Makapuku Forum

Makapuku Forum

Wanahakikisha pia kuwa mmegawika. Eti Anglophone Africa, Francophone Africa na Lusophone Africa. Ulishaona wapi bara linagawanywa kulingana na lugha za waliolitawala? Na wakazi wake wakakubali? Na mgawanyo huu hauishii hapa tu bali kiichumi, kitamaduni n.k. Divide and rule mpaka kesho na keshokutwa!


Kuna kitabu kimoja cha prof mkenya jina limenitoka, nitaandika tena nikikumbuka. Kaongea sana haya mambo kama ulivyoyaeleza, inakera sana.

Tukirudi sisi kwa sisi ndo tatizo kubwa zaidi na wala hatuhitaji kuwasingizia wazungu, ni mindset zetu tu. Haiwezekani hadi leo bado tuendelee kusema matatizo yetu yanaletwa na wazungu. Hivi ni kweli tunapokuwa na tatizo la kukosa umeme tuseme ni wazungu? Hawa si wanauza majenereta? Tunatoa kodi ilhali tunakosa shule zeney kujitosheleza, barabara mbovu, maji shida, na hii kweli tuwasingizie wazungu? Nipe mapumziko tafadhari.

Yaani viongozi kula rushwa na kwenda kuficha mali wanaoztuoibia huko Yuropa na Marikani, tuwasingizie wazungu? No way, tusiangushe lawama zetu kwa mwingine, hii si njia nzuri ya kupambana na stress zetu.

tuseme kweli, sheria za migoodi zisizotunufaisha tuwasingizie wazungu? tembo wetu kuuliwa tusingizie wachina? halafu ukiwmi tunasingizia sokwe😱, sokwe mtu labda.

Shimba na Makapuku asante kwa kuchokoza hii kipenegele kwa leo
 
Huwa Najitahidi saaana kukuelewa lakini hilo limeshindikana
Wakati mwingine ili kuielewa mijadala ya hapa Makapuku inabidi ifuatilie ilikoanzia. Mara nyingi huwa nafanya hivyo kama nina interest na kitu au nafumba macho tu na kudandia treni kwa mbele liwalo na liwe. Na hapa Makapuku wengine hatuishii tu katika matani ya ushemela, ukoromije na upedeshee bali tunajaribu kuweka vihoja chokonozi chokonozi na tumada twa maana maana hivi ili kuendelea kuipa hadhi forum yetu hii tuipendayo.

Uko off mode umesema. Pengine ndiyo sababu. Hope your dopamine level balances itself out...and that you feel better. Usiku mwema!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom