Muziki: Huhitaji Leseni Kuendesha, Funga Mkanda
Maisha yanakwenda kasi sana, kataa kubali maana sijauliza swali ujibu ndiyo au hapana. Ukweli unabaki kusimama muda wote na uongo hata ukisimama si muda mrefu utachutama kabisa na kwa aibu kubwa. Ninakusalimia wewe Kapuku ambaye unalifanya Jukwaa hili kuwa sehemu nzuri ya kuwepo, nipo kwa sababu wewe upo. Asante sana.
Nilikuwa najisomea gazeti na nilivutiwa na katuni, yeah, ninapenda kuangalia katuni na kuzisoma, huwa zinawasilisha ujumbe kwa maana kubwa sana. Sote tunajua kuendesha kiuhalali kunahitaji kwanza upitie mafunzo (namaanisha kuendesha barabarani), upate majaribio na kisha ndo unaruhusiwa kukata leseni, hapo utaitwa dereva kamili na una nafasi ya kutumia barabara pamoja na watumiaji wengine. Lakini si kila anayeendesha kaipitia hizo hatua, wengine unakuwa umekula mlo mbaya na unasikia leo ninaendesha na sifungi mkanda kama dereva mwingine na ninapoendeshea nakuwa peke yangu nguo ya ndani magotini
Muziki sasa, furahia muziki maana kesho ikimpendeza Manani ni furahiday