Makapuku Forum

Makapuku Forum

Nguo za mitumba zina raha yake. Na kama wewe na waliokuzunguka hamjui kilichoandikwa basi ni poa tu. Tatizo ni pale unapokutana na wanaojua maana yake, na kwa sababu ya "werevu" wao wala hawakwambii zinasemaje bali wanakucheka tu na kukupiga picha. Siyo fair kabisa!
5d7557949141d8319366a5e7ab2dde3e.jpg
Bagheshi wewe noma kweli
 
SHIMBA huwa unanifurahisha pia najifunza mengi kila unapoongelea siasa,uchumi.historia n.k
Kiufupi nchi imeoza au km ni kansa basi imeshafika kichwani na tukimpasua mgonjwa ana % ndogo ya kupona na tukiamua kumuacha anateseka na maumivu na hachelewi kufa

Tuliipuuza misingi aliyotuwekea Kambarage

.......
Asante Madenge. Kuna watu huwa wanadhani kuwa huku Makapuku ni watoto tupu hatuelewi cho chote. Kumbe sivyo. Na sisi huku hata kama ni ishu siriazi tunajadiliana kwa heshima na staha bila kutukanana kama ilivyo huko kwao.

Ni kweli ulivyosema. We have to go back to the drawing board. Tatizo ni kwamba tuliacha misingi ya Kambarage na hatukuweka mingine. Matokeo yake sasa hata falsafa yetu kama jamii haieleweki japo bado tunajifanya tu wajamaa wenye lengo la kujitegemea. Na mimi naamini kuwa hata aje malaika kutuongoza bado tutakuwa tunaangukia pale pale kwenye kisiki na shimo lile lile. Inabidi kabisa kabisa tuamue kwa nia moja kutafuta dhana mpya kuhusu majukumu ya viongozi wetu (pamoja na uadilifu wao), elimu yetu (lengo lake ni nini katika wakati huu?) na hata utajiri (ifike mahali kiongozi aone aibu kutajirika kwa ufisadi, na jamii imkoromee - siyo sasa ambapo ukiiba sana ndiyo unasifiwa na kuitwa mjanja, na ukiwa mwadilifu ukastaafu bila kujilimbikizia mali unachekwa). Na mahali pazuri pa kuanzia ni kuwa na katiba mpya nzuri yenye uwiano na inayotokana na matakwa ya wananchi. Ndiyo maana namdharau sana Kikwete kwa sababu alikuwa ameji-position kuwa mmojawapo wa viongozi bora kabisa tuliowahi kuwa nao kama angetupatia katiba mpya ile ya Warioba. Lakini akaweka matakwa ya chama chake mbele baada ya kuona kuwa pengine kisingeshinda kama uchaguzi uliopita ungefanyika chini ya tume huru. Na kama hiyo haitoshi akatuongezea na sheria ya makosa ya mtandao. Leo hii rais ni kama mungu kwa sababu ana madaraka makubwa mno na watu hawana mahali hata pa kusemea.

Tupiganie kwanza katiba mpya mengine haya ni makelele tu na hakuna kitakachobadilika. Hata the so called wapinzani sijui kama wanalijua hili. Makapuku!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom