Makapuku Forum

Makapuku Forum

7/John F Kennedy
b378a0702fc31e71bdd33a20ed57ac31.jpg
4d29617720582633480eeaa7169d9324.jpg

Alizaliwa mwaka 1917 na kuuawa mwaka 1963 akiwa madarakani
Ni maarufu kwa jona la JFK ila kando yake pia kuna RFK{Robert} na EFK(Edward} bila kumsahau RFK Jr wote hawa wanatokea kwenye ukoo unaoaminika kuwa na nuksi zaidi duniani kwani ukoo wao umeandamwa na vifo tatanishi
Inaaminika aliuawa n CIA/FBI kutokana na kutopendezwa nae
Ndiye Rais aliyeanzisha vita ya Vietnam
Anaaminika kuwa Rais bishoo na mpenda wanawake ...yeye na akina RFK na EFK wote wanaaminika kumlalia Marilyn Monroe na inaaminika wanahusika na kifo chake kupitia CIA/FBI
Alikaa madarakani kuanzia 1861 hadi 1963

Yaani siku 1,036
.....

Aisee
 
6/Millard Fillmore
e45e3c9812638a3aab4f6eac628c8c6d.jpg
df6062766e1749e76794251fdaedd99a.jpg
3c9f503d136fc0c5c2e6bc6b9b611221.jpg
Alizaliwa mwaka 1800 na kufariki dunia 1874
Huyu nae alimalizia muhula wa Rais aliyeachia ngazi sijui alifariki (Taylor)
Akajotahidi kukijenga chama kwa njia sahihi na kufanikiwa kuifanya amani na utulivu kuwa nguzo kuu ya kudumisha umoja na baadaye kurudi tena kilingeni
Aliingoza Marekani kuanzia mwaka 1850 hadi 1853

Yaani siku 969

..............................
Zitaendelea baadaye
 
5/Gerald Ford
f7eb4dd9e67abbcc016b992d674cf089.jpg
2c784cbd28e380c486def82790048380.jpg
d9e787d3642c244f015300855707b539.jpg
Alizaliwa mwaka 1913 na kufariki dunia 2006
Alichukua madaraka kutoka kwa Richard Nixon aliyejiuzulu kwa hiyari kufuatia kuvuja kwa kashfa ya Watergate ambaye hadi leo bado ni kaa la moto kwenye historia ya Marekani wakati huku kwetu kuna kashfa za kibwege bwege na kiki kama vile ESCROW .EPA na Richmond ambazo uwajibikaji wa marais wala hatuhusikii ila milunzi inapigw tu kila siku
Huyu alikuta nchi ikiwa hovyo na mambo ya Cold War na kushindwa kuiweka kwenye mstari
Kilichomponza ni mfumuko wa bei na kuporomoka kwa uchumi hivyo wananchi kupiga miayo kama paka na mwisho wa siku mzigo akabebeshwa yeye
Alikaa madarakani kuanzia mwaka 1974 hadi 1977

Yaani aliogelea swimming pool White House kwa siku 895
......
 
4/Warren G Harding
4414bb97510b40dde05191426e0f7f9b.jpg
b2303654473f69dcee161fcdedc565c6.jpg
AliAliwa mwaka 1865 na kufariki dunia mwaka 1923
Huyu alifariki akiwa madarakani kutumikia muhula wake wa kwanza
Kabla ya kifo chake alikuwa mstari wa mbele kurejea amani katika nchi za Austria na Ujerumani kutokana na Vita Kuu ya kwanza ya dunia
Naye alipitisha sheria kibao nzuri pamoja na za kidwanzi kama vile Sheria ya Uhamiaji na Sheria ya Radio na mawasiliano kama za jamaa wa TCRA bila kusahau kukamuana kodi kama Sizonje na mitambo yake ya EFD
Aliiongoza Marekani kuanzia mwaka 1921 Machi 4hadi alipofariki dunia Agosti 2 1923

Yaani alitawala siku 881 tu
.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom