Magazetiii soon ...kwa udhamini mnono wa binamu wangu jamaa langu la faida lenye busara sema shida yake moja kubwa hapendii kupitwa na chochote kizuriiiii ....

Muziki: Jana Sio Zamani
Hata huwa sijui zamani inaanzia lini lakini nina uhakika kabisa jana au juzi haiwezi kuwa zamani maana unaweza kukimbia na ukaifikia jana. Kama huamini hilo sio tatizo langu na kuonesha kuwa hili si tatizo langu ninakusalimia kapuku mwenzangu na kukuambia kuwa nilikuwa na siku njema.
Asante sana anko Lyon Lee kwa magazeti, unalifanya jukwaa hili kuwa zuri sana tunapoamka. Nikushukuru husna muba kwa kuja tena, nilikumiss sana. Simu yangu alikuwa nayo anko kwa hiyo kwa yale utakayoyasoma kuhusu lolote jua kabisa sikuwa mimi.
Muziki sasa, ninafurahi sana kukuona hapa Transcend , BlessedHope , Tumosa , Shunie mama wa Biko, Mkushi wa kusi , mzeewakungoa , Mndali ndanyelakakomu SHIMBA YA BUYENZE na wewe kapuku unayenifanya nije hapa kila wakati
Jumatano nzurii kwa wale wote tuliobahatika kuiona na wenzangu na mim ni siku muhimu sana siku ya majivu na tumkumbuke Baba Muumba wetu kwa kutenda mazuriii....
![]()
Magazetiii soon ...kwa udhamini mnono wa binamu wangu jamaa langu la faida lenye busara sema shida yake moja kubwa hapendii kupitwa na chochote kizuriiiii ....
Tuwe na siku njema ...
Na mimi leo nimeamua kufata mawazo ya binamu wangu Obe ...make kanambia mfano ujitoe ufahamu Valentine' flower ukijibana 30,000...Valentine dinner kitu cha kuanzia 50,000
UEFA CHAMPIONS LEAGUE mechi kubwa kwenye vibanda vyetu ni buku aka elfu 1 ...cha kufia nini nawatakia mpira mwema ....
Ahsante kwa mziki mzuri Obe
Love you my baby girlMama shikamoo
Muziki: Jamii na Kujamiiana
...nianze kwa kukutakia Jumatano nzuri ya majivu, kwa sasa kuna watu watatulia kwa kaucha kunywa pombe na kuamsha tamaa zao za mwili wakazihamishia kwa wengine, sio mmoja kama inavyotakikana bali kupunguzia tamaa za mwli kwa wengine hata kama hamko pamoja ila mmekubaliana. Nakusalimia Kapuku mwenzangu na kukutakia Valentine's day njema pia ambayo ndo inaishiria kwa sasa na ninaamini kabisa upo panapostahili kuwepo muda huu, chumbani.
Nilikuwa naongea na mjomba wangu na baada ya kuona sasa anataka damu nyeupe akaingia zinapopatikana na akawka miadi na ili kuikamilisha ikabidi apate upembuzi yakinifu wa gharama zitakavyokuwa. Kununua ua, kulipia meza maalum na kulipia malzi (hakupanga kurudi kwake), gharama ikawa ni milioni 22 tu, pesa za kitanzania. Hamad, kuona hivyo mjomba wangu akakumbuka kuwa leo kuna mechi za uefa akazima simu na kuamua kwenda kwenye banda umiza kuangalia mpira. Hili banda analipenda maana pembeni yake yupo Zuena mpika chapati mwenye uzuri unaompendeza. Na anko akaagiza afungiwe chapati atakuja kuzichukua game likiisha, maana yake anambeba mwenye chapati na chapati
Muziki sasa, nikutakie kwaresma njema na muendelezo mzuri wa siku ya Wapendanao. Unajua nakupenda