Makapuku Forum

Makapuku Forum

Huenda unajisikia umepotea, na unaona marafiki wako bize hawakukumbuki.

uenda unahisi hakuna kitu kizuri mbele yako. Unatamani muda uishe haraka uende kulala tena . Huenda unahisi kitu kilichotokea kwako kama ndoto ya mchana. Ni kwa sababu huna kitu cha kufanya.

Ni mtazamo wako unatesa akili yako . jinsi unavyojisikia unavuta hali ile ile ya watu wakuone jinsi ulivyo. Unajihisi kama hakuna kitu kinachowezekana kwako zaidi ya kurudi kulala au kwenda kulewa. Lakini sio kweli. Mara zote kuna kitu cha kufanya.Ni kwa sababu bado uko gizani, Toka gizani nenda kwenye Nuru.

Acha kulalamika kwa sababu zipo kazi mamilioni ambazo unaweza kufanya bila hata ya kumuomba mtu kwa kutumia muda wako tu. Kila siku anza na ratiba yako, unaweza kujifunza kitu ambacho hujawahi kufanya. unaweza kusoma vitabu, unaweza kwenda kwenye semina mbalimbali. Unaweza kwenda baharini kama mahali ulipo kuna bahari. unaweza kutoka na kutembea kwenye Nature. Unaweza kujifunza kupika chakula ambacho hujawahi kupika. Unaweza kuanza mazoezi .Fanya kitu chochote ambacho utakiweza.

Hata kama hujisikii kuvaa hata nguo, hata kama hujisikii hata kusogea, unao uwezo wa kujilazimisha kufanya hivyo. Ondoka kwenye hali hio. Usipoteze siku yako, tengeneza siku yako. Kwa sababu utakapopoteza siku moja ndivyo ambavyo utapoteza siku inayofuata. Usipende kukaa mahali salama kila wakati, unapoteza muda wako. Usipende maisha ya kawaida wakati una uwezo wa kuishi maisha ya juu.

Maisha yako yasiwe na mazoea ya kuamka na kwenda kazini au shuleni na kurudi tena kulala. Pata muda wa kukaa na kufikiri kujiboresha zaidi ya unachokifanya kwa siku nzima. Hisi kama unatembea huku umelala wiki nzima.

Fanya kitu leo, pata kitu ndani ya siku yako, ili ujisikie kuwa mtu bora Duniani, kwamba una faida ya kuwepo hapa. Kwa sababu utatambua kuwa hukutumia muda wako vibaya.

Fanya mazoezi kwa dakika 40 na kuendelea, jibu simu ambazo umekuwa ukizikataa, jibu meseji, Fanya Usafi, Fanya kitu cha upendo kwa mtu mwingine, utaona furaha inakaa kwako. Jipongeze mwenyewe.

Usisubiri Kesho kukamilisha lengo lako. Vitu vikubwa huchukua muda kukamilika, havitokei kwa usiku mmoja. Itakuchukua miaka kadhaa kufika lengo lako. Kama kila kazi zako unaziweka ili ufanye wiki ijayo au mwaka ujao, hutakaa ukamilishe lengo lako.

Huwa ni ngumu sana kusubiri kitu, lakini ni rahisi kukaa muda mrefu bila kufanya kitu, Lakini kumbuka kukaa bila ya kufanya kazi sio afya. Jitoe muhanga kama unataka kufanikiwa maisha yako.

Kama unajipenda, kama unajali furaha yako, Basi weka nguvu kubwa kwenye kitu unachokipenda . Utaipata ndoto yako , hutakuwa mtu wa kulalamika tena. utakuwa umepiga uvivu kwa nguvu zako zote. Fanya kitu leo , Usisubiri kesho.
 
Ukiona mtu amekuzidi kwa kitu chochote, tambua kuwa kuna kitiu amekiona ambacho wewe hukioni.

Atakuwa anaishi kwa mafunuo sio kwa mawazo ya kawaida. Mafunuo ni Mungu anakupa lakini mawazo yanatoka kwa watu.

Ukiwa na mafunuo ya kazi yako, yatakuwa ni ya kudumu kwa sababu yanatoka kwa Mungu, lakini wazo la mwanadamu huwa halidumu.

Ziko siri ambazo zimejificha , na kama ukitaka kujua siri hizi , ni kutafuta mahusiano na Mungu, kutumia Muda vizuri , kumwamini Mungu na kumpenda Mungu.

Kutumia muda vizuri ni kufikiri kwa muda wa kutosha. Fikiri mpaka akili itoke jasho. Muombe Mungu akupe mafunuo ili uweze kuona vitu ambavyo havionekani.
Kuna watu wamefungwa macho na masikio yao, Wapo gizani japo wanajiona wapo kwenye Mwanga. Akili zao zimefungwa na giza kubwa la kukosa maarifa ya neno la Mungu. Ukiona huwezi kutambua vitu vizuri, unatambua vitu vibaya , umefungwa kama sio kujifunga mwenyewe.

Walakini iko Hekima tusemayo kati ya mwanadamu, ila si hekima ya Dunia hii. Wala ya wale wanaoitawala Dunia, wanaobatilika, bali Hekima ya Mungu katika siri. Ile Hekima iliyofichwa ambayo Mungu aliiazimu tangu Milele. Kwa utukufu wetu. Ambayo wenye kuitawala Duinia hii Hawaijui hata mmoja.

Kama ilivyoandikwa Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio kusikia , mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao. Mungu anawafunulia wale tu wampendao, kama humpendi Mungu utapata mawazo ya kawaida lakini hutaweza kupata mafunuo ya Mungu.

Mungu hawezi kukushushia kiti , meza, kitanda, mbao za kujengea.

Mungu anakupa MTI ili upate mafunuo ya kutengeneza kiti, meza na kitanda na vingine.

Mungu hawezi kukushushia gari bali atakupa HEKIMA ya kutengeneza gari, pikipiki, meli, treni , ndege na vingine.


Ukiona mtu analalamika, analalamikia serikali, wazazi, ndugu, marafiki na kujilalamikia mwenyewe, Muda wake umekufa, hafikiri na yupo gizani. ana macho lakini haoni furusa, ana masikio lakini hasikii . Hana mafunuo . Hayupo na Mungu.

Siku ukiona fursa umeona maisha.Watu wanaweza wakakudharau lakini kumbe ulichonacho ndani yako ni kikubwa. umebeba mafunuo makubwa.

Kwa hio usilegee, bali ijapokuwa utu wako wa nje umechakaa, lakini utu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku. maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio.

Tusiangalie vinavyoonekana bali visivyooonekana, kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu, bali visivyoonekana ni vya kudumu.

Usikubali mtu akudharau, wewe una akili , wewe ni wa kipekee, wewe ni shujaa, Jitambue upesi.

Mungu atakutengeneza na kukuthibitisha na kukutia nguvu.

Tafuta kupata mafunuo ya Mungu.
 
kutokana na ugumu wa ajira kwenye zama hizi watu wengi wanaona kujiajiri au kuwa mjasiriamali ndio njia mbadala ya kuyakomboa maisha yao. Hivyo kumekuwa na wimbi kubwa la watu kuondoka kwenye kazi na kwenda kujiajiri au kuanzisha biashara zao. Ni kitu kizuri sana kwa sababu angalau watu wanaweza kuwa na mamlaka na maisha yao na wanaeza wakaajiri na wengine pia. Ila kwa upande wa pili sio wote wanaokwenda njia hiyo wanafanikiwa kufikia malengo waliyojiwekea. Wengi sana wanashindwa na kujikuta wako kwenye mazingira magumu kuliko hata yale waliyokuwa nayo kwenye ajira.

Leo tutazungumzia mambo unayotakiwa kuyajua au kuyafanya kabla hujaacha kazi na kuingia kwenye ujasiriamali au biashara. Sisemi mambo haya ili kukukatisha tamaa na uendelee kuwa mtumwa, ila nayasema ili kukupatia mwanga wa kule unakokwenda ili usije kushangazwa na mambo haya baadae. Mambo hayo ni kama ifuatavyo;

1. Kujiajiri au ujasiriamali ni kugumu.

Kama unafikiri kujiajiri au kuingia kwenye ujasiriamali ndio nJia rahisi kwako kufanikiwa ni vyema ukabadili mawazo yako mara moja kabla hujaingia na ukashindwa vibaya. Zaidi ya nusu ya biashara zinazoanzishwa zinakufa ndani ya mwaka mmoja baada ya kuanzisha. Na hata zile zinazoendelea kudumu zinakuwa na hali ngumu sana na hazitengenezi faida kubwa. Hizi ni takwimu ambazo zinasikitisha sana ila ndio ukweli wenyewe.

Kujiajiri ni kugumu, ujasiriamali ni mgumu na biashara ni ngumu. Jua kabisa unaingia kwenye njia ambayo uwezekano wa kushundwa ni mkubwa hivyo mipango na kufanya kazi kwa bidii na maarifa ni muhimu sana

2. Utafanya kazi kuliko ulivyokuwa umeajiriwa.

Unafikiri ukishajiajiri wewe ndio bosi mwenyewe unakaa nyuma ya meza kubwa yenye kiti cha kuzunguka huku ukiongea na simu au wageni na wateja waliokutembelea ofisini. Ndoto za mchana hizo. Unaweza kukaa kwenye kiti cha kuzunguka na meza kubwa ila utafanya kazi zaidi ya unavyofanya kwenye ajira. Unaweza kujikuta unafanya kazi masaa kumi na mbili ofisini na ukirudi nyumbani unaendelea tena na kazi kwa zaidi ya masaa mawili. Mwanzo wa biashara au ujasiriamali kuna misingi mingi unayotakiwa kuijenga na ni wewe pekee utakaefanya hivyo.

3. Utavaa kofia nyingi kwa wakati mmoja.

Kwenye ajira yako una jukumu moja tu au machache yaliyoelezwa. Labda unafanya kazi kwenye idara ya masoko, au idara ya uzalishaji au idara ya huduma kwa wateja na kadhalika. Unapojiajiri utajikuta unafanya kazi za kila idara katika biashara yako. Kuna wakati utavaa kofia ya kiongozi, wakati mwingine masoko, wakati mwingine huduma kwa wateja na kadhalika. Kuwa tayari kubadilika kutokana na hitaji la biashara yako kwa wakati husika.

4. Usichome madaraja.

Kuna dhana moja iliyokuwa ikitumika sana kipindi cha nyuma ambapo mtu alikuwa akiondoa uwezekano wowote wa kurudi nyuma. Kwa mfano kama wewe unataka kuacha kazi na kwenda kujiajiri basi unagombana na waajiri wako kiasi kwamba huwezi kurudi tena kwenye ulimwengu wa ajira, hii inakusababisha uhakikishe unafanya kila mbinu kufanikiwa kwani huna kimbilio jingine. Dhana hii ilifanya kazi sana zamani ila kwa sasa usijaribu kuitumia. Ondoka kwa amani na kama ikiwezekana mwambie muajiri wako unakwenda kufanya nini, mwajiri wako tayari ana mtandao mkubwa hivyo anaweza kukusaidia kupata wateja wa biadhaa au huduma uayokwenda kutoa. Nguvu ya mtandao ni kubwa sana kwenye ulimwengu wa sasa wa biashara na ujasiriamali.
 
kutokana na ugumu wa ajira kwenye zama hizi watu wengi wanaona kujiajiri au kuwa mjasiriamali ndio njia mbadala ya kuyakomboa maisha yao. Hivyo kumekuwa na wimbi kubwa la watu kuondoka kwenye kazi na kwenda kujiajiri au kuanzisha biashara zao. Ni kitu kizuri sana kwa sababu angalau watu wanaweza kuwa na mamlaka na maisha yao na wanaeza wakaajiri na wengine pia. Ila kwa upande wa pili sio wote wanaokwenda njia hiyo wanafanikiwa kufikia malengo waliyojiwekea. Wengi sana wanashindwa na kujikuta wako kwenye mazingira magumu kuliko hata yale waliyokuwa nayo kwenye ajira.

Leo tutazungumzia mambo unayotakiwa kuyajua au kuyafanya kabla hujaacha kazi na kuingia kwenye ujasiriamali au biashara. Sisemi mambo haya ili kukukatisha tamaa na uendelee kuwa mtumwa, ila nayasema ili kukupatia mwanga wa kule unakokwenda ili usije kushangazwa na mambo haya baadae. Mambo hayo ni kama ifuatavyo;

1. Kujiajiri au ujasiriamali ni kugumu.

Kama unafikiri kujiajiri au kuingia kwenye ujasiriamali ndio nJia rahisi kwako kufanikiwa ni vyema ukabadili mawazo yako mara moja kabla hujaingia na ukashindwa vibaya. Zaidi ya nusu ya biashara zinazoanzishwa zinakufa ndani ya mwaka mmoja baada ya kuanzisha. Na hata zile zinazoendelea kudumu zinakuwa na hali ngumu sana na hazitengenezi faida kubwa. Hizi ni takwimu ambazo zinasikitisha sana ila ndio ukweli wenyewe.

Kujiajiri ni kugumu, ujasiriamali ni mgumu na biashara ni ngumu. Jua kabisa unaingia kwenye njia ambayo uwezekano wa kushundwa ni mkubwa hivyo mipango na kufanya kazi kwa bidii na maarifa ni muhimu sana

2. Utafanya kazi kuliko ulivyokuwa umeajiriwa.

Unafikiri ukishajiajiri wewe ndio bosi mwenyewe unakaa nyuma ya meza kubwa yenye kiti cha kuzunguka huku ukiongea na simu au wageni na wateja waliokutembelea ofisini. Ndoto za mchana hizo. Unaweza kukaa kwenye kiti cha kuzunguka na meza kubwa ila utafanya kazi zaidi ya unavyofanya kwenye ajira. Unaweza kujikuta unafanya kazi masaa kumi na mbili ofisini na ukirudi nyumbani unaendelea tena na kazi kwa zaidi ya masaa mawili. Mwanzo wa biashara au ujasiriamali kuna misingi mingi unayotakiwa kuijenga na ni wewe pekee utakaefanya hivyo.

3. Utavaa kofia nyingi kwa wakati mmoja.

Kwenye ajira yako una jukumu moja tu au machache yaliyoelezwa. Labda unafanya kazi kwenye idara ya masoko, au idara ya uzalishaji au idara ya huduma kwa wateja na kadhalika. Unapojiajiri utajikuta unafanya kazi za kila idara katika biashara yako. Kuna wakati utavaa kofia ya kiongozi, wakati mwingine masoko, wakati mwingine huduma kwa wateja na kadhalika. Kuwa tayari kubadilika kutokana na hitaji la biashara yako kwa wakati husika.

4. Usichome madaraja.

Kuna dhana moja iliyokuwa ikitumika sana kipindi cha nyuma ambapo mtu alikuwa akiondoa uwezekano wowote wa kurudi nyuma. Kwa mfano kama wewe unataka kuacha kazi na kwenda kujiajiri basi unagombana na waajiri wako kiasi kwamba huwezi kurudi tena kwenye ulimwengu wa ajira, hii inakusababisha uhakikishe unafanya kila mbinu kufanikiwa kwani huna kimbilio jingine. Dhana hii ilifanya kazi sana zamani ila kwa sasa usijaribu kuitumia. Ondoka kwa amani na kama ikiwezekana mwambie muajiri wako unakwenda kufanya nini, mwajiri wako tayari ana mtandao mkubwa hivyo anaweza kukusaidia kupata wateja wa biadhaa au huduma uayokwenda kutoa. Nguvu ya mtandao ni kubwa sana kwenye ulimwengu wa sasa wa biashara na ujasiriamali.
Shukrani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom