Guterres atoa wito kwa nchi za Magharibi kulipa fidia Waafrika kutokana na biashara ya utumwa

Malaria 2

JF-Expert Member
Oct 17, 2023
2,648
3,938
Mar 26, 2024 10:52 UTC

Guterres atoa wito kwa nchi za Magharibi kulipa fidia Waafrika kutokana na biashara ya utumwa.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito wa kulipwa fidia watu waliosafirishwa kwa njia haramu kama watumwa kutoka Afrika hadi katika nchi za Bahari ya Atlantiki.

Katika taarifa yake kwa mnasaba wa Siku ya Kimataifa ya Kuwakumbuka Wahasiriwa wa Utumwa na Biashara ya Utumwa katika Bahari ya Atlantiki, Guterres amesema utumwa "uliweka misingi ya ubaguzi wa kikatili unaozingatia utawala wa Wazungu ambao bado unaendelea hadi leo."

Kuanzia karne ya 15 hadi 19, Waafrika wasiopungua milioni 12.5 walitekwa nyara, wakasafirishwa kwa lazima kwa meli na wafanyabiashara Wazungu wa Ulaya, na kuuzwa utumwani. Wale walionusurika safari hiyo ya kikatili waliishia kuhangaika kwenye mashamba ya Amerika, hasa Marekani, Brazil na Karibea.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema: "Wengi wa wale waliopanga na kuendesha biashara ya utumwa katika Bahari ya Atlantiki walijikusanyia utajiri mkubwa. Wakati huo huo, watumwa walinyimwa elimu, huduma za afya, fursa na ustawi."
 
Huko West Africa Wazungu wanaweza kulipa hapa Africa ya Mashariki kama tujuavyo ni Waarabu ndio walitusomba kwenda Utumwani je hawa Waarabu watalipa hata Ndururu kweli?
 
Unguja ndani ya kanisa. Kanisa akitumia mwarabu?
Kanisa lilikuja kujengwa baada kukomeshwa kwa Biashara ya Utumwa na European Power British Empire.

Hii picha inaonyesha Biashara ya Utumwa huko Uarabuni👇
220px-Slaves_Zadib_Yemen_13th_century_BNF_Paris.jpg

Hao Weusi kuna uwezekano mkubwa ni East Africans japokuwa kulikuwa na Njia zingine za Sahara.
 
Kanisa lilikuja kujengwa baada kukomeshwa kwa Biashara ya Utumwa na European Power British Empire.

Hii picha inaonyesha Biashara ya Utumwa huko Uarabuni👇
View attachment 2945403
Hao Weusi kuna uwezekano mkubwa ni East Africans japokuwa kulikuwa na Njia zingine za Sahara.
Ukiingia kanisani utaona mashimo ya watumwa wakifungwa humo. Propaganda zenu mliwadanganya mababu zetu..hivi sasa hii jamii nyengine
 
Ukiingia kanisani utaona mashimo ya watumwa wakifungwa humo. Propaganda zenu mliwadanganya mababu zetu..hivi sasa hii jamii nyengine
Hilo eneo lilijengwa Kanisa lilikuwa ni Soko la Watumwa wa Kiafrika hapo Unguja.

Watumwa walikuwa wakipelekwa hadi "Bwaga Moyo" ambayo ndio hii leo tuiita Bagamoyo Mkoa wa Pwani Tanganyika.

Kuna Vitabu vingi vimeandikwa kuhusu hili la Biashara ya Utumwa hata Mwanahistoria mkubwa wa Jamii ya Kiislamu Ibin Batuta aliiongelea hili sasa wewe unakataa bila ushahidi wowote lengo na nia yako ni nini?
 
Tuanze na Waarabu miungu wako waliobaka wazee wetu pwani na kupandikiza dini yao hiyo.
 
Huko West Africa Wazungu wanaweza kulipa hapa Africa ya Mashariki kama tujuavyo ni Waarabu ndio walitusomba kwenda Utumwani je hawa Waarabu watalipa hata Ndururu kweli?
Ulimezeshwa upuuzi tu ulipokua darasa la 7 b.
Hakuna ushahidi wa moja kwa moja unao muhusisha mwarabu na biashara ya utumwa.
 
Tunazungumza Moshi ambao bibi yako alifanywa ntumwa. Nani alimfanya mtumwa wakati waarabu huko hawajatia mguu?
Bro acha ubishi ulishawahi sikia Zanj rebellion huko middle East kwa hao unaowatetea au unamjua tipp tippu
 
Moshi mbeya wamebakwa na wazungu

Ujerumani yaomba radhi kwa ukoloni wake Afrika Mashariki
 
Back
Top Bottom