Makapuku Forum

Makapuku Forum

1,KUWA MAKINI NA MAWAZO NA MATENDO YAKO:

Mara nyingi tunachukua muda mwingi kujiuliza tabia zetu ambazo zinakuwa mbaya, kwa mfano ; kwanini nimechukua hatua hii , kwa nini mawazo haya yameibuka wakati nafikiria kuhusu afya .


2.SIKILIZA MWILI WAKO UNATAKA NINI:

Je unahisi maumivu , msongo wa mawazo au uchovu? mwili wako unasema nini muda huu? mara nyingi mwili wako huwa unakupa vielelezo au saini ya kutaka kitu fulani na kukataa kitu kingine,lakini kutokana na hali ya maisha inakuwa ngumu kufuata matakwa ya mwili, tunakuwa tunalazimisha kula vyakula ambavyo havistahili .ndipo hapo mwili unapovunjika .

changamoto hizi za mwili na chakula ziko kukusaidia wewe na kukufundisha kusikiliza .
 
3.VUNA MAFANIKIO

Mara nyingi hatuna muda wa kusherehekea vitu ambavyo tumepata ,au umbali gani tumetoka , kila wakati tunakuwa na sababu nyingi na mawazo ya kusikiliza mwili.lakini kuna kusherehekea kwa namna nyingi , waweza kuruka juu na chini, kulala na kufikria, kuimba kwa kutoa sauti, kwenda kumsaidia mtu yeyote mwernye mahitaji na unatakiwa wakati mwingine kupumua na kuvuta hewa tu

4.TOA UJUZI WAKO KWA WENGINE

Mara nyingi tunaandika vitu visivyowezekana ambavyo hatuna uwezo navyo, tunakuwa kama mpanda ngazi, ni kama mjasiria mari mdogo .toa ujuzi wako kama wewe ni mwalimu fundisha kwa bidii,kama wewe ni dactari fanya kazi yako vizuri , hudumia watu kwa moyo wote , maana wewe uko hapo ni nafasi uliyopewa na MUNGU ili uhudumie. fanya kazi kwa ajili ya watu si kwa ajili yako utapata mafanikio.

wewe ni kisima kinachotoa maji , sasa basi chota hayo maji yagawe kwa wengine.,ili watu wafaidike na ulichonacho.
 
5,MWAGILIA MBEGU

Maisha yetu ni sawa na shamba au mmea uliooteshwa ,unatakiwa kumwagiliwa na kupaliliwa ili uwe na rutuba na afya njema, wakati tunapopalilia tunaondoa uchafu na vitu ambavyo vinaleta kukosesha hewa , kwa hiotunatoa ili kuacha mwili uwe safi .

unapokuwa na tabia nzuri unajiongoza kuwa na mawazomazuri,jisamehe mwenyewe, usiige tabia za watu ,amini utendacho,fanya upendacho,kula vizuri ,matunda mboga ,tafakari ,ishi sasa.

6. FURAHIA MIPANGO ULIONAYO.

Acha kufikiria mambo yaliyopita,anza kufikiria yaliyopo , Hakuna mtu ambaye anaweza kurudi nyuma nsa kuanza upya, lakini unaweza kuanza upya ulipo na kumaliza salama safari yako yenye mafanikio makubwa.

Kufanikiwa kuwa na afya kila mtu anataka, furahia maisha,furaha ya kweli haiji tu kwa kuangalia TV.au kuangalia idadi ya vitu ulivyonavyo hapana , furaha ya kweli huja pale unapofurahia kila dakika na kilahatua ya maisha yako ya ushindi.
 
7.WEKEZA AFYA YAKO MWENYEWE USISUBIRI MTU.

Unapowekeza nguvu katika kutengeneza afya yako, hayo ndio maisha yako.kwa sababu hio mafanikio ya afya ni ushindi na ni ushuhuda.kutafuta ukamilifu wa usawa na kuishi muda mrefu hayaji kwa usiku mmoja. fanya mabadiliko na kazania yale unayofanya kwa ajili nya afya yako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom