Majibu ya Tuhuma Dhidi Yangu!

Majibu ya Tuhuma Dhidi Yangu!

Kigwangallah, mi siyo shabiki wako lakini pia sikumaindi na kila kitu kutokana na mambo yako. Lakini mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Nakupa big up sana kwa kujibu. Wanasiasa wengine wangemyuti upepo upite. Nawashangaa wanaoyapinga maelezo yako. Gazeti limekukashifu. Wewe umejisafisha. Sasa ambaye hakubaliani nawe ana jukumu la kututhibitishia kuwa wewe mwongo. Pia nikupe pongezi. Bila shaka hicho chuo kitatoa fursa ya ajira kwa Watanzania directly na indirectly. Directly ni kwa wale watakaoajiriwa hapo. Indirectly ni kwa wale watakaopata ujuzi hapo na kuajiriwa kwingine.
Watakuita fisadi poa. Lakini bora wewe unayerudisha kwa wananchi kuliko wanaoficha Uswisi.
Lakini jamani sisi Wabongo tunapenda sana kuona wenzetu wakisota. Wakifanikiwa tu ni maneno.
Hamisi, kila la heri. Ila basi kwa kuwa wewe ni kijana jitahidi uwe na mwenendo mzuri kwa jamii. Nyie ndo tunawategemea mshike nchi baadaye. Yaliyopita achana nayo. Kila mtu ana background yake. Wanaokuponda wajibu kwa kuchapa kazi.
 
kwa kweli nashindwa kuelewa utetezi wa huyu mbunge wa nzega!
1. yeye anamiliki hisa 40 na mkewe hisa 11 jumla ni hisa 51 ni zaidi ya nusu ya hisa kiufupi yeye ndo final say
2. hajaonyesha kwa uthibisho kuwa hivyo vifaa anavyotumia kujenga nyumba zake hachukui toka kwenye kampuni yake
3. anasema atayebainika anauza hivyo vifaa atamchukulia hatua kali, hii inathibitisha yeye ndo mwenye kampuni
4. kama hayo magaezi yameandika uongo juu yake kwanini asiyashitaki?
5. athibitshe jinsi alivyopata tenda ya kujenga hicho chuo kihalali bila upendeleo wowote.
6. n.k


binafsi namuona huyu jamaa hamnazo kabisa nillianza kumuona mpuuzi pale alipokuwa anachangia bajeti ya waziri mkuu. na ninaamini kuwa huyu jamaa si kweli kama anapendwa kihivyo na wana nzega, maana hata kwenye kura za maoni alishika nafasi ya 3.

kiufupi wana nzega wamepoteza sana kwa miaka 5!
 
Dr you are being unrealistic people are not as foolish as you suppose, those days are gone when ccm would cheat indiscriminately, It is time for an open government, This is the reason that you intimidate people when they ask you want to come to your constituency shame on you young politician with not heart of your country
 
Kajamaa kamelala mbele baada ya hoja kukazidi. Hahahahaaaaaaaaaa! Watu wameshaleta attachment kwenye uzi huu kuonyesha yeye Kigwa ana hisa 78 na mkewe hisa 22. Sijui documents hizo zimekurupushwa wapi! (Tazama attachments ulipo uzi huu kwenye jukwaa la siasa). Tabu yake huyu Mbunge anabishana na watu asiowajua, yeye anachukulia kama vile anahutubia mkutano wa hadhara pale Nyasa, Nzega. Akiendelea kubisha utaona zinaletwa tena documents alizosamehewa kodi kwa bidhaa asizozitaja. In short kaanzisha ubishi mbaya na sasa inakula kwake.
 
if you don't need to prove anything then delete your non sense which you have blindly posted to the public, take your case to your family and do not involve the public in any of your mess again.

Thank you and let him know(Dr. Kigwangalla) that he has brought his case to the public jury and the burden of proof is on him to prove to usbeyond reasonable doubt(or to our satisfaction) that he is innocent of all allegations as charged. Otherwise he should have kept quiet and sue Tanzania Daima for defamation. He ain't anywhere to receiving rubber stamp of clean bill of health from JF to except him from "fisadis club". No sir, no!!
 
if you don't need to prove anything then delete your non sense which you have blindly posted to the public, take your case to your family and do not involve the public in any of your mess again.

Thank you and let him know(Dr. Kigwangalla) that he has brought his case to the public jury and the burden of proof is on him to prove to usbeyond reasonable doubt(or to our satisfaction) that he is innocent of all allegations as charged. Otherwise he should have kept quiet and sue Tanzania Daima for defamation. He ain't anywhere to receiving rubber stamp of clean bill of health from JF to except him from "fisadis club". No sir, no!!
 
Mkuu Tukundane
Kama hoja ya misamaha imetokana na sheria zilizopo; na kwa maelezo ya mh. HKigwangalla hajengi hoteli ni chuo cha afya ambacho kinaendana na taaluma yake; sasa kosa lake ni lipi kama sheriaa inamruhusu kufanya? Ningepingana naye kama ametumia misamaha ya kodi kujitarisha kwa kuuza mali iliyosamehewa kodi; wengi huu uchangiaji wenu ni wa kisiasa ambao umeegemea zaidi siasa za maji taka; kama ni kweli mna hoja ya kupinga maelezo ya HKigwangalla njooni na data ambazo zitasuta kauli yake; magazeti ya bongo yamegeuka ni uwanja wa mipasho na majungu wataandika chochote ili wauze magazeti; lile gamba lilojipa milioni 140 au lile gamba lilojipa tenda kwa mlango wa uani wa zaidi ya milioni 350 mbona mmeyanyamazia? Mngeanza na nyumbani kabla ya kupiga kelele kwa jirani
Chama
Gongo la mboto DSM

Mkuu uungwana ni kitu kizuri sana kama wewe ulivyoonyesha uungwana wako kwa kukiri wazi na kujionyesha wazi kuwa wewe na siasa ni vitu ambavyo huwezi ukaviweka pembeni kwa ajili ya kuliponya Taifa letu.Pia umeonyesha uungwana wako kwa kuweka wazi kuwa viongozi wa Ccm na sekali yake wanaiba mali ya watz kwa sababu kuna gamba lilojilipa milioni 140 halafu likanyamaziwa.pia watz wanafanyiwa ufisadi kwa sababu kuna gamba lingine lilojipa tenda ya zaidi ya sh.milioni350 kupitia mlango wa uani nalo likanyamaziwa.kwa maana hiyo nchi yetu inapewa adhabu ya kuhujumiwa na serekali ya Ccm kutokana na makosa ambayo yalitendwa na magamba 2 halafu yakaachwa bila kusemwa.kumbuka kuwa siyo haki kabisa kumuadhibu mtu yeyote kwa kosa lililofanywa na mtu mwingine pia huwezi ukasahihisha kosa kwa kujibu na kosa lingine.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu KALOKAZA, asante kwa huo ushahidi wako, maana yake yeye anasema anamiliki 40% lakini vielelzo vinasema ana 78%. Yaani nimejitahidi kusoma maswali na maoni hadi ukurasa huu wa 9 sasa lakini sijamuona kabisa mleta uzi akiwa amejibu swali lolote. Au labda tusubiri kikao cha bunge kitakapomalizika. Mbunge wa nzega, ya nini lakini kumchokoza kichaa wakati unajua unakaa kwenye nyumba ya vioo?
 
Kuwa kiongozi au Mbunge ni dhamana. Kuwa kiongozi haina maana kuwa una akili na hekima kuliko wale unaowaoongoza. Na kuitwa mzee,mzee kila siku na watu wazima kila siku usiwe mvinyo wa kuwalewesha madaraka na kujisahau kiasi hiki. Sasa unaleta maneno ya kukanusha unachosema ni uongo, ujieleza halafu unajionea huruma hapo mwisho. Kumbe kweli kampuni wewe na mkeo ni wanahisa wakubwa. Ulichopaswa kufanya ni kuandika maelezo mafupi na kuweka ushahidi basi. Haya mambo mengine ya kuoneana wivu na kwamba tuchape kazi ni porojo tu. Kwa umeambiwa sisi humu hatuchapi kazi? Nonsense kabisa!!!
 
Mbona Mbunge uko kimya sasa wakati
umeleta Hoja mezani.



Njoo ujibu maana unataka kujiosha.
 
Bwana mbunge.

Wewe ni mtumishi wa watu, umechaguliwa na watu, unawakilisha watu, umebeba taadhima kubwa sana.

Sasa unapoanza kuhamaki na wananchi wa kawaida unajionyesha kukosa kifua, kukosa maarifa, kukosa kujua kwamba unajibizana na watu usiowajua,unajionyesha kutofikiri kwa kina.

Kama mtu uliyepewa heshima na watu ningetegemea heshima kutoka kwako, hata kwa waliokukosea heshima ili wao wapate kujifunza na kuona aibu.

Na hata kama wameumbwa bila aibu, waja wengine watakaotembelea jukwaa hili waone tu kwamba hapa kwa kweli mbunge wetu kakosewa heshima.

Ukimaka unajionyesha hujakomaa.

Ukiandika "why do you think and believe that I need to prove to you anything?!!" unajionyesha hutambui kwamba wazo la kuja kutoa taarifa kutoka upande wako hapa JF tu ni kutaka ku prove kitu.

Maadam wewe ni mtumishi wa umma, kauli hii haifai. Kwa sababu si ya kiungwana na haiendani na utumishi wa umma.Hususan kwa sababu hujui huyo unayejibizana naye ni nani.


My salutes mkuu!
 
Ukisoma katikati ya mistari utagundua kuwa huyu bwana amekiri yote. Kwa akili yake alidhani akianza na maelezo marefu ndio atafanikiwa kushawishi kumbe ndio anajifunga kamba. Kulisifia NIPASHE ni janja ya kutaka gazeti hilo lisiandike habari hiyo. Mimi nilisoma habari ile. Mh. alipewa nafasi ya kueleza tuhuma akakwepa.
 
Huwa najiuliza hivi huko bungeni huwa mnakimbilia nini? kumbe mna agenda zenu za nyuma ya pazia mnaanzisha makampuni halafu mnatafuta tiketi za kuingia bungeni ili biashara zenu mziendeshe kwa kutuibia sisi wananchi. Wakati huku wenzenu PAYE inatumaliza na nyie hata hii haiwagusi. Kweli aliyeshiba hamjui mwenye njaa.
we unalilia PAYE ishushwe wakati mwenzako anapigana kuanzisha kampuni..... ..kinachosikitisha sana huwezi kumwona huyu mbunge hata siku moja anapigania PAYE ishushwe.....pamoja na kwamba naye alishawahi kuajiriwa na kuathirika na PAYE.....hawa wabunge wengi wako hivyo....wanapopata nafasi wanasahau hata walikopitia.....hii ndio aina ya wabunge tulionao......wamejaa ubinafsi uliokithiri......inasikitisha napoona watu wanawatetea wabunge aina hii......
 
Si kweli kwamba nina hisa 78% na mke wangu Dr. Bayoum Kigwangalla ana hisa 22% - ni uongo.

Ya ukweli:
ni nina hisa 40% na mke wangu Dr. Bayoum Kigwangalla anamiliki hisa 11%. Sijihusishi na kuendesha biashara hii kama mtendaji wa kila siku.

attachment.php


Watanzania tuache kushabikia uongo.

Taarifa hii nimeiandika na kuitoa mimi mwenyewe, Hamisi Andrea Kigwangalla, M.D., Mbunge, Jimbo la Nzega. (simu yangu ya kiganjani ni 0782636963 na email yangu ni hkigwangalla@gmail.com, website: www.hamisikigwangalla.com )

Hamisi Andrea Kigwangalla, M.D., Mbunge, Jimbo la Nzega, hizo hisa usizozitolea maelezo zinamilikiwa na nani?
 
Kigwangallah, mi siyo shabiki wako lakini pia sikumaindi na kila kitu kutokana na mambo yako. Lakini mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Nakupa big up sana kwa kujibu. Wanasiasa wengine wangemyuti upepo upite. Nawashangaa wanaoyapinga maelezo yako. Gazeti limekukashifu. Wewe umejisafisha. Sasa ambaye hakubaliani nawe ana jukumu la kututhibitishia kuwa wewe mwongo. Pia nikupe pongezi. Bila shaka hicho chuo kitatoa fursa ya ajira kwa Watanzania directly na indirectly. Directly ni kwa wale watakaoajiriwa hapo. Indirectly ni kwa wale watakaopata ujuzi hapo na kuajiriwa kwingine.
Watakuita fisadi poa. Lakini bora wewe unayerudisha kwa wananchi kuliko wanaoficha Uswisi.
Lakini jamani sisi Wabongo tunapenda sana kuona wenzetu wakisota. Wakifanikiwa tu ni maneno.
Hamisi, kila la heri. Ila basi kwa kuwa wewe ni kijana jitahidi uwe na mwenendo mzuri kwa jamii. Nyie ndo tunawategemea mshike nchi baadaye. Yaliyopita achana nayo. Kila mtu ana background yake. Wanaokuponda wajibu kwa kuchapa kazi.

Nenda Nzega Mkuu, ndani ya Hospitali ya Wilaya ya Nzega kaone mauza uza yake anayoyaita chuo cha afya Nzega! Mwizi/fisadi ni fisadi hakuna afadhali, kama na wewe ni mmoja wao basi hongera!!
 
Back
Top Bottom