Makapuku Forum

Makapuku Forum

Sana yani halafu mwingine ukimpiga kibuti hapa anakasirika kweli wakati hapa tunaflirt tu
Niliwahi kuumizwa sana na Patience123 na Sumbai utafikiri ni kweli. Nilitokea kumpenda sana utafikiri ipo siku tuta...aliponipiga kibuti na kuchukuliwa na sumbai iliniuma kweli.
Japo kwa sasa tu marafiki ni watu wazuri sana
 
Hahahaha jambilo si ndio huyu jamaa au

Ila mwandiko nao usikudanganye ujue, si umeona ule Uzi kule
Mwandiko unadanganya plus Ids, usiconclude kwa Id wala mwandiko, watu tunaficha mengi sana, naweza kuigiza utaahira flani humu kuwajua matahira, endapo utaingia mkenge kwa hilo, misheni done.
Tumkumbuke mpenzi wa Jimena lkn alivyotuacha wakati tumemwamini sana, tulibaki na maswali. Mtu alikuja na misheni zake, alpoona lengo tayari akang'oa..naweza kuwa siko sahihi kwa hili pia
 
Cabblepots kuna siku alirudi kwa jina la Malcom lumumba, siku hizi simuoni.
Kiukweli sina mfano wa kufananisha zile siku.
Ni kweli kuna siku tulikuwa twatofautiana kwa muda lkn mwisho wa siku tulibaki WAMOJA, kf ilinifunza mengi kuanzia kuchukuliana kitabia na kukubaliana.
Tulionekana tunafanya mambo ya kijinga LAKINI nimegundua jf sasa wanaielewa kf na wengi hupita humu kimyakimya wanajifunza na KULIKE KIMOYOMOYO.
Kf imenipa marafiki wengi hadi wengine tunafanya project za maana baada ya kukutanishwa na kf.
Mimi huwa ninamsemo usemao "unaweza kuokota fedha jalalani"
Tuliitwa kila aina ya majina na kebehi eti kisa jina KAPUKU lkn leo wengi hupita humu na kujifunza, nimeshuhudia wakikiri kwa vinywa vyao.
Ni kweli hata nami natamani tukutane siku moja, I have nothing to hide hata niogope kukutana na mtu wa jf.
Cc mkongo
Shululu
Bitoz
Jimena
Sweetiepie
Lizzie
Beilly5
Manuu
Briz
Pat123
Mussoli5
Youngblood
Nawamis hawa viumbe wa kipindi kile
Si maanishi waliopo hawafai lahasha
Wakuu hapa twakumbuka mbaali sana mtuwie radhi. Tunaheshimu uwepo wenu sana
Transcend
Lee
Shunie
Sakayo
Husna
Fakalava
Bleesedhope
Mondray
Na wengine wengi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom