....kijana wa Sunday skuli mimi na chuo nimesoma, sio kwa fimbo zile ila zimeniwezesha kupata ufahamu wa kupiga mpunga bila kijiko.
Nyumba yangu ya ibada imebadilishwa badilishwa sana, mara bar kutegemea na muandamo wa mwezi

...Jackie Cheni anaweza kumharibu Bruce Lee? Au Chuck Norris anaweza kumharibu komandoo suzi Cynthia Rothrock

..hapana, muulize, hapa ni mwendo wa mapambio na singeli tu

MmhI feel you aunty, ni moja ya nyimbo ambayo imeimbwa ikiwa na kila vionjo vinavyotakiwa kuwasilisha ujumbe, pathos na logos.
Ukimaliza kulia kumbuka kutuma sadaka
HahahaUsiku mwema wadau, hii wiki imekuwa mbovu sana kwangu. Naamini jua litawaka tena
hebu fikiria, Chelsea kapigwa 3 mtungi na Real Madrid kapigwa Three Suitors One Husband
![]()
Tuko na singeli saa hizi mazoeziAnko akiwa anawashwawashwa kuitafuta furahi deii ambayo anaamini ndo siku muhimu kuliko zote make ndo siku anayopewa self service ila hajasahau kukusalimia wewe kapuku na mm nikiwepo na kama usku hukuzipata salamu zake mama mchungaji ataziletaa kwa niaba yake make now wapo wanapasha kama ....

Ubarikiwe my SonMuwe na siku njema wapendwa
Tuombe*
Sawa sawa mama mimi nakusalimia sanaTuko na singeli saa hizi mazoezi![]()
Amina mamaTuombe*
Baba uliyeketi mahali palipo inuka,
Tunasema asante kwa kutupa kibali cha kuiona siku hii mpya siku ambayo kuanzia kuumbwa kwa dunia haijawahi kuwepo.
Wengi walikuwa wamepanga kuiona siku hii lakini Baba hawakufanikiwa kuiona.
Ila sisi Baba kwa rehema zako na upendo wako tumeweza kuiona.
Baba tunajua ya kwamba sisi sio bora sana hadi tuweze kufika siku kama hii bali Baba unakusudi lako juu yetu.
Baba tembea na kila mmoja katika mapito yake ya kila siku
Mungu angalia hitaji la Baba huyu ukapate kumbariki
Baba angalia hitaji la Mama huyu ukapate kumsaidia sawasawa na haja ya moyo wake.
Mungu kutana na hitaji la kijana huyu
Mungu kutana na hitaji la binti huyu
Mungu kutana na hitaji la Mjane/mgane huyu
Mungu kutana na hitaji la mkulima huyu.
Mungu kutana na hitaji la mfanyakazi huyu
Mungu kutana na hitaji la wagonjwa hawa.
Mungu kutana na hitaji la hawa ambao hawana kazi
Bwana wabariki na uwaonekanie katika mapito yao.
Mungu wabariki Wachungaji na Wahubiri wote wanaolihubiri jina lako takatifu.
Asante Bwana kwa kuwa utaenda kutenda sawasawa na upendavyo.
Nikatika jina la YESU KRISTO TUNAOMBA,TUNAAMINI NA KUSHUKURU
*AMENI*
Naomba nitumie zisiwe youtubeSawa sawa mama mimi nakusalimia sana
Mwanao kama hajakutumia nitume