
Tuombe*
Baba uliyeketi mahali palipo inuka,
Tunasema asante kwa kutupa kibali cha kuiona siku hii mpya siku ambayo kuanzia kuumbwa kwa dunia haijawahi kuwepo.
Wengi walikuwa wamepanga kuiona siku hii lakini Baba hawakufanikiwa kuiona.
Ila sisi Baba kwa rehema zako na upendo wako tumeweza kuiona.
Baba tunajua ya kwamba sisi sio bora sana hadi tuweze kufika siku kama hii bali Baba unakusudi lako juu yetu.
Baba tembea na kila mmoja katika mapito yake ya kila siku
Mungu angalia hitaji la Baba huyu ukapate kumbariki
Baba angalia hitaji la Mama huyu ukapate kumsaidia sawasawa na haja ya moyo wake.
Mungu kutana na hitaji la kijana huyu
Mungu kutana na hitaji la binti huyu
Mungu kutana na hitaji la Mjane/mgane huyu
Mungu kutana na hitaji la mkulima huyu.
Mungu kutana na hitaji la mfanyakazi huyu
Mungu kutana na hitaji la wagonjwa hawa.
Mungu kutana na hitaji la hawa ambao hawana kazi
Bwana wabariki na uwaonekanie katika mapito yao.
Mungu wabariki Wachungaji na Wahubiri wote wanaolihubiri jina lako takatifu.
Asante Bwana kwa kuwa utaenda kutenda sawasawa na upendavyo.
Nikatika jina la YESU KRISTO TUNAOMBA,TUNAAMINI NA KUSHUKURU
*AMENI*