Obe
Platinum Member
- Dec 31, 2007
- 10,282
- 35,645
Tafasiri Unavyoweza: Mwalimu Andaa Raia Mwema
Tunaweza kuwa na uelewa wa nani ni raia mwema, ndiyo, wale walio magereza tunaweza kuwaona kuwa hao si raia wema na ndiyo maana wako jela. Lakini vile vile tunaweza kukubaliana au kutokubaliana kuwa walio uraiani wengi wetu tunastahili kuwa jela kwa sababu tu sheria haijatuona. Ndo uzuri wa sheria zetu, zinaona na wakati mwingine zinaacha kuona na wala hazijapofuka maana kupofuka si kutoona kwa tafasiri ngumu. Tafasiri unavyoweza. Mwalimu usifungwe, andaa raia mwema.
Raia mwema aliyekamilika ni yule anayesimama na kuhoji mamlaka juu ya hatua inazochukua bila kumtaarifu, ujue raia mwema ndo anaipa mamlaka serikali na kama inafanya kwa niaba yake bila kumtaarifu basi ni wajibu wake kufungua mdomo na kuhoji wala si kukaa na kupiga makofi kwa kitu asichoelewa. Raia mwema ni zao la mwalimu mzuri, ndiyo mwalimu wa shule na nyumbani, mwalimu anayemwandaa raia mwema kuwa mpiga kura anayetambua thamani ya kura yake, mwalimu anayemwanadaa raia mwema kujua umuhimu wa kulipa kodi na kuhoji matumizi yake, mwalimu anayemwandaa raia mwema kusaka maarifa na kuwa mhojaji (inquisitive).
Tafasiri unavyoweza, mwalimu mwandae raia mwema ambaye anaweza kubuni na kuleta maendeleo yatakayolinufaisha taifa zima na wakati huo huo faida itakayopatikana isishikiriwe na wachache bale wote tufaidike nayo (a privatized profit while the risks and failures are communalized). Mwalimu una nafasi na kama unadhani mwalimu ni yule anayekaa darasani basi unaweza kutafasiri unavyoweza maana leo ni mwalimu kumuandaa raia mwema.
Tunaweza kuwa na uelewa wa nani ni raia mwema, ndiyo, wale walio magereza tunaweza kuwaona kuwa hao si raia wema na ndiyo maana wako jela. Lakini vile vile tunaweza kukubaliana au kutokubaliana kuwa walio uraiani wengi wetu tunastahili kuwa jela kwa sababu tu sheria haijatuona. Ndo uzuri wa sheria zetu, zinaona na wakati mwingine zinaacha kuona na wala hazijapofuka maana kupofuka si kutoona kwa tafasiri ngumu. Tafasiri unavyoweza. Mwalimu usifungwe, andaa raia mwema.
Raia mwema aliyekamilika ni yule anayesimama na kuhoji mamlaka juu ya hatua inazochukua bila kumtaarifu, ujue raia mwema ndo anaipa mamlaka serikali na kama inafanya kwa niaba yake bila kumtaarifu basi ni wajibu wake kufungua mdomo na kuhoji wala si kukaa na kupiga makofi kwa kitu asichoelewa. Raia mwema ni zao la mwalimu mzuri, ndiyo mwalimu wa shule na nyumbani, mwalimu anayemwandaa raia mwema kuwa mpiga kura anayetambua thamani ya kura yake, mwalimu anayemwanadaa raia mwema kujua umuhimu wa kulipa kodi na kuhoji matumizi yake, mwalimu anayemwandaa raia mwema kusaka maarifa na kuwa mhojaji (inquisitive).
Tafasiri unavyoweza, mwalimu mwandae raia mwema ambaye anaweza kubuni na kuleta maendeleo yatakayolinufaisha taifa zima na wakati huo huo faida itakayopatikana isishikiriwe na wachache bale wote tufaidike nayo (a privatized profit while the risks and failures are communalized). Mwalimu una nafasi na kama unadhani mwalimu ni yule anayekaa darasani basi unaweza kutafasiri unavyoweza maana leo ni mwalimu kumuandaa raia mwema.
