nyboma
JF-Expert Member
- Aug 29, 2021
- 2,199
- 6,890
Hii nimeishuhudia leo Mlimani city katika mgahawa mmoja maarufu wa chakula, yaani kijana na nguvu zake inakuaje anakubali kununuliwa chakula na mwanamke ili hali angeweza kutumia nguvu na akili zake katika kutafuta pesa.
Na katika uchunguzi nimegundua yule mama atakuwa amemzidi kijana wa watu miaka si chini ya 20.
Sisi kama taifa tunaelekea wapi katika malezi, huyu kijana niliye mshuhudia leo alikuwa amejazia kifua, kachora tatoo kila mahali kavaa nguo zimebana miguu kama skin tight za wadada, au ndio ule msemo unaosema kila mtu hula kwa urefu wa kamba yake.
Vijana wa sasa mnatuabisha wazee wa zamani, nikiweka kumbukumbu sawa kwa miaka yetu hali haikuwa hivi, mambo yalikuwa tofouti sana vijana wa sasa wanatumia muda mwingi katika kioo (kujipodoa) na gym (kutengeneza mwili) badala ya kutumia muda huo kutafuta pesa.
Vijana wa sasa mnatuangusha sana sisi wazee, mbadilike.
Na katika uchunguzi nimegundua yule mama atakuwa amemzidi kijana wa watu miaka si chini ya 20.
Sisi kama taifa tunaelekea wapi katika malezi, huyu kijana niliye mshuhudia leo alikuwa amejazia kifua, kachora tatoo kila mahali kavaa nguo zimebana miguu kama skin tight za wadada, au ndio ule msemo unaosema kila mtu hula kwa urefu wa kamba yake.
Vijana wa sasa mnatuabisha wazee wa zamani, nikiweka kumbukumbu sawa kwa miaka yetu hali haikuwa hivi, mambo yalikuwa tofouti sana vijana wa sasa wanatumia muda mwingi katika kioo (kujipodoa) na gym (kutengeneza mwili) badala ya kutumia muda huo kutafuta pesa.
Vijana wa sasa mnatuangusha sana sisi wazee, mbadilike.