Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 97,150
- 137,132
Hivi bongo hakuna PR firms?
mbunge wa nzega,dk. Hamisi kigwangalla (ccm), amejikanganya katika maelezo aliyoyatoa kukanushatuhuma za kutumia vibaya misamaha ya kodi ya mamilioni ya shilingi kwa ajili yaujenzi wa chuo cha afya eneo la uchama, wilayani ya nzega.
katika taarifa yake aliiweka kwenye mitandaoya kijamii na vilevile mazungumzo yake na gazeti hili kwa simu, dk. Kigwangallaalitoa maelezo ya kukinzana ambayo yanatofautiana na yale yaliyoko kwenyenyaraka za kampuni yake ya emergent africa ltd.
wakati kigwangalla akisema msamaha wa vifaahivyo ni kwa ajili ya ujenzi wa chuo cha afya nzega (kitakachoitwainternational institute for health tabora), nyaraka za tra na kituo chauwekezaji (tic) zinataja kituo hicho kamataasisi ya kisasa ya kliniki ya madawa, afya ya jamii na elimu ya biashara.
sambamba na hilo, mbunge huyo anadai kuwa nahisa asilimia 40 na mkewe dk. Bayoum kigwangalla ana asilimia 11 wakati nyarakaza tic zinaonyesha kuwa anamiliki asilimia 78 na mkewe 22.
nyaraka hizo zinaonyesha kuwa kampuni yaemergent africa ltd, ilisajiliwa tic septemba 27, 2011 na iliruhusiwa kupatamisamaha hiyo kuanzia septemba 2011 hadi agosti 2014.
hata hivyo, akizungumza na gazeti hili, dk.kigwangalla alishindwa kufafanua kuhusu utata wa nyaraka kutofautiana tarehe zakuagiza na kupokea bidhaa.
wakati nyaraka nyingine zikionyesha kuwamanunuzi yalifanyika nchini china oktoba mosi 2012, nyaraka za tra zinaonyeshakuwa bidhaa hizo zilishaingizwa nchini tangu aprili 14 mwaka huo, kupitiakampuni ya innovative freight yenye tin 100-145-596, risiti namba2012/0000002986.
pia utata huo, unaonekana katika taarifa zashirika la viwango tanzania (tbs) ambazo zinaonyesha bidhaa hizo zilikaguliwamachi 28, 2012 kwa fomu na 40381.
kuhusu hilo,dk. Kigwangalla alisema, "suala la tarehe ni suala dogo sana, na haliwezi kuathiri bidhaazilizoingizwa nchini. Wewe unakimbilia kujadili tarehe tu, hilo hata watu wa tra hawakuangalia tarehebali bidhaa ndiyo maana wakaruhusu. Pengine tarehe zimekosewa china.
"na wewe una uelewa mdogo wa mambo ya biasharanakuvumilia tu," alisema.
dk. Kigwangalla alisema, "niliwahi kuibiwabidhaa na nyaraka za dukani, ingawa mke wangu alinizuia kuripoti polisi na sasanitachukua hatua, we nenda katoe taarifa unayojua, mimi nitakuja tena kuongezaufafanuzi. Sina uadui na wewe hata mbowe, nitawashtaki mahakamani kadirimnavyonichafua."
aliongeza kuwa bidhaa zilizoingizwa tanguaprili mwaka jana, hazijauzwa; kwamba ziko katika stoo dar es salaam kwani anasubiri kupata mkopoili aweze kuzisafirisha kwenda wilayani nzega.
tanzania daima ilidokezwa kuwa hata kampuni yainnovative freight forwarders co. Ltd iliyoshughulikia upakuaji wa mzigo huo nakuutoa bandarini haijalipwa hadi leo.
akizungumza na gazeti hili kwa simu jana,meneja wa kampuni hiyo, queen mwasanguti, alisema: "kwa kweli wewe ni mtu wanne kuniulizia suala hilo, ni kweli sijajua kuna nini, ingawa ni kwelisijalipwa ila kila nikimuuliza kigwangalla anasema yeye atakuja anikutanishe navijana wake waliosimamia mizigo hiyo ili aweze kunilipa."
aliongeza, "bidhaa ziliingia ndio, sisitulikabidhiwa nyaraka hizo unazotaja tukashughulikia mizigo hiyo kwa taratibuza kawaida, ingawa ni kweli ‘bill of lading' na ankara za manunuzi ya biasharazilitofautiana."
kwa mujibu wa makubaliano kati ya kampuni yaemergent afica ltd na tic, mamlaka ya mapato tanzania (tra) iliombwa kuisamehekodi kampuni hiyo ya dk. Kigwangala vitu mbalimbali vyenye orodha toka namba 1hadi 390.
[font=&] bidhaa hizo kwauchache ni kompyuta 1042, mashine za kutolea kopi 12, printa 12, mashine zakufungia (binding machines) 12, vikokotozi (calculators) 640, projekta 12,‘video camera' 12, feni 30, vifaa vya simu, maboksi 28, jenereta moja, magariaina ya toyota 13, malori matatu, nissan navarra pik up nne, mitsubishi cantermbili na mabasi madogo manane
tanzania daima
[/font]