Makapuku Forum

Makapuku Forum

Nimerudi tena wadau baada ya ratiba kubadilika kiaina na sasa wiki hii imetengemaa angalau naweza kukaa chini na kuchangia sehemu hii ninayoipenda kupita maelezo.

Sitaki kuuliza kama kuna jipya ila kutoka kwangu, niliwakumbuka sana wadau mnaolifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo
 
Nimerudi tena wadau baada ya ratiba kubadilika kiaina na sasa wiki hii imetengemaa angalau naweza kukaa chini na kuchangia sehemu hii ninayoipenda kupita maelezo.

Sitaki kuuliza kama kuna jipya ila kutoka kwangu, niliwakumbuka sana wadau mnaolifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo
Binamu jamani tulikumiss
 
Muziki: Kama Mwanzo

....itoshe tu kusema nililikukumbuka wewe Kapuku unayelifanya Jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo. Uwepo wako hapa unaweza usiwe unaniingizia pesa mkononi (wengine huwa wanaweka pesa mfukoni, tunatofautiana, wengine wanaweka kwenye matiti, nimesema tunatofautiana na hakuna ubaya ili kuna wale wanaziweka wanapojua wao na ndo maana huwa silambi vidole nihesabu hela, nainusa kwanza hela nijue kama ilihifadhiwa sehemu nisiyoweza kupata kipindupindu). Maarifa ninayoyapata kila ninaposoma chochote unachoandika basi ni fahari sana kwangu.

Muziki sasa, ilipopigwa pini JF nilikosa jinsi, nilijua wapo waliohamia Kenya, kuhama ni mchakato na wazee kama mimi kuhama inachukua muda, kuhamisha hamu kuzipeleka sehemu nyingine ni mchakato. Sitoandika nikuchoshe, itose tu kusema kama mwanzo kipengele hiki kimerudi. Asante na uwe na wiki njema

 
Nilimiss mambo haya binamu jamani
Muziki: Kama Mwanzo

....itoshe tu kusema nililikukumbuka wewe Kapuku unayelifanya Jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo. Uwepo wako hapa unaweza usiwe unaniingizia pesa mkononi (wengine huwa wanaweka pesa mfukoni, tunatofautiana, wengine wanaweka kwenye matiti, nimesema tunatofautiana na hakuna ubaya ili kuna wale wanaziweka wanapojua wao na ndo maana huwa silambi vidole nihesabu hela, nainusa kwanza hela nijue kama ilihifadhiwa sehemu nisiyoweza kupata kipindupindu). Maarifa ninayoyapata kila ninaposoma chochote unachoandika basi ni fahari sana kwangu.

Muziki sasa, ilipopigwa pini JF nilikosa jinsi, nilijua wapo waliohamia Kenya, kuhama ni mchakato na wazee kama mimi kuhama inachukua muda, kuhamisha hamu kuzipeleka sehemu nyingine ni mchakato. Sitoandika nikuchoshe, itose tu kusema kama mwanzo kipengele hiki kimerudi. Asante na uwe na wiki njema

 
Tafasiri Unavyoweza: Cheo Cha Uwezo, Madaraka ya Kujipendekeza

....kwanza nitangaze maslahi kabla sijaandika hiki ninachotaka kuandika. Maslahi yenyewe ni kuwa ninamiliki kadi ya kupigia kura ni raia mkamilifu, ninayelipa kodi na hivyo ninategemea kodi yangu isiishie kulipa mishahara wengi wasiowajibika. Ninataka kuona kodi yangu ikiboresha huduma za kijamii nchini, ninataka kodi yangu niione ikijenga barabara. Na zaidi ninapenda kuona kodi yangu ikimfanya rais awajibike kwa wote sababu ikiwa ni kuwa yeye halipi kodi. Tafasiri Unavyoweza.

Kuna tofauti ya cheo na madaraka, hilo lazima ulifahamu na kabla hujafanya juhudi za kuniuliza tofauti nitajitahidi kukuelekeza maktaba zilizo karibu yako ukafanye utafiti kulijengea uwezo swali lako. Majuzi tumeona mabadiliko kidogo serikalini na pia tumeona dege kubwa likitua nchini. Mabadiliko chanya ni jambo zuri na uwepo wa usafiri timamu wa anga nalo ni jambo zuri. Shida inakuja pale mteuaji anapoteua mtu kwa sababu tu ya kutoa maneno yanayomfurahisha bwana mkubwa.

Uongozi ulio timamu wa dola una sifa moja kubwa, unaundwa na wanaokukubali na wanaokupinga wana nafasi ya kuwemo. Ukiwa na watu wanaosema ndiyo mzee usitegemee mabadiliko yenyemaana sana maana hawana jipya, badala ya kukushauri wewe ndo unawashauri na kazi yao inabaki ni kunyanyua kichwa toka chini kwenda juu. Kuna tofauti ya uwezo na madaraka ya kujipendekeza. Tafasiri unavyoweza
 
Nimerudi tena wadau baada ya ratiba kubadilika kiaina na sasa wiki hii imetengemaa angalau naweza kukaa chini na kuchangia sehemu hii ninayoipenda kupita maelezo.

Sitaki kuuliza kama kuna jipya ila kutoka kwangu, niliwakumbuka sana wadau mnaolifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo
Shikamoo binamu
Tulikumiss pia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom