Makapuku Forum

Makapuku Forum

Ishu hapo siyo wakili bali aina ya sheria /hukumu
Kwa Bongo kosa la mauaji ni kifungo cha maisha(life imprisonment) na kuua bila kukusudia adhabu inaweza kuwa miaka miwili na kuendelea
Nchi zinatofautiana sheria hivyo Tz ukipatikana na hatia ya mauaji(murdsr) hata utetewe na Kibatala adhabu ni hiyohiyo
Mambo kaka ake
 
Kuwa na afya bora haitokani na kula nyama , pilau, chips , biriani , soseji, bugger, n.k, mafanikio ya afya bora inatokana na vitu vifuatavyo.

1.Angalia afya ya akili , kimwili na kiroho.

kuwa mwenye afya bora ni rahisi sana kuliko unavyofikiria wewe, haikuchukulii muda mwingi wala pesa nyingi , mfano usafi wako mwenyewe kimwili, usafi wa mazingira yako, mahusiano yako , ndoa yako ina amani, na je mahusiano yako na Mungu yakoje,

kuna watu hata kuoga wao wanaona kama adhabu , eti akiwa ameoga asubuhi , basi hata usiku haogi anaenda kulala hivyo hivyo, nguo nazo hata hafui anavaa mara mbili au tatu eti mpaka aone imechafuka. haendi kucheki hata kama anaumwa bali anameza dawa kwa kuwa tu ana maumivu ya kichwa . unaongeza sumu mwilini.
 
2.Mawazo yako yote yawe na afya.

kuna watu wawili tofauti , kuna mtu anaeishi na kuna mwingine haishi, ingawa wote wako hai. mawazo yakom yakiwa na afya kila siku utakuwa unatafuta naman ya kufanikiwa , na kama una mafanikio basi utatafuta kusonga mbele zaidi, lakini mtu ambae haishi yeye siku zote anawaza kushindwa kushindwa, hata haoni njia ya kupita ili akafanikiwe.

mawazo yenye afya hutafuta ni wapi nikawasaidie wenye mahitaji , wakati wenye mawazo yalikufa wanawaza namna gani nitaiba , nitadhulumu, nitadanganya na kuharibu watu.
 
3.Fanya mazoezi.



mazoezi yakusaidia kuwa mwenye afya na mwenye furaha na nguvu, utakuwa unajisikia vizuri kila siku. utaonekana mwenye amani . na wala hutachukua muda mrefu , dakika 20-30 zinakutosha kukupa changamoto kubwa ya mafanikio


4.Usichukulie mazoezi kama ndio yatakusaidia kupunguza mwili.



huwezi kuwa unakula kila chakula maadamu ni chakula na kufikiria kuwa kwa sababu unafanya mazoezi basi utapungua mwili au ndio utakuwa mwenye afya nzuri sio. utakuwa ni kichaa maana utafanya mazoezi ya nguvu lakini hutafanikiwa malengo yako.

fanya mazoezi kwa afya na huku ukiwa makini katika ulaji wako wa kila siku. njia hizi zitakusaidia.

_kula kila unaposikia njaa tu.

_ukiwa huna njaa usile.

_kunywa maji ya kutosha.

_lala masaa 7 usiku,

_fanya mazoezi kila siku.
 
5.usisikilize watu.

Ninaposema usikilize mtu , kuna watu wanapenda kukatisha watu tamaa , ukiwa umeamua kufanya kitu songa mbele bila ya kusikia ya watu. unaweza kusikiliza lakini unapima. kama yana akili.


6.Changamoto itakufanya utokezee mahali.

kama ukikutana na watu wenye mafanikio makubwa , wale wanaojulikana ulimwenguni , wamepitia changamoto nyingi na ngumu sana. na ni lazima uelewe hakuna mafanikio yanayokuja bila ya changamoto. . changamoto huleta mafanikio na mafanikio huleta changamoto. huwezi kufanikiwa ikiwa maisha ni rahisi .
 
7.JIULIZE KWA NINI. SWALI HILI NI KUBWA.

Unaweza kuwa unajiuliza kwa nini mimi , kwa nini yule, labda kwa sababu ya kuwa na afya nzuri kuliko wewe, au kuwa na maendeleo makubwa kuliko wewe. majibu unayo wewe , upande wangu naona kuwa kuna watu huchukua maamuzi magumu kuliko wengine huwa wanajihurumia na kuona kama aibu kufanya vitu ambavyo vinawaletea mafanikio.
 
8.Kumbuka kuwa kitasa kidogo kinafungua milango mikubwa na mageiti makubwa.



Unapoamua kufanya kitu kimoja kitasaidia vitu vingi, ukifanya maamuzi mazuri katika maisha yako, kila kitu kitakwenda vizuri, kitu kidogo utakachoanza nacho kitafungua mambo makubwa maishani.


9.Unapofanya kitu kimoja kitasaidia vitu vyote.

unapojiwekea kipaumbele afya yako iwe namba moja, utaona furaha amani, kazi zikienda vizuri. unatakiwa kuwa na mazoea hayo ya kila siku.
 
10.Unastahili kuwa na afya bora.

kwa nini uteseke kwa kwa sababu tu ya vitu vinavyovutia macho , chips zinavutia sana , nyama za kuchoma, pombe, sigara, na vyakula vingi vya kukaanga. unaweza kula lakini ule kwa adabu , sio kwa fujo. wenye afya wana uchaguzi. chagua vyakula vyenye akili hata kama una hela nyingi kula vyakula vyenye akili vipo . isile mradi unakula.


11.Kila asubuhi panga miango yako ya siku.

Kila siku ikiwa unapanga mipango yako na kuhakikisha unafanya yote, ingawa kuna ambayo hutafanikisha lakini kwa sehemu kubwa utafanya. utaona mafanikio yako na kutimiza ndoto yako.
 
12.Uwe mwoga.

Utapataje kitu bila msukumo , kitu kinachoonekana ni kigumu na hakina hata njia ya kufanya kinaogopesha, lakini kinakufanya uondoke katika kiti chako na kukifanya kwa sababu ya kuogopa kupoteza. na kwa kuwa unatafuta kufanikiwa lazima ule woga utakufanya uondoke.
 
CHAKULA NA DAWA.

Ilikuwa vigumu kufikiria muda nguvu utulivu na pesa ambayo nilitumia kutafuta uponyaji na afya njema na amani .ilikuweka afya yangu vizuri kila wakati nilijaribu kitu kipya cha kunisaidia kiafya ,mara mazoezi na jinsi kuwa vizuri ,nilichanganyikiwa katika kuchunguza namna ya ulaji mbalimbali na namna tofauti tofauti.

NILIKUWA NA MATUMAINI NA KUPATA KITABU KIMOJA CHA KUNISAIDIA AU UTARATIBU WOWOTE AMBAO UNGENISAIDIA BILA YA KUHARIBU MAISHA YANGU



Hii ni baada ya kugundua kitu gani kinafanya kazi vizuri. watu wengi pia wamekuwa wakikumbana na matatizo kama yangu ya kutafuta afya na kuishi kwa na afya njema.

kwa nini kuna kuwa na watu au makundi mengi yanahangaikia kutafuta maamuzi na kutafuta majibu ,pia watu wa wa bidhaa za afya pia nao kwa nini wapo kwetu ? ni kwa sababu wengi wetu tu wagonjwa , tumechoka,na tuna misongo ya maisha ,kabla hata ya wakati .
 
Katika matatizo haya ya afya tunatakiwa kuangalia kiini ni nini , ili kuundoa mzizi wake, tuangalie imani zetu, zisizo na ukweli,zinazoleta fikra mbaya , matendo na tabia zetu za ulaji nazo ni sababu tosha ya kuleta matatizo ya afya zetu.tukipata kiini ndipo tutajua na kuweza kurudisha fikra zetu kuwa nzuri , na hatuta hangaika na matatatizoya afya.



Kwa kupitia udadisi wa vitabu mbalimbali nimegundua funguo za saba za kufungua ,ambazo zitakutoa mahali ulipo na kukupeleka unakotaka kuwa.na utapata majibu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom