Mar 26, 2024 10:52 UTC
Guterres atoa wito kwa nchi za Magharibi kulipa fidia Waafrika kutokana na biashara ya utumwa.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito wa kulipwa fidia watu waliosafirishwa kwa njia haramu kama watumwa kutoka Afrika hadi katika nchi za Bahari ya Atlantiki.
Katika taarifa yake kwa mnasaba wa Siku ya Kimataifa ya Kuwakumbuka Wahasiriwa wa Utumwa na Biashara ya Utumwa katika Bahari ya Atlantiki, Guterres amesema utumwa "uliweka misingi ya ubaguzi wa kikatili unaozingatia utawala wa Wazungu ambao bado unaendelea hadi leo."
Kuanzia karne ya 15 hadi 19, Waafrika wasiopungua milioni 12.5 walitekwa nyara, wakasafirishwa kwa lazima kwa meli na wafanyabiashara Wazungu wa Ulaya, na kuuzwa utumwani. Wale walionusurika safari hiyo ya kikatili waliishia kuhangaika kwenye mashamba ya Amerika, hasa Marekani, Brazil na Karibea.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema: "Wengi wa wale waliopanga na kuendesha biashara ya utumwa katika Bahari ya Atlantiki walijikusanyia utajiri mkubwa. Wakati huo huo, watumwa walinyimwa elimu, huduma za afya, fursa na ustawi."
Guterres atoa wito kwa nchi za Magharibi kulipa fidia Waafrika kutokana na biashara ya utumwa.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito wa kulipwa fidia watu waliosafirishwa kwa njia haramu kama watumwa kutoka Afrika hadi katika nchi za Bahari ya Atlantiki.
Katika taarifa yake kwa mnasaba wa Siku ya Kimataifa ya Kuwakumbuka Wahasiriwa wa Utumwa na Biashara ya Utumwa katika Bahari ya Atlantiki, Guterres amesema utumwa "uliweka misingi ya ubaguzi wa kikatili unaozingatia utawala wa Wazungu ambao bado unaendelea hadi leo."
Kuanzia karne ya 15 hadi 19, Waafrika wasiopungua milioni 12.5 walitekwa nyara, wakasafirishwa kwa lazima kwa meli na wafanyabiashara Wazungu wa Ulaya, na kuuzwa utumwani. Wale walionusurika safari hiyo ya kikatili waliishia kuhangaika kwenye mashamba ya Amerika, hasa Marekani, Brazil na Karibea.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema: "Wengi wa wale waliopanga na kuendesha biashara ya utumwa katika Bahari ya Atlantiki walijikusanyia utajiri mkubwa. Wakati huo huo, watumwa walinyimwa elimu, huduma za afya, fursa na ustawi."