Makapuku Forum

Makapuku Forum

Miotoooooo jiotoooooo
Mamaa hivi wingi wa moto nini ??
tapatalk_1528367536799.jpeg
 
Tafasiri Unavyoweza: Cheo Cha Uwezo, Madaraka ya Kujipendekeza

....kwanza nitangaze maslahi kabla sijaandika hiki ninachotaka kuandika. Maslahi yenyewe ni kuwa ninamiliki kadi ya kupigia kura ni raia mkamilifu, ninayelipa kodi na hivyo ninategemea kodi yangu isiishie kulipa mishahara wengi wasiowajibika. Ninataka kuona kodi yangu ikiboresha huduma za kijamii nchini, ninataka kodi yangu niione ikijenga barabara. Na zaidi ninapenda kuona kodi yangu ikimfanya rais awajibike kwa wote sababu ikiwa ni kuwa yeye halipi kodi. Tafasiri Unavyoweza.

Kuna tofauti ya cheo na madaraka, hilo lazima ulifahamu na kabla hujafanya juhudi za kuniuliza tofauti nitajitahidi kukuelekeza maktaba zilizo karibu yako ukafanye utafiti kulijengea uwezo swali lako. Majuzi tumeona mabadiliko kidogo serikalini na pia tumeona dege kubwa likitua nchini. Mabadiliko chanya ni jambo zuri na uwepo wa usafiri timamu wa anga nalo ni jambo zuri. Shida inakuja pale mteuaji anapoteua mtu kwa sababu tu ya kutoa maneno yanayomfurahisha bwana mkubwa.

Uongozi ulio timamu wa dola una sifa moja kubwa, unaundwa na wanaokukubali na wanaokupinga wana nafasi ya kuwemo. Ukiwa na watu wanaosema ndiyo mzee usitegemee mabadiliko yenyemaana sana maana hawana jipya, badala ya kukushauri wewe ndo unawashauri na kazi yao inabaki ni kunyanyua kichwa toka chini kwenda juu. Kuna tofauti ya uwezo na madaraka ya kujipendekeza. Tafasiri unavyoweza
Ankoo heshima yakoo jaman
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom