Makapuku Forum

Makapuku Forum

1955 - Watazamaji 83 wa mbio za za magari wanafariki Dunia huku 100 wakijeruhiwa baada ya magari mawili kugongana katika mashindano ya 24 hours of Le Mans.

Inakuwa ni ajali iliyoua watazamaji wengi katika historia ya mashindano ya magari.
f2b6d68ae84c07761a518863a827b4cf.jpg
0f3164a931ba9a2266295ef7025ec95e.jpg
 
Uzuri wa wenzetu ajali ikitokea wanajifunza na kufanya marekebisho. Bila shaka huu ulikuwa ndiyo mwanzo wa kujenga zile kuta imara na bonyevu kutenga magari na watazamaji. Siyo kama sisi ajali ile ile inatokea kila leo na hakuna kinachofanyika. Tunaishia kusema eti watu wanatoa makafara yao ya Freemason!
 
1962 - Wafungwa Frank Morris, na ndugu wawili Clarence na John Anglin wanakuwa wafungwa pekee kufanikiwa kutoroka katika Gereza la kisiwa la Alcatraz huko Marekani.

Gereza la Alcatraz lipo kisiwani na limezungukwa na maji yenye baridi kali na kina kirefu sana lakini Wafungwa hawa walifanikiwa kutoroka na hawakuwahi kuonekana tena.

Licha ya msako mkali wa kwenye maji, ardhini na anga wafungwa hawa hawakuwahi kupatikana tena, licha ya tetesi kudai walifanikiwa kutoroka na kwenda Brazil ila kuna wengine wanaamini wafungwa hao walikufa kutokana na baridi kali ya maji japo hakuna maiti iliyowahi kupatikana.
0b3945243e2a171235596264ed71951c.jpg
a951fc6fb3f13457e10e036425dca80c.jpg

Heri kufika msituni kuliko utumwani gerezani
.....
 
Uzuri wa wenzetu ajali ikitokea wanajifunza na kufanya marekebisho. Bila shaka huu ulikuwa ndiyo mwanzo wa kujenga zile kuta imara na bonyevu kutenga magari na watazamaji. Siyo kama sisi ajali ile ile inatokea kila leo na hakuna kinachofanyika. Tunaishia kusema eti watu wanatoa makafara yao ya Freemason!
Na tulivyo na imani za kishirikina km za "bwana yule"
Eti ajali ya Lucky Vincent utasikia wachawi na mvua hawapatani hivyo ni msimu wa makafara ya barabarani
Hata ajali ya basi kuteketea Butiama ni kafara la damu

.......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom