Muziki na Mapovu Makanikia bila kuwa Makini
Utatoa hutoi, ndivyo kibwagizo cha singeli moja inasikika kwa mbali, najipitia zangu tu kurudi home maana tayari nishaingiza siku kwa deni. Yeah, kukopa ndo ubinadamu huo, tunakopa na kukopesha, tunakopeshana kuanzia mali hadi mwili. Hongera kwa mliokopa leo. Tunakopesheka.
Jumatano inaenda kuisha, na bila kujali muda huu tunarudi kuburudika na muziki huku kama kawaida maneno sikiza mwenyewe , kipengele kinaangalia utamu wa gitaa.
Nilitamani kuweka kibao cha kukataliwa kubaya kukataliwa matesooooo matesoooo lakini nikagundua kuwa nitakuwa ninajiumiza bure bila malipo. Ninasonga na usiku huu tumewaona wote wenye shobo walioamua kubugia foma gold (bila makanikia) na spaleta moto ili kushambulia jukwaa hili, tuwakaribishe. Tuko pamoja
Bendi ya Msondo (kwa ombi maalum la
Shunie na anko
lee empire ) inaweza kuwa bendi maarufu kabisa kwa hapa Tanzania tangu tumepata Uhuru, imebadili majina mara kadhaa kutokana na umiliki na mambo kadhaa lakini mtindo wake umebaki kuwa alama yake, msondo ngoma.
Inaundwa na wanamuziki maarufu na badhi washatangulia mbele ya haki lakini nani anaweza hata kuwakumbuka wapiga gitaa walionogesha sauti za kina Guruma, Bitchuka, Moshi, Jumbe na wengine, sana sana mtamkumbuka Romario na kidevu chake akipuliza midomo ya bata.
Kwenye clip hii hebu angalia na usikize gitaa la mtaalamu Said Mabera, lakini pia wapigaji wengine maarufu wa Msondo ni pamoja na Uvuruge bila kumsahau Pangamawe Ridhiwani
Burudika mdau na nianwapongeza wote mliomeza foma gold bila makanikia kuisema makapuku forum bila kutafuata ukweli wake. Hongereni