika siku za usoni
Screenshot_20181010-083517.jpeg
 
"Nikiwa na miaka 16 baba yangu aliandika hotuba yake kwa ajili ya kuisoma siku ya harusi yangu.

Kila nilipokuwa nasherehekea siku yangu ya kuzaliwa mama yangu alikuwa akiniombea, na kwa miaka ya karibuni maombi yake yalikuwa pamoja na kupata mume bora, ambaye atanifaa," amesema Bi Lulu Jemimah mwenye umri wa miaka 32 aliyejioa mwezi Agosti jijini Kampala na kudai kuwa kwa miaka kadhaa watu wamekuwa wakimuuliza kuwa lini angefunga ndoa.
Screenshot_20181010-083632.jpeg
 
Baada ya kutamba sana akiichezea klabu ya KRC Genk nchini Ubelgiji

, Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Tanzania Mbwana Ally Samatta anang'ang'aniwa na klabu tatu za England.

Tetesi zinasema nyota huyo anatafutwa na West Ham United, Everton na Burnley. Wewe Ungemshauri ajiunge na klabu ipi
Screenshot_20181010-083824.jpeg
 
Chuo Kikuu cha Makerere Uganda kimewataka wakufunzi kuweka wazi uhusiano wao wa kimapenzi na wanafunzi ili kuepusha mgongano wa kimaslahi.

Makamu Mkuu, Prof. Barnabas Nawangwe amesema, chuoni uhusiano wa kimapenzi unaruhusiwa, lakini lazima uwekwe wazi ili kutoathiri pande zote.
Screenshot_20181010-084211.jpeg
 
Nada Zaelnoon Ahamed (raia wa Sudan Kusini) na Mohamed Belal (raia wa Syria) wamekamatwa katika uwanja wa ndege wa Dar es Salaam wakisafirisha USD 70,000 na Paundi 3,410 za Sudan bila kufuata taratibu.

Sheria inataka ukiwa na fedha kuanzia USD 10,000 ujaze fomu ya maelezo kuhusu fedha hizo.

Watuhumiwa wote wawili wamezuiwa na hawawezi kuendelea na safari zao kwa ajili ya uchunguzi zaidi na hatua za kisheria zilizopo
Screenshot_20181010-084351.jpeg
 
Mmoja wa mashuhuda amesema kuwa, huenda Pancho Latino alizidiwa na pombe wakati akiogelea kwani walipoopoa mwili wake kutoka baharini na kuugandamiza, pombe nyingi ilitoka.

Imeelezwa, alikaa ndani ya maji kwa dakika 10, hali iliyowashtua watu, na walipomwendea akawa amefariki dunia
Screenshot_20181010-084624.jpeg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom