Ukiona mtu amekuzidi kwa kitu chochote, tambua kuwa kuna kitiu amekiona ambacho wewe hukioni.
Atakuwa anaishi kwa mafunuo sio kwa mawazo ya kawaida. Mafunuo ni Mungu anakupa lakini mawazo yanatoka kwa watu.
Ukiwa na mafunuo ya kazi yako, yatakuwa ni ya kudumu kwa sababu yanatoka kwa Mungu, lakini wazo la mwanadamu huwa halidumu.
Ziko siri ambazo zimejificha , na kama ukitaka kujua siri hizi , ni kutafuta mahusiano na Mungu, kutumia Muda vizuri , kumwamini Mungu na kumpenda Mungu.
Kutumia muda vizuri ni kufikiri kwa muda wa kutosha. Fikiri mpaka akili itoke jasho. Muombe Mungu akupe mafunuo ili uweze kuona vitu ambavyo havionekani.
Kuna watu wamefungwa macho na masikio yao, Wapo gizani japo wanajiona wapo kwenye Mwanga. Akili zao zimefungwa na giza kubwa la kukosa maarifa ya neno la Mungu. Ukiona huwezi kutambua vitu vizuri, unatambua vitu vibaya , umefungwa kama sio kujifunga mwenyewe.
Walakini iko Hekima tusemayo kati ya mwanadamu, ila si hekima ya Dunia hii. Wala ya wale wanaoitawala Dunia, wanaobatilika, bali Hekima ya Mungu katika siri. Ile Hekima iliyofichwa ambayo Mungu aliiazimu tangu Milele. Kwa utukufu wetu. Ambayo wenye kuitawala Duinia hii Hawaijui hata mmoja.
Kama ilivyoandikwa Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio kusikia , mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao. Mungu anawafunulia wale tu wampendao, kama humpendi Mungu utapata mawazo ya kawaida lakini hutaweza kupata mafunuo ya Mungu.
Mungu hawezi kukushushia kiti , meza, kitanda, mbao za kujengea.
Mungu anakupa MTI ili upate mafunuo ya kutengeneza kiti, meza na kitanda na vingine.
Mungu hawezi kukushushia gari bali atakupa HEKIMA ya kutengeneza gari, pikipiki, meli, treni , ndege na vingine.
Ukiona mtu analalamika, analalamikia serikali, wazazi, ndugu, marafiki na kujilalamikia mwenyewe, Muda wake umekufa, hafikiri na yupo gizani. ana macho lakini haoni furusa, ana masikio lakini hasikii . Hana mafunuo . Hayupo na Mungu.
Siku ukiona fursa umeona maisha.Watu wanaweza wakakudharau lakini kumbe ulichonacho ndani yako ni kikubwa. umebeba mafunuo makubwa.
Kwa hio usilegee, bali ijapokuwa utu wako wa nje umechakaa, lakini utu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku. maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio.
Tusiangalie vinavyoonekana bali visivyooonekana, kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu, bali visivyoonekana ni vya kudumu.
Usikubali mtu akudharau, wewe una akili , wewe ni wa kipekee, wewe ni shujaa, Jitambue upesi.
Mungu atakutengeneza na kukuthibitisha na kukutia nguvu.
Tafuta kupata mafunuo ya Mungu.