Makapuku Forum

Makapuku Forum

8e7d0f5c77995c7acb754a69c7c87123.jpg
 
Katika dondoo za bbc. .


Polisi jijini London nchini Ungereza wamesema ni vigumu kutambua miili ya watu waliokufa katika tukio la ajali ya moto ulioteketeza jengo la ghorofa Magharibi mwa mji huo siku ya Jumanne kutokana na kuharibika vibaya.

Ziwa Tanganyika limetajwa kuwa ziwa la mwaka lililo hatarini.Wanasayansi wanasema, shughuli za binadamu kama vile ukataji miti pembezoni mwa ziwa, umwagaji wa sumu kutoka viwandani na hata kutoka kwa makazi ya watu kunaendelea kuathiri samaki na viumbe vingine vilivyomo ziwani humo.

Maendeleo ya sayansi na teknologia kama vile kuwepo kwa vipindi mbalimbali vya Televisheni, yanatajwa kuchangia kuvunjika kwa maadili ya watoto katika nchi za Afrika mashariki.

Kenya yakabiliwa na upungufu mkubwa wa mahindi.Wakulima wameishiwa na akiba, hifadhi ya serikali imeisha, na mahindi yanayoagizwa kutoka nchi za nje hayakidhi mahitaji.

Utasikia mwimbaji mashuhuri wa Kenya, Linet Munyali kwa jina la kisanii Size Eight, akizungumzia wimbo alioutunga juu ya maisha magumu aliyoyapitia awali.
 
MITHALI 22

4.Thawabu ya unyenyekevu ambao ni kumcha BWANA .Ni utajiri ,na heshima,nayo ni uzima.

MUNGU AWABARIKI SIKU YA LEO AWAPONYE,AWAFANIKISHE AWAEPUSHE NA HATARI ZOTE ZA MWILI NA ROHO MUWE NA SIKU NJEMA YENYE BARAKA TELE
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom