denoo49
JF-Expert Member
- Mar 29, 2011
- 6,113
- 6,953
Honestly sijawahi angushwa na sijui kama itatokea niangushwe na wewe. Maombi mjarabu kabisa mpaka yamenitoa usingizini ghafla. Ndio maana huwa najisema "husinikubali haraka"1 YOHANA 5
14. Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake,ya kuwa tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake,atusikia.
TUOMBE
Asante Baba kwa ulinzi wako mchana kutwa,tunaomba toba kwa mabaya yote tuliyotenda kwa mawazo ,maneno,matendo na kwa kutotimiza wajibu wetu mbalimbali tusamehe twakusihi.
Tunajikabidhi mikononi mwako tulinde tuondoe katika hatari mbalimbali tukumbatie usiku kucha hadi tutakapoamka kesho mfalme wa Amani.
Ponya wagonjwa,fariji wafiwa na wajane ,yatima .
Tunakuomba tuimarishe tukuamini na kukupenda na kuleta mahitaji yetu mbele zako tukiamini kupokea.
Tunakemea nguvu zote za giza,pepo wachafu na tunaenda kinyume na hila zote za shetani,damu ya Yesu itawale.
Asante Baba kwa kutupa mahitaji yetu sawa na mapenzi yako,Roho Mtakatifu mfariji wetu kaa nasi tufundishe kuomba na kutii
Tunaomba na kushukuru Amen![]()
USIKU MWEMA MBARIKIWE![]()
![]()
Eeh Baba Mungu sikiliza na bariki mahitaji ya nafsi zetu si kwa mapenzi yetu sisi, bali kadiri ya mapenzi yako Baba. Pokea na bariki Sala na maombi ya jamii hii, ili vipepee kama moshi wa ubani mbele ya uso wako. Ameen.
Barikiwa sana Mama Mchungaji tumaini langu.
"ALIYEPUNGUKIWA NA AKILI UWAONEA WATU"
1 YOHANA 5