ASIWAJU
JF-Expert Member
- Nov 18, 2022
- 1,939
- 1,625
Habari za sasa wanachama wa Jamiiforums natumai wote ni wazima wa afya, nilikuwa na jambo lini kereketalo moyoni mwangu liitwalo “MAHARI”
Nilikuwa na tatizo na huu utamaduni ulio zoeleka hapa dunia mpaka kukomaa wa malipo ya kifedha/mali kwa mwanaume/mwanamke ili kuweza kukidhi vigezo vya kuoa au kuolewa.
Mahari ni kitendo kinacho shusha utu wa watu hapa duniani kwa wake na kwa waume hauna tofauti na biashara ya utumwa iliyo kuwa imemea hapa duniani Karne za 19 kurudi karne nyuma iliyo husisha kununua watu walio thaminishwa kwa viwango mbalimbali vya kifedha na kimali kutokana na maumbile yao na uwezo wao wa kinguvu.
Duniani mpaka sasa kwa asilimia kubwa watoto wa kike wana thaminishwa kama bidhaa sokoni kwa kigezo cha mahari kama utamaduni kitu ambacho kinavunja utu wa mtu kwa kuwa mtu hawezi kuthaminishwa kwa kiwango chochote kile cha fedha au mali.
Sasa wazazi wameshikwa na viburi vya kitamaduni za kitumwa kwa kuwa thaminisha wanao kutokana na tabia nzuri walizo nazo wanao au uzuri wa rangi/ maumbile ya wanao na kutaja viwango mbali mbali vya kifedha au mali mfano [ Mzazi anasema“ hauwezi kuoa mwanangu bila million 5-10 au bila ng'ombe 10-20]
Huu utamaduni wa mahari ulio mbaya unao vunja utu wa watu hapa dunia umekaliwa kimya sana na dunia tofauti na tamaduni nyingine kama ukeketaji, ndoa za utotoni, biashara ya utumwa wakati wa ukoloni n.k hizi ni baadhi ya tamaduni zilizo pigiwa kelele na dunia mpaka kukoma nyingine kupungua kwa kasi sana hapa duniani.
Ushauri binafsi: Kwa nini fedha/mali zinazo tumika kukamilisha biashara hii ya utumwa[ mahari ] visiwanye wazazi wa pande zote mbili wakutane kwa pamoja na kukusanya fedha au mali hizo kwa pande zote mbili na kuwa changia watoto wao fedha za kuanzia maisha yao kitu ambacho kitakuwa msaada kwao na kwa maisha yao.
Maswali:
1. Kwa nini dunia ipo kimya kuhusu kukomaa kwa biashara hii ya utumwa ya kuuza watu kwa kigezo cha tamaduni ?
2. Licha ya kuwa wanawake ndio waathirika wakuu wa biashara hii ya utumwa iitwayo mahari, kwa nini wame likalia kimya swala hili ?
3. Kwa nini wapiganiaji wakuu wa swala la usawa wa kijinsia na haki za binadamu wame likalia kimya swala hili la biashara ya utumwa linalo vunja utu wa binadamu kwa kigezo cha mahari ?
4. Je ni haki na ni sahihi mtu kuendelea kuthaminishwa kwa viwango vya kifedha au mali ?
5. Kwa nini wanawake walio wengi hawataki kuolewa bila kunuliwa ? Na hutambiana wao kwa wao kwa viwango vya kifedha au mali vilivyo tumika kuwa nunua ?
Karibuni wadau kwa michango yenu, Ila zingatieni zaidi mada husika na maswali tajwa.
Nilikuwa na tatizo na huu utamaduni ulio zoeleka hapa dunia mpaka kukomaa wa malipo ya kifedha/mali kwa mwanaume/mwanamke ili kuweza kukidhi vigezo vya kuoa au kuolewa.
Mahari ni kitendo kinacho shusha utu wa watu hapa duniani kwa wake na kwa waume hauna tofauti na biashara ya utumwa iliyo kuwa imemea hapa duniani Karne za 19 kurudi karne nyuma iliyo husisha kununua watu walio thaminishwa kwa viwango mbalimbali vya kifedha na kimali kutokana na maumbile yao na uwezo wao wa kinguvu.
Duniani mpaka sasa kwa asilimia kubwa watoto wa kike wana thaminishwa kama bidhaa sokoni kwa kigezo cha mahari kama utamaduni kitu ambacho kinavunja utu wa mtu kwa kuwa mtu hawezi kuthaminishwa kwa kiwango chochote kile cha fedha au mali.
Sasa wazazi wameshikwa na viburi vya kitamaduni za kitumwa kwa kuwa thaminisha wanao kutokana na tabia nzuri walizo nazo wanao au uzuri wa rangi/ maumbile ya wanao na kutaja viwango mbali mbali vya kifedha au mali mfano [ Mzazi anasema“ hauwezi kuoa mwanangu bila million 5-10 au bila ng'ombe 10-20]
Huu utamaduni wa mahari ulio mbaya unao vunja utu wa watu hapa dunia umekaliwa kimya sana na dunia tofauti na tamaduni nyingine kama ukeketaji, ndoa za utotoni, biashara ya utumwa wakati wa ukoloni n.k hizi ni baadhi ya tamaduni zilizo pigiwa kelele na dunia mpaka kukoma nyingine kupungua kwa kasi sana hapa duniani.
Ushauri binafsi: Kwa nini fedha/mali zinazo tumika kukamilisha biashara hii ya utumwa[ mahari ] visiwanye wazazi wa pande zote mbili wakutane kwa pamoja na kukusanya fedha au mali hizo kwa pande zote mbili na kuwa changia watoto wao fedha za kuanzia maisha yao kitu ambacho kitakuwa msaada kwao na kwa maisha yao.
Maswali:
1. Kwa nini dunia ipo kimya kuhusu kukomaa kwa biashara hii ya utumwa ya kuuza watu kwa kigezo cha tamaduni ?
2. Licha ya kuwa wanawake ndio waathirika wakuu wa biashara hii ya utumwa iitwayo mahari, kwa nini wame likalia kimya swala hili ?
3. Kwa nini wapiganiaji wakuu wa swala la usawa wa kijinsia na haki za binadamu wame likalia kimya swala hili la biashara ya utumwa linalo vunja utu wa binadamu kwa kigezo cha mahari ?
4. Je ni haki na ni sahihi mtu kuendelea kuthaminishwa kwa viwango vya kifedha au mali ?
5. Kwa nini wanawake walio wengi hawataki kuolewa bila kunuliwa ? Na hutambiana wao kwa wao kwa viwango vya kifedha au mali vilivyo tumika kuwa nunua ?
Karibuni wadau kwa michango yenu, Ila zingatieni zaidi mada husika na maswali tajwa.