Muziki na Kutokelezea
Piga pamba unavyoweza, tokelezea unavyoweza, jipambe upambike na usishau kutumia muda wako kwenye kioo ili kutambua kuwa kila mmoja wetu ni kichaa kwa aina yake.
Sijui kama ninarudia hiki ninachoandika, lakini hata kama ninarudia hakuna ubaya maana maana inaweza kubadilika kutokana na sababu kadha wa kadha ikiwemo siku. Ukiwa katika siku zako basi unaweza kuona rangi zote na kama hauko kwenye siku zako basi usishangae ukijikwaa na kulaumu ulipoangukia.
Salama lakini humu ndani? Nilitingwa kidogo, si unajua tena mambo ya kuitafuta siku uimalize mapema, sasa leo nilikuwa kwenye siku yangu, niliiona yaani tight ile mbaya lakini nimeimaliza na sasa nausubiri mwezi, nipokee mshahara. Kadri unavyoimaliza siku yako ndivyo mshahara unakaribia, haijalishi unalipa au unalipwa.
Turudi kwenye muziki, jana nilikwambia kuwa wanamuziki waanzilishi wa Les Wanyika kina Ngereza na Kinyonga walikimbilia Kenya kutokana na ugumu wa uchumi katika tasnia ya muziki, well, hizi mambo ukiona kwako kugumu mwingine anatamani aje. Wakongo kibao walimiminika Bongo miaka ya 70, 80 na 90 na kuendelea hadi kesho.
Mmoja wao alikuwa ni mpiga gitaa mzuri tu ambaye ukisikiza anavyopiga gitaa na kuimba utampenda sana, sauti na gitaa lake, solo hilo. Anaitwa Nguza Viking.
Unajua yanayoendelea kwake na watoto wake, na hii si mada ya leo. Leo tunawmangalia tu katika muziki na gitaa. Aliwahi kupiga gitaa na nguli wetu wa bongo komandoo Hamza Kalala.
Nguza mbali ya kupiga muziki alikuwa ni mtunzi mzuri na moja ya kibao kilichompatia umaarufu ni Seya na hasa pale alipokiboresha na mwanae Papi kocha
tizama hii clip ya YouTube ufurahie, hadi wakti mwingine tena