Makapuku Forum

Makapuku Forum

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 27
ILIPOISHIA:
Nilipokuja kushtuka, nilijikuta nikiwa nimelala kitandani, mapigo yangu ya moyo yakinienda mbio kuliko kawaida, nikiwa nimeunganishwa mashine ya kunisaidia kupumua huku mwili wangu ukiwa umeunganishwa na vifaa vingi vya kitabibu, milio ya mashine mbalimbali ikisikika ndani ya chumba kile ambacho hata bila kuuliza, niligundua kwamba ni wodini.
“Amefumbua macho! Dokta... amefumbua macho! Njooni haraka!”
SASA ENDELEA...

Harakaharaka madaktari wengi waliingia ndani ya kile chumba na kuzunguka kitanda changu, kwa mbali nikawa nawatazama mmoja baada ya mwingine, wote wakionekana kukiinamia kitanda changu. Macho yangu yalikuwa na ukungu, hali iliyonifanya nisiwe na uangavu wa kutosha machoni kuwaona ingawa bado nilikuwa na uwezo wa kutambua sura zao.
“Unaendeleaje Jamal?” nilisikia daktari mmoja akiniuliza. Kwa jinsi sauti yake ilivyokuwa ikisikika, ilikuwa mithili ya inayotoka kwenye redio mbovu. Nilijaribu kufumbua mdomo lakini nilishindwa kwani nilikuwa nimeunganishwa na mabomba mengi, mdomoni na puani, nikawa natingisha tu kichwa kuashiria kwamba najisikia vizuri.
Jopo la madaktari waliendelea kunizunguka pale, nikamuona mwingine akinipima kwa kutumia kifaa maalum kusikiliza mapigo ya moyo wangu, mwingine akaniweka ‘thermometer’ kwapani kwa lengo la kunipima joto huku mwingine akiwa bize kufuatilia maandishi yaliyokuwa yanaonekana kwenye mashine inayofanana na kompyuta, iliyokuwa ikipiga kelele kwa kutoa milio ya ‘kubipu’ kila mara.
“He is recovering! His heartbeats are stabilizing, blood sugar is coming to normal and the wound is healing!” alisema daktari mmoja wakati akiwaambia wenzake, kwa kuwa Kiingereza hakikuwa kikinipiga chenga, niliweza kuelewa vizuri kwamba alikuwa akiwaambia wenzake kwamba nimeanza kupata nafuu, mapigo yangu ya moyo yanaimarika, kiwango cha sukari kinarudi kwenye hali ya kawaida na jeraha langu linapona.
Niliwaona wote wakitabasamu na kunitazama usoni, kila mmoja akawa ananipongeza kwamba eti nimepigania vizuri maisha yangu kwa sababu nilikuwa na hali mbaya sana. Daktari mwingine ambaye kiumri alikuwa kijana mdogo, alinitania kwamba eti mimi ndiye binadamu wa kwanza niliyeweza kwenda kuzimu na kurudi, wenzake wote wakacheka.
Japokuwa mwenyewe alizungumza kama utani na wenzake nao wakacheka wakichukulia utani, kile alichokisema hakikuwa utani ingawa siwezi kusema kwamba kule nilikofika ndiyo kuzimu kwenyewe au la lakini ukweli ni kwamba nilikuwa nimefika mahali ambako sidhani kama kuna binadamu aliye hai amewahi kufika.
Kuna muda nilihisi huenda bado nipo kwenye ile hali ya kuuona mwili wangu wakati mwenyewe nikiwa pembeni lakini haikuwa hivyo, ni kweli nilikuwa nimerejewa na fahamu na kila kilichokuwa kinaendelea kilikuwa kikitokea kwenye ulimwengu halisi.
Unajua namna nyepesi ya kujigundua kwamba unaishi kwenye ulimwengu wa kawaida unapoona upo kwenye mazingira ambayo huelewielewi kama upo ndotoni au la, ni kujaribu kupepesa macho, kukunja vidole vya mikono au kuigusa ngozi ya mwili wako kwa kutumia kitu chenye ncha kali.
Ukiona umeweza kupepesa macho, kukunja vidole au umesikia maumivu baada ya kujifinya au kujichoma na kitu chenye ncha kali, basi ujue kwamba haupo ndotoni au kwenye ulimwengu wa tofauti bali upo kwenye ulimwengu halisi. Hicho ndicho nilichokifanya mimi na kweli majibu yalionesha kwamba nilikuwa nimerejea kwenye ulimwengu wa kawaida.
Madaktari waliendelea kujadiliana na mwisho walifikia muafaka wa kuamua kunipunguza baadhi ya vifaa mwilini mwangu, ikiwemo mirija ya kunisaidia kula pamoja na ile ya kutolea haja ndogo kwani kwa kipindi chote nilichokuwa sina fahamu, kila kitu kilikuwa kikifanyika kwa msaada wa mirija.
Hilo lilifanyika, kitu pekee kilichoachwa mwilini mwangu ilikuwa ni mashine ya kunisaidia kupumua ambayo nayo walikubaliana kwamba niendelee kuitumia kwa muda lakini nitakapofikia hatua ya kuweza kupumua mwenyewe vizuri, wataitoa.
Niliwaona madaktari wote wakiwa na nyuso za furaha sana mle ndani ya wodi yangu, tofauti kabisa na kipindi nilipokuwa nikiwatazama kutokea pembeni kabla sijarejewa na fahamu ambapo kila mmoja alikuwa akionesha sura ya kukata tamaa.
“Vipi Jamal, unajisikiaje?” nesi mmoja wa kike aliniuliza kwa sauti ya upole wakati akinisafisha mwili wangu kwa kutumia kitambaa laini kilichokuwa kimewekwa kwenye kopo lenye maji ya uvuguvugu.
Nikamjibu kwa sauti ya chini kwamba nilikuwa najisikia vizuri, akaendelea kunifutafuta uso wangu, hasa kwenye yale maeneo niliyokuwa nimebandikwa bandeji za kushikilia ile mirija iliyotolewa. Yule nesi aliendelea kunipigisha stori za hapa na pale, huku mara kwa mara akiingizia utani ambao nilielewa kwamba ulikuwa ni kwa lengo la kunichangamsha.
Unajua jambo ambalo watu wengi hawalijui, madaktari, manesi na wauguzi, huwa wanafundishwa saikolojia ya namna ya kucheza na akili za mgonjwa na kumfanya ajisikie amani ndani ya moyo wake na kuamsha upya matumaini ya kupona, hata kama alikuwa mahututi.
Ndiyo maana ni nadra sana kumuona daktari aliyesomea vizuri kazi yake na kuhitimu, akimfokea mgonjwa au kuzungumza naye kwa lugha isiyo rafiki. Fuatilia kwa makini, madaktari karibu wote, wa hospitali za binafsi na za serikali, huwa wanakuwa wapole sana wanapozungumza na wagonjwa wao, hata kama una tatizo kubwa, atakupa maneno laini ya kishujaa yatakayokufanya uamini kwamba lazima utapona.
Hata manesi wale waliofundishwa vizuri na kuelewa, huwa wapole sana kwa wagonjwa kwa sababu wamefundishwa hivyo. Ukiona nesi anawabwatukia wagonjwa wake, anawatolea lugha chafu na za matusi, wengi wanakuwa ni wale ambao wameingia kwenye fani hiyo kwa njia za kiujanjaujanja, pengine wamefoji vyeti au vyuoni walifeli lakini wameingizwa kwa migongo ya ndugu zao au kwa kutoa rushwa.
Basi yule nesi aliendelea kunipa maneno matamu, eti akawa ananisifia kwamba japokuwa nilikuwa nimepoteza fahamu kwa muda mrefu, eti bado nilikuwa naonekana ‘handsome’, nikashindwa kujizuia na kuachia tabasamu hafifu.
Akaniambia eti kama angekuwa hana aibu za kikekike, angenitongoza ili nimuoe, nikazidi kuachia tabasamu pana kwani sijawahi kusikia eti mwanamke anamtongoza mwanaume amuoe, japokuwa anaweza tu kumrahisishia mazingira ya kumpata, nikajikuta nikivutiwa naye kwani ukiachilia mbali masihara yake, pia alikuwa na sura nzuri ya kuvutia na umbile lililokaa kikekike haswaa!
“Yaani sikomi tu, tamaa za wasichana warembo na huruma zangu ndiyo iliyonifanya niingie kwenye mtego wa Shenaiza, hata kupona vizuri bado nimeanza kumzimikia nesi,” nilijisemea mwenyewe moyoni na kuzidi kutabasamu.
Alizidi kunipigisha stori mpaka nikaona ile mashine ya kunisaidia kupumua kama inaninyima uhuru, nikamuomba aitoe ili nijaribu kupumua mwenyewe, akafanya hivyo na kwa bahati nzuri, tayari nilikuwa na uwezo wa kupumua mwenyewe vizuri, madaktari wakazidi kufurahi na kushauri kwamba kwa kuwa nilikuwa na hali nzuri, nihamishiwe kwenye wodi za kawaida kwa sababu kwa muda wote huo, bado nilikuwa kwenye wodi ya wagonjwa mahututi (ICU).
Mipango ilianza kuandaliwa na hatimaye nilihamishiwa kwenye wodi ya wanaume ambapo nilipoingizwa tu, ndugu, jamaa na marafiki walianza kufurika kwa wingi kuja kuniona kwani fursa hiyo waliikosa nilipokuwa ICU kwa sababu kule huwa ndugu hawaruhusiwi kumuona mgonjwa ambaye yupo kwenye hali mbaya kama niliyokuwa nayo mimi, labda kama kuna sababu maalum.
Miongoni mwa watu wa mwanzomwanzo kabisa kuja kuniona, alikuwa ni Raya ambaye hakuamini kabisa aliponiona nikiwa nimefumbua macho, akanikumbatia kwa nguvu pale kitandani bila kujali dripu niliyokuwa nimeunganishwa, akawa ananibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu huku akiangua kilio kwa nguvu.
“Nilijua nimekupoteza mpenzi wangu, ooh ahsante Mungu! Ahsante Mungu,” alisema Raya, ikabidi niinue ule mkono ambao haukuwa na dripu nikaupitisha mgongoni kwake na kumkumbatia, nikambusu shavuni, kitendo ambacho kwa kiasi kikubwa kilimfariji sana.
Japokuwa mwili wangu haukuwa na nguvu, ilikuwa ni lazima nifanye hivyo kwa sababu kusema ukweli, tangu nipatwe na matatizo, Raya alionekana kuguswa pengine kuliko mtu mwingine yeyote.
Niliamini uchungu ambao alikuwa nao msichana huyo, ungekuwa sawa na wa mama yangu endapo angefahamu kilichokuwa kimenitokea mwanaye lakini kwa kuwa wazazi wangu hawakuwa wakijua chochote kutokana na mazingira ambayo mimi mwenyewe ndiye niliyeyatengeneza (nitafafanua kuhusu hili baadaye), Raya ndiye aliyesimama kwenye nafasi ya mama yangu.
Kingine nilichojifunza, ni kuacha kuhukumu watu wote kwambe eti siku hizi duniani hakuna tena mapenzi ya kweli! Siyo sahihi kabisa, kuna watu wana mapenzi mpaka shetani mwenyewe anayaogopa, mmoja wapo akiwa ni Raya.
Niliendelea kumkumbatia msichana huyo huku marafiki na jamaa zangu wengine wakiwa pembeni wakitutazama, tukiwa kwenye hali hiyo, nilisikia mlango wa wodi ukifunguliwa na mtu akaingia mbiombio mpaka pale kitandani kwangu, nikashtuka na kumuachia Raya, Raya naye akainua uso wake, watu wote tukawa tunamtazama kwa mshangao mtu yule aliyeingia, tukiwa ni kama hatuamini.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 28
ILIPOISHIA:
Niliendelea kumkumbatia msichana huyo huku marafiki na jamaa zangu wengine wakiwa pembeni wakitutazama, tukiwa kwenye hali hiyo, nilisikia mlango wa wodi ukifunguliwa na mtu akaingia mbiombio mpaka pale kitandani kwangu, nikashtuka na kumuachia Raya, Raya naye akainua uso wake, watu wote tukawa tunamtazama kwa mshangao mtu yule aliyeingia, tukiwa ni kama hatuamini.
SASA ENDELEA...

Hakuwa mwingine, bali Shenaiza ambaye alikuwa amevaamavazi ya hospitalini hapo kuonesha kwamba alikuwa amelazwa, mkononi akiwa na sindano iliyofungwa na plasta, nafikiri kwa ajili ya kumuingizia dawa au kumtundikia dripu, nikawa namtazama usoni, naye akawa ananitazama.
“Jama! Kumbe ni kweli hujafa?” alisema Shenaiza kwa sauti ya kukwamakwama, wote tukatazamana tena kisha nikageuka na kumtazama Shenaiza, alionesha kabisa kwamba hakuwa sawa, nikawa najiuliza maswali mengi kichwani ambayo sikuwa na majibu yake.
Nilikumbuka kwamba kuna muda mimi na Shenaiza tulikuwa tumnekaa siti moja kwenye treni la ajabu, tukielekea kusikojulikana, giza likiwa limetanda kila sehemu. Kama mimi nilikuwa kitandani, wodini, na Shenaiza naye alikuwa hospitalini hapo akiwa amelazwa, ina maana kwamba mimi na yeye tulikutana wapi?
Nilikumbuka pia kwamba yeye mwenyewe aliniambia kwamba ameamua kuyakatisha maisha yake kwa kujiovadozi dawa ya usingizi, na kwamba aliamua kufanya hivyo kama njia ya kupumzika na mateso aliyokuwa anayapata, sasa Shenaiza aliyejiua ni nani na huyo aliyekuwa amesimama mbele yangu ni nani?
Nilihisi kama kichwa kinapata moto kwa sababu ya utata wa kilichokuwa kinaendelea, hata hivyo nilipoemndelea kutuliza kichwa changu, nilianza kupata baadhi ya majibu.
“Kumbe kweli hukufa?” Shenaiza aliniuliza tena swali lile ambalo lilinizindua kutoka kwenye lindi la mawazo.
“Hebu naomba mtupishe kidogo nizungumze na Shenaiza,” niliwaambia watu wote waliokuwa wamenizunguka pale wodini lakini Raya alikataakatakata.
“jamal! Are you out of your mind?” (Jamal umechanganyikiwa) alisema raya kwa sauti ya juu. Akaendelea kuniambia kwamba Shenaiza ndiye aliyekuwa chanzo cha mimi kutaka kupoteza maisha, iweje leo nimuone yeye ndiyo wa maana kiasi c ha kuwataka watu wote watoke nje?
“Kama amekuja kwa lengo la kukumalizia je? Mimi siendi popote, nitakaa hapahapa kukulinda,” alisema Raya huku akionesha kutokuwa na hata chembe ya masihara, nikashindwa cha kufanya.
Wale watu wengine wote walitoka lakini kama Raya alivyosema, hakutaka kuinuka pale pembeni ya kitanda changu alipokuwa amekaa na mimi sikuona sababu yoyote ya kumlazimisha.
Bado tulikuwa tukiendelea kutazamana na Shenaiza, kadiri nilivyokuwa nazidi kumtazama ndivyo nilivyokuwa naendelea kukumbuka mambo mengi yaliyotokea kwenye ulimwengu usio wa kawaida na kwenye ulimwengu wa kawaida.
“Haya sema shida yako iliyokuleta,” Raya alivunja ukimya, Shenaiza akashusha pumzi ndefu na kusogea kwenye kitanda nilichokuwa nimelazwa.
‘Samahani dada wala mimi sijaja hapa kwa nia mbaya, kwanza nimejikaza tu kwani bado naumwa sana, nimetoroka tu wodini baada ya kusikia Jamal yupo hapa,” alisema Shenaiza kwa sauti ya chini, nikamuona Raya naye akishusha pumzi kwani alishajiandaa kwa shari lakini msichana huyo akaonesha kwamba hakuwa amekuja kisharishari.
“Nilisikia kwamba umekufa na mimi nilithibitisha hilo,” alisema Shenaiza kwa upole, nikamuliza amesikia wapi na amethibitishaje hilo?
“Niliambiwa na daktari mmoja kati ya wale waliokuwa wanakutibu, akaniambiakwamba ulishakata roho lakini walikuwa wamekuunganisha kwenye mashineya kusaidia moyo wako uendelee kudunda, akanihakikishia kwamba saa chache baadaye watakutoa kwenye mashine hiyo.
“Mh! Sikuelewi! Raya wewe unamuelewa anachokisema huyu?”
“Mimi namuelewa, ni kweli hata mimi daktari aliniambia kwamba huwezi kupona,” alisema Raya na kunifanya nikose cha kujibu, nikawa nawatazama mmoja baada ya mwingine usoni kwa zamu. Unajua miongoni mwa mambo ambayo sikuwa nataka kuyasikia, ni kwamba eti watu wote walikuwa wanajua kwamba nimekufa.
“Halafu kuna mambo yananichanganya sana kichwa changu, sijui ni ndoto, maruweruwe au uchawi hata sielewi. Mbona nakumbuka kama mimina wewe kuna sehemu tulikutana halafu tukaongea mambo mengi tu? Na kubwa zaidi mbona nakumbuka kama na mimi nilikufa?”
Swali hilo la Shenaiza liliunga kabisa na kile nilichokuwa nakifiria kichwani mwangu muda wote. Ni kweli hata mimi nilikuwa najua kwamba kuna sehemu mimina Shenaiza kuna sehemu tulikuwa pamoja na tukazungumza mambo mengi tu pamoja, tena tukiwa tumekaa kwenye siti moja kwenye treni la ajabu.
“Utakuwa ulikuwa unaota, ulikutana wapi na Jamal wakati tangu siku ile ulipomsababishia atake kufa hajainuka kitandani na leo ndiyo amefumbua macho?” Raya aliingilia mazungumzo yale, sote tukawa tunamtazama kwa sababu hakuwa akijua chochote.
“Mh! Inawezekana kweli nilikuwa naota, kwa sababu katika maisha yangu sijawahi kupanda treni hata siku moja lakini nakumbuka eti tulikuwa tumekaa kwenye siti mojaya treni,” alisema Shenaiza na kuzidi kunihakikishia kwamba kumbe kile kilichotokea kilikuwa ni jambo halisi, Raya akazidi kubisha.
“Sasa mtu yupo kitandani anaumwa hoi hajitambui atapandaje treni? Dada ulikuwa unaota na sidhani kama Jamal anahitaji kusikia ndoto zako, kama hicho ndicho kilichokuleta naomba uondoke, mgonjwa anahitaji kupumzika,” alisema Raya kwa msisitizo.
“Basi tuachane na hayo, Jamal nimekuja kukuomba msamaha!”
“Msamaha wa nini Shenaiza?”
“Kwa yote niliyokufanyia. Haikuwa kusudioa langu kukuingiza kwenye matatizo, najua wewe na watu wako wote wa karibu mnanichukia sana.”
“Msamaha wako una maana gani leo? Kama angekuwa amekufa ungemuomba nani msamaha? Dada hebu nakuomba uondoke,” Raya alijibu kwa ukali, nikamuona Shenaiza akijiinamia na kuanza kuangua kilio.
“Wewe! Kwa nini unatusumbua kukutafuta? Kwa nini unatoka wodini bila taarifa wakati unajua hali yako siyo nzuri? Unatusababishia matatizo kwa ndugu zako,” manesi wawili waliingia mbiombio mle wodini, akawamshika Shenaiza huku an kule na kumtoa msobemsobe huku mwenyewe akiendelea kuangua kilio. Mimi na Raya tukatazamana!
“Inaonesha mnafahamiana kuliko hata mimi ninavyojua, huyu si mmekutana juzijuzi tu hapo, mbona inaonesha kama kuna kinachoendelea nyuma ya pazia?” Raya aliniuliza, akionesha dhahiri kuwa na wivu mkali ndani ya moyo wake, nikashindwa cha kumjibu.
“Jamal, nakupenda sana mpenzi wangu, nakuomba uamini ninachokisema. Sijawahi kumpenda mtu yeyote katika maisha yangu na wewe mweyewe ni shahidi kwamba umenikuta nikiwa simjui mwanaume yeyote.
“Niliamua kukupa zawadi ya kuwa mtu wa kwanza kunijua na nataka uwe wa mwisho kwangu, nataka unioe tuishi pamoja milele Jamal,” alisema Raya huku machozi yakimlengalenga.
Kiukweli na mimi nilikuwa nimetokea kumpenda Raya baada ya kuwa nimeutezsa moyo wake kwa kipindi kirefu na kweli nilishaanza kuweka mnalengo ya maisha yangu ya baadaye nikiwa naye lakini niliona kama huo siyo muda muafaka wa kuzungumzia mapenzi.
Ndiyo kwanza nilikuwa nimerejea kwenye ulimwengu wa kawaida, bado kuna maswali mengi ambayo sikuwa nimeyapatia majibu, kuhusu mimi mwenyewe na pia kumhusu Shenaiza na familia yake.
Hata hivyo, sikutaka Raya ajisikie vibaya kwa namna yoyote, mwenyewe nilishajiwekea nadhiri moyoni kwamba nitakuwa sehemu ya furaha ya raya, hasa baada ya kugundua ni kwa kiasi gani alikuwa akinipenda.
Nikamkumbatia na kubusu kwenye paji lake la uso, nikamwambia hakuna chochote kinachoendelea kati yangu na Shenaiza isipokuwa ilikuwa ni lazima niendelee kuwa naye karibu kwa sababu kuna mambo muhimu ilikuwa ni lazima niyajue, hasa kuhusu baba yake Shenaiza.
“Kuna kazi nimepewa ya kuhakikisha namzuia baba yake Shenaiza hicho anachokifanya, na ni lazima nitimize.”
“Kazi? Nani aliyekupa hiyo kazi? Halafu umzuie kwani anafanya nini na wewe umejuaje?” Raya alinibana kwa maswali, nikawa nashindwa hata namna ya kumjibu.
Je, nini kitafuatia?
 
Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 29
ILIPOISHIA:
“Kuna kazi nimepewa ya kuhakikisha namzuia baba yake Shenaiza hicho anachokifanya, na ni lazima nitimize.”
“Kazi? Nani aliyekupa hiyo kazi? Halafu umzuie kwani anafanya nini na wewe umejuaje?” Raya alinibana kwa maswali, nikawa nashindwa hata namna ya kumjibu.
SASA ENDELEA...

“Si naongea na wewe Jamal!”
“Aah! Unajua ni stori ndefu kidogo na... na... ni...” nilijikuta nikishikwa na kigugumizi, Raya alikuwa akinitazama huku amenikazia macho. Nadhani kuna mambo alianza kuhisi kama hayaendi sawa.
Nilichokifanya ilikuwa ni kumzugazuga na kubadilisha mada, nikamhakikishia kwamba nitakapokaa na kutulia nitamueleza kwa kirefu kila kitu kilichokuwa kinaendelea. Bado Raya alionesha kutoridhishwa na maelezo yangu na kikubwa kilichokuwa kikimsumbua ilikuwa ni wivu.
Kwa sababu kihistoria alishajenga mawazo akilini mwake kwamba mimi simpendi isipokuwa yeye ndiyo analazimisha mapenzi, alikuwa akiteseka sana ndani ya moyo wake akiamini kwamba akitokea mwanamke ambaye nitampenda, kama alivyokuwa akihisi kwa Shenaiza, nitamuacha jumla, jambo ambalo hakuwa tayari kuona linatokea.
“Halafu kuna mambo yananichanganya sana kichwa changu, sijui ni ndoto, maruweruwe au uchawi hata sielewi. Mbona nakumbuka kama mimi na wewe kuna sehemu tulikutana halafu tukaongea mambo mengi tu? Na kubwa zaidi mbona nakumbuka kama na mimi nilikufa?” kauli aliyoitoa Shenaiza muda mfupi uliopita ilijirudia ndani ya kichwa changu, nikawa natazama juu darini nikitafuta majibu ya maswali yangu.
Alichokisema Shenaiza ndicho kilichokuwa ndani ya akili yangu, ni kweli mimi na yeye kuna sehemu tulikutana na tukaongea mambo mengi tu, akanieleza kwamba ameamua kujiua kwa kujiovadozi madawa ya kulevya, akanihakikishia na mimi kwamba nilikuwa nimekufa lakini nikawa nambishia.
Shauku ya kutaka kufahamu zaidi kuhusu kilichotokea, ilinisukuma kuweka nadhiri ndani ya moyo wangu kwamba lazima nimtafute tena Shenaiza ili tuzungumze kwa kina, huenda mwenzangu alikuwa anaelewa kilichotokea kwa ufasaha zaidi.
Raya aliendelea kunisemesha mambo mengi lakini nikiri kwamba akili yangu haikuwa pale wodini, nilikuwa nikimfikiria Shenaiza na yote yaliyotokea. Naomba nieleweke kwamba hiyo haikumaanisha kwamba sikuwa nampenda Raya, nilishaamua kuwa naye baada ya kugundua kuwa ananipenda sana lakini kila nilipomfikiria Shenaiza, nilijikuta mwili wangu ukisisimka mno.
Bado kuna swali kubwa halikuwa limepata majibu akilini mwangu, haya yote yaliyokuwa yakitokea kwenye maisha yangu, kuanzia Shenaiza kunipigia simu na baadaye kunieleza kwamba amekosea namba, akaniganda kwamba hata kama amekosea anaomba nimsaidie na yote yaliyofuatia mpaka muda huo niliokuwa wodini.
“Hivi kama Mungu angeamua kuyachukua maisha yangu jumla, ningekufa nikiwa gizani kabisa, nikiwa sielewi chochote kilichosababisha mpaka nikafikwa na mauti? Mimi ni mtu wa ajabu eeh!” nilijikuta nikimuuliza Raya swali hilo, akashusha pumzi ndefu na kunitazama.
“Kwa hiyo kumbe muda wote nilikuwa naongea peke yangu?” alisema Raya huku akionesha kukasirishwa na kitendo cha mimi kuzungumza kitu ambacho hakikuwa na uhusiano wowote na kile alichokuwa akiniongelesha.
Niligundua kwamba nimekosea na kwa kuwa sikutaka kumuudhi Raya, ilibidi nimdanganye kwamba tangu nimerejewa na fahamu zangu, nahisi kichwa changu hakipo sawa kwa hiyo asinielewe vibaya, nikamuona akishusha tena pumzi na kunisogelea, akanibusu na kuninong’oneza:
“Nakupenda sana mpenzi wangu, nakuombea upone kabisa ili tuendelee na maisha yetu,” akanibusu na lipsi zake laini kwenye midomo yangu, akanibusu tena kwenye paji la uso kisha akaniambia kwamba anaenda kuniandalia chakula.
Alipofungua mlango na kutoka, ndugu na marafiki zangu waliokuwa wakisubiri nje, waliingia wodini na kukaa pembeni yangu, tukaendelea na stori za hapa na pale, wengi wakinipa pole kwa kilichotokea. Japokuwa hali yangu ilikuwa ikizidi kuimarika kwa kasi, lakini niliwaona watu wote wakiwa na shauku kubwa ya kutaka kujua nini hasa kilichotokea.
Sikuwa tayari kueleza kila kitu, nikawa nafupisha tu kwamba nilivamiwa na majambazi walionijeruhi vibaya na kunifanya ninuse kaburi. Nilikuwa na sababu maalum za kutoeleza kila kitu kilichotokea, bado nilikuwa na kazi kubwa ya kuifanya.
Muda wa kuona wagonjwa ulipoisha, watu wote waliondoka na kuniacha nikiwa na nesi aliyekuwa akinihudumia tu, huku nikiendelea kumsubiri Raya ambaye aliahidi kwamba ndiyo atakayeniuguza mpaka nipone na kuruhusiwa kutoka wodini.
Kwa kuwa ndiyo kwanza alikuwa ametoka na kwenda kuniandalia chakula kama mwenyewe alivyosema, niliona huo ndiyo muda muafaka wa kumtafuta Shenaiza ili anieleze ukweli wa mambo mengi niliyokuwa nahitaji kuyajua.
“Nesi samahani naomba nikuulize,” nilimuuliza yule nesi mchangamfu aliyekuwa akipenda kunitania.
“Niulize tu honey wangu, nakupenda lakini mume mwenyewe una wanawake kibao, hujui najisikia wivu?” alisema huku akinisogelea, nikajikuta nikicheka kwa sauti. Nilimuuliza kuhusu Shenaiza kama anafahamu wodi aliyolazwa.
Alinipa majibu ambayo yalinishangaza sana, aliniambia kwamba msichana huyo alikuwa amelazwa kwenye wodi ya wagonjwa wa akili na kwamba kuna muda ilikuwa ni lazima wamfunge kamba kwa jinsi alivyokuwa akiwasumbua madaktari na wagonjwa wenzake.
Kiukweli nilishangazwa sana na maelezo hayo kwa sababu muda mfupi uliopita, nilikuwa nimezungumza naye na hakuonesha dalili zozote za kuchanganyikiwa mpaka alipokuja kuchukuliwa kwa nguvu na wale manesi.
Nilimuomba anielekeze vizuri wodi aliyokuwa amelazwa kwa sababu nilikuwa na mazungumzo muhimu naye, akaniambia kwamba utaratibu wa hospitalini hapo hauruhusu. Ilibidi niendelee kumbembeleza ambapo aliniambia atanisaidia kwa sababu ananipenda, akanisaidia kuinuka pale kitandani, tukaongozana kuelekea kwa Shenaiza kama nilivyomuomba.
Njia nzima yule nesi alikuwa akiendelea kunitania kuhusu mambo ya kimapenzi mpaka ikafika kipindi nikawa na wasiwasi kama kile alichokuwa anakisema ni utani au ananifikishia ujumbe kwa njia ya utani! Ukarimu na ucheshi wake, achilia mbali uzuri wa kipekee wa sura na umbo aliojaliwa, vilinifanya nimzoee haraka.
Alinipeleka mpaka kwenye wodi hiyo lakini kutokana na mazingira ya mle ndani, aliniambia nimsubiri hapohapo nje, akaingia na kwenda kuzungumza na manesi wenzake na muda mfupi baadaye, alitoka akiwa na Shenaiza ambaye aliponiona tu, alinikimbilia na kunikumbatia.
“Eti wameamua kunipakazia kwamba mimi ni mgonjwa wa akili. Jamal, eti mimi naongea kama mtu aliyechanganyikiwa?” aliniuliza Shenaiza huku akilia kwa uchungu, nikamuomba yule nesi atuache kidogo ili tuzungumze wawili tu, akanitazama kwa macho yake mazuri ya kurembua kisha akatingisha kichwa kuonesha kukubaliana na nilichomwambia.
“Nakupa dakika tano tu, nakusubiri pale pembeni,” alisema, nikamshukuru na kumshika mkono Shenaiza, tukakaa kwenye benchi lililokuwa pembeni.
“Akina nani wanaokupakazia kwamba wewe ni mgonjwa wa akili?”
“Baba na watu wake, wanataka kuniziba mdomo maana nimetishia kwamba nitaueleza ulimwengu wote ukweli wa wanachokifanya, naomba unisaidie,” alisema Shenaiza huku akilia, akanikumbatia kwa nguvu huku machozi mengi yakinichirizikia mwilini.
Kitu ambacho lazima nikikiri hapa, japokuwa nilikuwa nimeamua kumchagua Raya kuwa mke wangu mtarajiwa, nilipokuwa nikimtazama Shenaiza au kukaa naye karibu, moyo wangu ulikuwa ukisuuzika mno. Nadhani hata yeye alikuwa analijua hilo ndiyo maana kila tunapokaa pamoja, ilikuwa ni lazima anishike mkono, aniegamie au anikumbatie.
“Sasa nakusaidiaje Shenaiza mbona unazidi kuniweka kwenye wakati mgumu?”
“Unataka kuwajua watu waliokuwa nyuma ya tukio lako la kunusurika kuuawa?”
“Ndiyo, hata sasa hivi nataka kuwajua. Bado nina maswali mengi kichwani ambayo hayana majibu.”
“Najua, majibu ya maswali yako yote ninayo na kwa hali ilipofikia, nipo tayari kukueleza kila kitu kabla hawa mashetani hawajaniharibu kumbukumbu zangu maana najua haya madawa ya wagonjwa wa akili wanayolazimisha nichomwe, huwa yanaenda kuvuruga kabisa ubongo,” alisema Shenaiza kisha akanibusu kwenye paji la uso.
“Nenda Kisutu, Mtaa wa Mama Zayumba, nyumba namba 203, muulize mtu anaitwa Firyaal, ni mdogo wangu wa kuzaliwa na nilishampa maelekezo, kuna bahasha atakupa na hiyo ndiyo yenye majibu ya maswali unayoyahitaji,” alisema Shenaiza huku akinitazama kwa macho ya upole.
“Narudia tena kukuomba msamaha kwa yote yaliyotokea Jamal, naomba unisamehe. Nahitaji ukaribu wako na msaada wako katika kipindi hiki kigumu ninachopitia,” alisema Shenaiza huku macho yake yakiwa yamebeba ujumbe mzito zaidi, tukatazamana kama sekunde tano mfululizo, nikamuona akiachia tabasamu hafifu lililofanya uzuri wake wa asili uonekane vizuri.
“Ukikamilisha kazi nitakupa zawadi ya ushindi,” alisema Shenaiza huku akinifinyia kijicho kimoja, nilishaelewa alimaanisha nini. Nikasimama na kumshukuru, nikambusu kwenye paji la uso wake na kugeuka nyuma ili nirudi kule wodini kwangu.
Sijui Raya alikuwa amefika muda gani eneo hilo kwani nilipogeuka tu, macho yangu na yake yaligongana, japokuwa alikuwa umbali wa mita kadhaa, niliweza kuona hali aliyokuwa nayo. Ilionesha hata kitendo cha mimi kumbusu Shenaiza alikiona kwa macho yake, nikamuona akianza kububujikwa na machozi.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 30
ILIPOISHIA:
“Ukikamilisha kazi nitakupa zawadi ya ushindi,” alisema Shenaiza huku akinifinyia kijicho kimoja, nilishaelewa alimaanisha nini. Nikasimama na kumshukuru, nikambusu kwenye paji la uso wake na kugeuka nyuma ili nirudi kule wodini kwangu.
SASA ENDELEA...

Sijui Raya alikuwa amefika muda gani eneo hilo kwani nilipogeuka tu, macho yangu na yake yaligongana, japokuwa alikuwa umbali wa mita kadhaa, niliweza kuona hali aliyokuwa nayo. Ilionesha hata kitendo cha mimi kumbusu Shenaiza alikiona kwa macho yake, nikamuona akianza kububujikwa na machozi.
Nilijikuta mwili wangu ukipigwa na ganzi, nikabaki nimesimama nikihisi hata miguu ilikuwa mizito kuinyanyua. Raya alipoona nimemuona, aligeuka na kuanza kutembea harakaharaka huku akiendelea kulia. Niljihisi kuwa na hatia kubwa sana ndani ya moyo wangu.
Japokuwa mimi na Shenaiza hatukuwa tumebusiana kwa nia mbaya, nilijaribu kujiweka kwenye nafasi ya Raya na kuhisi maumivu ambayo alikuwa anayahisi kwa wakati huo. Kwa wale ambao wamewahi kupitia maumivu ya mapenzi watakuwa wanaelewa vizuri ninachomaanisha!
Ukimpenda mtu halafu ukasikia au ukahisi mtu mwingine pia anampenda, ukiwaona pamoja lazima moyo uume sana, na hapo ni ukiwaona kawaida tu, iwe wameongozana barabarani au wamekaa sehemu! Raya alishajua kwamba kuna kitu kipo kati yangu na Shenaiza na kama hakipo basi kinakuja lakini kibaya zaidi, alikuwa amenifuma laivu nikimbusu msichana huyo!
Uso wangu ulinishuka kwa haya, sikujua nitatumia maneno gani kumlainisha Raya, nikawa nazidi kuongeza mwendo kumfuata lakini ghafla nikahisi kitu kikinipasua pale kwenye jeraha langu kifuani ambalo japokuwa nilikuwa na nafuu kubwa, bado halikuwa limepona kabisa.
Licha ya maumivu niliyoyasikia, sikutaka kurudi nyuma, nilijikaza kisabuni na kuendelea kujikokota kumfuata Raya ambaye naye alizidi kuongeza mwendo, akiwa hataki hata kugeuka nyuma kunitazama. Nilivuka kwenye mlango wa kuingia kwenye ile wodi niliyokuwa nimelazwa, nikawa naendelea kumfuatilia Raya aliyekuwa akielekea kwenye geti la kutokea kwa kasi.
Hatua chache mbele nilishindwa kuendelea kumfuatilia baada ya kuhisi maumivu yakizidi pale kifuani kwenye jeraha, nikainama kidogo ule upande wenye jeraha, katika hali ambayo sikuitegemea, nilishtuka mno kugundua kuwa kumbe damu zilikuwa zikinitoka pale kwenye jeraha kiasi cha kulowanisha shati nililokuwa nimevaa.
Nilipogeuka nyuma, niliona michirizi sakafuni kuonesha kuwa kumbe damu ilianza kunitoka pale nilipohisi kitu kikinipasua kifuani, hofu kubwa ikatanda moyoni mwangu. Nikawa nahaha kutaka kujifuta damu na kuzifuta sakafuni kabla mtu yeyote hajaona maana ningeonekana mzembe nisiyejijali afya yangu na huenda madaktari wangenifokea sana lakini sikuwa na nguvu ya kufanya hivyo.
Niligeuka huku na kule kutazama kama kuna mtu alikuwa akiniangalia, pande zote hakukuwa na mtu yeyote zaidi ya Raya aliyekuwa akiishia kwa mbali, lakini nilipotazama kwenye mlango wa ile wodi niliyokuwa nimelazwa, macho yangu yaligongana na ya yule nesi ambaye kumbe muda wote alikuwa akitazama kila kilichokuwa kikiendelea, akiwa ametulia tuli.
Nilishindwa cha kujibu zaidi ya kuendelea kuhaha huku na kule, yule nesi aliendelea kunitazama huku akitingisha kichwa kwa masikitiko. Maumivu yalinizidi, ikabidi niegemee kweye ukuta wa korido huku nikipumua kwa shida.
Harakaharaka yule nesi alikuja mpaka pale nilipokuwa nimeegemea ukuta lakini tofauti na nyakati zote, safari hii hakuwa akicheka wala kutabasamu, kwa mara ya kwanza nilimuona akiwa ‘serious’.
“Help me please!” (Nisaidie tafadhali) nilisema huku nikiendelea kupumua kwa shida, hakunijibu kitu zaidi ya kunipa ishara kwamba nimshike begani, nikafanya hivyo, akapitisha mkono wake mmoja kiunoni kwangu, wa kwangu nikaupitisha kwenye bega lake, akanisaidia kutembea kuelekea wodini huku damu zikiendelea kunitoka.
Yule nesi alinipeleka mpaka kitandani kwangu, akanisaidia kupanda na harakaharaka akanivua lile shati nililokuwa nimevaa, akatoka mbiombio na muda mfupi baadaye alirejea akiwa na kisinia kilichokuwa na vifaa vingi vya tiba.
Kimyakimya akaanza kunisafisha pale kweye jeraha, akanifungua bandeji iliyokuwa imeachia, akanipaka dawa ya kuzuia damu kutoka, akanifunga plasta na bandeji nyingine kisha akanipa dawa za kutuliza maumivu. Akachukua lile shati lililokuwa limeloa kwa damu na kutoka nalo.
Muda mfupi baadaye alirudi akiwa na fulana nyeupe, akanipa nivae huku pia akiwa na vifaa vya kupigia deki, wakati navaa ile fulana kwa umakini ili nisijiumize tena, yeye alikuwa akifuta damu harakaharaka pale chini ya kitanda changu, akaendelea kufuta mpaka kule koridoni nilikokuwa nimechafua.
Yaani hata kama ulikuwa unaumwa vipi, ukikutana na nesi wa namna hii, lazima upone, nilijihisi kuwa na bahati ya kipekee kuhudumiwa naye. Ile fulana aliyonipa nivae ambayo hata sikujua ameipata wapi, ilikuwa imepuliziwa manukato mazuri yaliyofanana na yale aliyokuwa amejipulizia mwilini mwake, nikajisikia raha fulani ndani ya moyo wangu, nikabaki sina la kusema zaidi ya kumshukuru ingawa mwenyewe wala hakunijibu chochote.
Aliendelea kusafisha mpaka nje, aliporudi wodini, niligundua kwamba kumbe wakati akinisaidia kuniingiza wodini, nilimchafua gauni lake jeupe kwa damu, nikazidi kujihisi kua na hatia kubwa. Kumbe na yeye alishagundua kwamba nimemchafua, bila kuzungumza chochote alienda mpaka kwenye chumba cha manesi na kubadilisha gauni, akarudi akiwa amevaa gauni jingine safi.
Kama ilivyokuwa mwanzo, hakutabasamu wala kucheka, hata yale masihara yake hayakuwepo tena, nikahisi nimemkwaza sana kwa nilichokifanya. Alinisogelea pale kitandani, akanipima joto la mwili wangu kisha nikamsikia akishusha pumzi ndefu.
Bila kuzungumza chochote, alienda kukaa kwenye meza iliyokuwa inatazamana na mlango, nikamuona akifunua mafaili mengi, akawa anajaza vitu ambavyo sikujua ni nini, nilihisi ni katika kutimiza majukumu yake ya kazi. Aliendelea kuwa kimya huku mara kwa mara akinitazama kwa kunikazia macho, nikimtazama anakwepesha macho yake na kujifanya hakuwa ananitazama, na mimi nikawa najifanya kama simuoni.
Japokuwa alikuwa ameamua ‘kunichunia’, moyoni nilishukuru kwa msaada alionipa kwani muda mfupi baadaye, yale maumivu yalitoweka kabisa na zile damu nazo zikaacha kutoka, moyoni nikajiapiza kwamba sitainuka tena kitandani mpaka kidonda kikauke kabisa.
Nikiwa pale kitandani, nilizama kwenye dimbwi la mawazo kuhusu mfululizo wa matukio yale yaliyonitokea maishani mwangu mpaka wakati huo, nilikuwa na shauku kubwa ya kupona haraka ili niende kule nilikoelekezwa na Shenaiza kwamba nitakutana na mdogo wake atakayenipa bahasha yenye maelezo ya nilichokuwa nakitafuta.
Hata hivyo, niliamua kujipa muda kidogo ili nipone kidogo na mwili wangu upate nguvu, mawazo mengi yakawa yanaendelea kukizunguka kichwa changu. Niliendelea kujiuliza maswali mengi kuhusu ule ulimwengu mwingine niliouona na maajabu yake, pia jinsi nilivyokuwa naweza kutoka kwenye mwili wangu halisi na kukaa pembeni kisha nikaanza kujitazama mwenyewe.
Ndani ya kipindi kifupi tu nilikuwa nimetokewa na matukio mengi ya kutisha na kustaajabisha ambayo hakuna ambaye angeweza kuniamini endapo ningemsimulia na ndiyo maana mwenyewe niliamua kubaki nayo moyoni, mtu pekee ambaye nilitaka nipate muda wa kutosha kuzungumza naye, alikuwa ni Shenaiza ambaye naye alionesha kutokewa na hali kama na iliyokuwa nayo mimi.
“Umefahamiana vipi na yule dada aliyelazwa kwenye wodi ya vichaa?” aliniuliza swali yule nesi lililonizindua kutoka kwenye lindi la mawazo, nilipogeuka na kumtazama, alionekana kuwa bize na simu yake ya kisasa, nikashusha pumzi ndefu na kuendelea kumtazama.
“Si naongea na wewe Jamal?” alisema, nikashtuka zaidi alipolitaja jina langu kwa ufasaha mno, kama vile linavyotakiwa kuitwa, tofauti na watu wengi waliokuwa wakilikosea.
“Ni rafiki yangu tu.”
“Baba yake unamjua?” aliniuliza swali lingine ambalo liliufanya moyo wangu ulipuke paah! Tayari alikuwa amesimama na kunisogelea pale kitandani, ule ‘u-serious’ wake ukawa umepungua kiasi. Alionesha kama kuna jambo muhimu anataka kuniambia kuhusu Shenaiza na baba yake ingawa sikujua ni jambo gani.
“Ha..pa...na! Hapana!” nilijibu kwa kubabaika huku nikiwa makini kutaka kusikia ataniambia nini.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
 
571d1f1b5a157659343b5cbfff2b7a77.jpg
Mkuu
 
Muziki: Bila Style

Mida imeenda hii, yeah, sikutaka niwahishe kuweka muziki ili nikupe nafasi ya kuangalia Futuhi, ujue blaza K ana mambo yake ya kufurahisha na ni bahati mbaya sana siku ya Wenger, eeh siku yake ya kuzaliwa ilikuwa juzi, ilipaswa iwe leo ili Arsenal acheze na tuangalie futuhi. Anyway, usifikiri ninataka kuandika jambo la muhimu sana maana kwa namna ambavyo kila kitu kimeshaandikwa na kuvumbuliwa, mimi ni nani hadi niandike kitu kipya au nivumbue kitu kipya. Kilichobaki ni hapa kazi tu.

Leo nisikuchoshe sana maana it's almost furahiday and with you great and awesome people, Kapuku remain not only to be the best but the perfect forum to visit and ukivutiwa zaidi unastay. Hakuna atakayejali maana humu kila mmoja anapambana na hali yake, kwa mfano, anko wangu yule mnayemjua, yeye tukio lolote hata kama halijatekelezwa, likitangazwa tu basi huyooo. Imetangazwa bomoa bomoa inakuja mjini, akaamua kwenda kuweka makazi Moshi mjini, mji wa wasafi, usafi wa mji sio wa mwili. Kuna tofauti. Leo kasikia uteuzi tayari kavaa suti kaenda kwa mdada mwajiriwa mpya kajitambulisha kuwa yeye ndo katibu mkuu muhtasi, mzee wa mafaili, pedeshee, mwajiriwa mpya kaingia kingi, unajua anko alichofanya, usikiseme maana nina aunty yangu ana moyo na mimi sipendi kumuumiza moyo. Na mvua zinavyonyesha, basi nikufungulia mikatiko ya wanakatitu.

Muziki sasa, kwa nini ujidai kumechisha eti kwenda na style, kesho tokelezea bila style maana ni furahiday na ninakupenda sana Kapuku mheshimika na kama nilivyosema kwa kimombo. Kuhusu umombo, wakati mwingine huwa namwaga ung'eng'e hadi natamani kuwauliza wazazi wangu kama walinitafuta wakati wakiwa tingasi aka walilalana kunitafuta wakiwa wamelewa bia, full kuongea kilugha cha kizungu hadi nikapatikana. Usikasirike kama wewe walilombana wakiwa na njaa, kila siku kulalamika tu. Nilichoandika leo dadeki unaniombea nipigwe radi, haiwezekani maana humu kila mornie BH anamwaga sala na ninazishiriki kikamilifu hadi wakati mwingine najistukia kwa namna navyozifatilia anaweza akatangaza tuanze kutoa sadaka. Nakupenda kapuku mwenzangu na unalijua hili, ujue nini, Easy friday ndo nayokuombea

 
...asante anko, ujue wewe ndo anko wangu ambaye unaniteteaga sana, achna na yule aliyehamisha makazi. Alininunulia simu ya smartphone haina internet wala huwezi kuzoom picha. Nilipomwambia kuhusu kuzuoom eti akaniambia niipeleke kwa mwalimu wa zoom technical college, yule mwalimu mdada anayesukaga kikurya
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom