TUKIO HALISI LA WIZI LILILOISHANGAZA DUNIA:
sehemu ya 08:
Baada ya UN na wachina kuingilia kati na kufanya msako lkn bado likawa fumbo kumpata huyu MTU. fumbo hili liliwatesa FBI kw miaka 7, mpaka mwaka 1978 ambapo kidogo mwanga ulipatikana.
ILIKUAJE........
Kwanza kabisa vidhibiti vinafanya fumbo la kumpata bwana Dan cooper Kua gumu.
Mwaka 1978, mwindaji mmoja aliokota kikaratasi chenye maelekezo ya namna ya kushusha mlango wa nyuma Wa ndege aina ya Boeing 737,( North orient flight 305. Hapo sasa na ndege wanayoifanyia uchunguzi wa tukio la bwana Dan cooper ni Boeing 727.. Hapo nisawa MTU avute bangi alafu umpe chipsi Kuku kw mlenda.
Utata mwingine km alikiangusha hicho kikaratasi bwana cooper kinawezaje kukaa miaka 7 bila kuchanika na karatasi sio Naironi?. Mtihani Mpya huo. Basi wakaashumu poa alikitupa yeye eheeee inakuaje sasa alikitupa yeye tunaamua nn?.
Hakuna cha kuamua maana ushahidi huu ni sinema tuu,
Bahati nzuri sasa ikaja kupatikana mwaka 1980
Mtoto wa miaka 8, alieitwa BRIAN IGRAM akiwa kwnye vacation na familia yake kwnye Beach ya mto Columbia alikua akichimba chimba chini km ujuavyo tabia za watoto....
...Basi bwana ndugu msomaji naona macho yamekutoka eeee.......
Mtoto alichimba shimo lefu kiasi, hapo ndipo alipokutana na makaratasi.
IKAWAJE?..........
Baada ya kuyatoa aliwaita wazazi wake na waligundua vilikua ni vibunda vitatu vya hela.
Presha baada ya kuzichunguza wakabaini ndizo zile zilizosambazwa serio namba zake mpaka mashuleni. Ole wake akutwe MTU anazo atajua kwnn kolea kaskazini hawavai Jean's za blue.
Wakawasiliana na vyombo vya ulinzi na usalama na FBI mbiombio wakaja na kuzibaini ndizo zenyewe
SWALI ZILIFIKAJE PALE?.
Msako uliokua ukifanyika tangu pesa zipotee haikua rahisi MTU aende bichi achimbe na kufukia mkwanja bila kuonekana hata usiku wa manane.
Pili ktk begi mbili vije vipatikane vibunda vitatu zingine ziko wapi?.
Basi FBI wakatumia utaalam wao kufumbua juu ya hili, kwnz vibunda vyenyewe vya hela vilikua km ifuatavyo.
..kibunda cha kwnz kilikua pekee kinajitegemea na kilikua na noti 100 zilizofungwa pamoja kw rubber.
Kibunda cha pili kilijitenga cha ajabu kilikua na noti 90.lkn nazo zilifungwa pamoja kw rubber band.
Kibunda cha tatu nacho kilikua na noti 100 zilozofungwa pamoja.
Licha ya Kua noti zilikua zimefungwa kw rubber band lkn zilikua zimekaa hovyo hovyo ktk umbo la mviringo.
Basi FBI wakatoa conclusion Kua zilikaa hivyo kwakua zilisombwa na maji kuletwa hapo. Lkn kwnn vibunda vijikusanye wa pamoja?.
Hayo maji yalijuaje km hizo hela zinaukoo?. Yaani zifungwe vibunda tofauti ila ziletwe pamoja na kufukiwa shimo moja inaingia akilini kweli?.
UTATA MZITO.......
Ufukwe huo wa mto ulifanyiwa marekebisho na kuchimbuliwa chini kabisa kutengeneza ufukwe wa kitalii miaka miwili kabla ya fedha kupatikana.
Kampuni zilizotumia magreda na katapila ziliboresha ufukwe huo na kuuchimbua mpaka chini zaidi, tifua timua wote na kuutengeneza upya.
Swali hizo pesa zimefikaje pale wakati ufukwe ni Mpya?. Km pesa ziliibiwa 1971 na ufukwe umetifuliwa mpaka chini 1978 pesa zipatikane 1980 zimekujaje?. Inamaana zimekuja baada ya ufukwe kutifuliwa. zilitoka wapi?. FBI wakaingia kazini tena mpaka cooper ajisalimishe.
Hapo kazi ikaibuka upyaaaaaaaaaa.
ITAENDELEAAA......