Kuwa na hisa kwenye kampuni inayofanya biashara halali siyo dhambi. Kupata msamaha wa kodi siyo dhambi. Dhambi ingekuwa kuviuza baada ya kupata msamaha. Kama
kuna mtu anaamini kuwa kuna vifaa vimeuzwa na kampuni yangu, kati ya hivi vilivyoingizwa nchini kwa msamaha,
anakaribishwa kuleta uthibitisho wa nyaraka za mauzo (
cash sale receipts, tax invoice ya mauzo, pay-in slip ya benki ya malipo, delivery note, ama receipt yoyote ile ya kampuni hii inayoashiria kuwa mauzo yamefanyika)
Msamaha wa vifaa hivi ni kwa ajili ya Ujenzi wa Chuo Cha Afya Nzega (kitakachoitwa International Institute for Health Tabora), ambacho nilikianza kwa fedha zangu mpaka pale kilipofikia na sasa tunasubiria majibu ya benki ya maombi yetu ya mkopo ndipo tuendelee.
Tuache kutazama mambo kwa macho ya
wivu, husda na majungu. Tusimame kwenye misingi ya ukweli daima. Nchi hii itaendelezwa na watu wenye kuchukua maamuzi thabiti na hatua za maksudi za kuleta mabadiliko – kama miradi ya namna hii (ya chuo cha afya Nzega
Si kila mtu aliyeko kwenye uongozi ndani ya CCM basi ni fisadi, watu wazuri na wasafi wapo pia. Tusimuangalie kila mtu kwa sura ya ‘ufisadi' na ‘ubadhirifu' tu! Tuaminiane jamani.
Taarifa hii nimeiandika na kuitoa mimi mwenyewe, Hamisi Andrea Kigwangalla, M.D., Mbunge, Jimbo la Nzega. (simu yangu ya kiganjani ni 0782636963 na email yangu ni hkigwangalla@gmail.com, website: www.hamisikigwangalla.com )
Koligi Kigwangalla, naomba nikupongeze kwa kujitokeza hapa Jf kujibu/kutoa tamko juu ya tuhuma za ufisadi zinazo kukabili si jana tu ila ni mara kwa mara kama ulivyojieleza kwenye hoja yako. Na kama ulivyoeleza vizuri sana kuwa si chombo kimoja tu cha habari kilichowahi/kinachopendelea kuweka front page tuhuma zako.
Ninaandika haya nikiwa kama mdau wa sekta ya afya na nimeshafika Hospitali ya wilaya ya Nzega na kufanya kazi karibu kwa wiki mbili, nilipata wasaa wa kuliona hilo jengo ambalo unasema kitakuwa chuo cha Afya Nzega, nilipata wasaa wa kuzungumza na baadhi ya wfanyakazi wa hospitali ya wilaya ya Nzega na kupata historia ya ujenzi unaosua sua wa hicho chuo!
Ukiwa kama Mdau/Daktari wa sekta ya afya, na pia mbunge wa wilaya ya Nzega, Je unayajua haya
1. DMO wako (Mwombeki) ni kama Mungu mtu, haambilikia au amejenga mtandao na mkurugenzi hivyo kila mtumishi atayehoji mambo ya msingi ikiwepo matumizi ya fedha anahamishwa?
2. Taratibu za uendeshaji wa ofisi ya DMO zinakiukwa? Mathalani DMO akisafiri ofisi anakaimu Katibu wa afya? Kwa nini anaogopa kuwakaimisha madaktari wenzake ambao kisheria na kanuni ndio wanaostahili?
Naomba nije kwenye hoja zako ambazo nimeziquote na nimezifayia formatting, nina maswali yafyatayo
1. Gazeti la Tanzania daima wanaamini kuwa kweli Kampuni yako imeuza vitu ambavyo havijalipiwa kodi, Je huoni kuwa ingekuwa ni busara uende mahakamani kuwashtaki Tanzania daima kwa kukuzushia na kuwadai wakuoneshe hivyo vielezo ambavyo wewe unataka sisi members wa Jf tukuletee kama uthibitisho? Tahadhari, najua vitu vya dili vingi havina risiti
2. Ujenzi wa chuo- unaweza kutuambia hatua ya ujenzi iliyofikiwa na jengo halijaendelezwa kwa muda gani? Unaweza pia kutuambia hilo jengo lilikadiriwa kugharimu shilingi ngapi na msamaha ulipaswa kuwa ni wa shilingi ngapi na utuambie mpaka sasa ni asilimia ngapi ya msamaha imeshatumika? Na kiasi gani kimebakia?
3. Wivu, husda na Majungu- Jiulize katika Wabunge wote wa Mkoa wa Tabora au wa CCM kwa nini uonewe wivu na husda koligi
HKigwangalla? Na bahati mbaya Wengi wenu na chama chenu mnakimbilia kutamka hayo maneno bila kujenga hoja, wewe si wa kwanza
4. Hoja ya si kila Mtu aliye CCM ni fisadi- Umetajwa wewe kama
HKigwangalla, na si CCM, sasa kwenye hoja yako CCM imekujaje? Haya tuache hili, lakini kumbuka kuna kada moja mkongwe wa CCM aliwahi tamka kuwa hakuna msafi ndani ya CCM, Koligi, unaweza kunitajia kwa kadiri ya uelewa wako angalau Kada mmoja tu wa CCM aliyemsafi? Ukishindwa uje hapa Jf uombe tukupe list of shame ya wabunge na makada wa CCM
Naomba kuwasilisha comrade!!