Numbisa
JF-Expert Member
- Dec 12, 2016
- 348,117
- 1,249,282
Jasho ni moja ya njia maalumu ya mwili ya kurekebisha kiwango cha joto la mwili, ila inapofika wakati jasho hili linaanza kutoa harufu mbaya hua kero kwa mtu anaetoa harufu na kwa jamii nzima inayomzunguka.
Kwa kawaida jasho hua halina harufu, kwani jasho ni mchanganyiko wa maji na aina mbali mbali za madini chumvi yanayotolewa kama taka mwili,
Harufu mbaya ya kwapa husababishwa baada ya bakteria kumeng`enya aina flani ya protini inayozalishwa pamoja na jasho kutoka katoka tezi maalumu za jasho ziitwazo apocrine glands. Tezi hizi zinapatikana katika maeneo ya makwapa, matiti, maeneo ya sehemu za siri na katika kope za macho.
Kwa baadhi ya watu hali hii ya kunuka kwapa hua sugu sana na hivyo kua kero kwao na jamii kwa ujumla. Ili kupunguza harufu au kuimaliza kabisa yapaswa kupunguza pia kiwango cha jasho unalozalisha kwa siku kwa kufanya yafuatayo;
1; Kula mlo kamili na fanya mazoezi ili kupunguza mwili, kwa sababu watu wanene huathiriwa sana na tatizo hili kwa sababu ya mikunjo mikunjo ya ngozi yao hivyo kutoruhusu jasho kukauka mwilini.
2; Vaa nguo za pamba , nguo za aina hii husharabu jasho la mwili na kukuacha mkavu, epuka pia nguo zanazokubana sana.
Kwa kawaida jasho hua halina harufu, kwani jasho ni mchanganyiko wa maji na aina mbali mbali za madini chumvi yanayotolewa kama taka mwili,
Harufu mbaya ya kwapa husababishwa baada ya bakteria kumeng`enya aina flani ya protini inayozalishwa pamoja na jasho kutoka katoka tezi maalumu za jasho ziitwazo apocrine glands. Tezi hizi zinapatikana katika maeneo ya makwapa, matiti, maeneo ya sehemu za siri na katika kope za macho.
Kwa baadhi ya watu hali hii ya kunuka kwapa hua sugu sana na hivyo kua kero kwao na jamii kwa ujumla. Ili kupunguza harufu au kuimaliza kabisa yapaswa kupunguza pia kiwango cha jasho unalozalisha kwa siku kwa kufanya yafuatayo;
1; Kula mlo kamili na fanya mazoezi ili kupunguza mwili, kwa sababu watu wanene huathiriwa sana na tatizo hili kwa sababu ya mikunjo mikunjo ya ngozi yao hivyo kutoruhusu jasho kukauka mwilini.
2; Vaa nguo za pamba , nguo za aina hii husharabu jasho la mwili na kukuacha mkavu, epuka pia nguo zanazokubana sana.

