Magufuli: DPP aliichezea kesi ya ''samaki wa Magufuli''

Magufuli: DPP aliichezea kesi ya ''samaki wa Magufuli''

Sasa kama muda ulikwisha hawezi kuniaminisha mm great thinker kuwa eti sijui nani alifanya ashindwe kesi. Labda ni njia ya kujisafisha ili aonekane anamaamuzi mazuri ambayo hayaliingizi taifa kwenye hasara. Vipi kuhusu sukari? Nani kasababisha emefeli? Msiongozwe na ushabiki. Lazima Muwe mnatumia akili zenu
Wewe unayewaambia wengine watumie akili inawezekana wewe ndiye hutumii hata common sense!
 
Sasa kama muda ulikwisha hawezi kuniaminisha mm great thinker kuwa eti sijui nani alifanya ashindwe kesi. Labda ni njia ya kujisafisha ili aonekane anamaamuzi mazuri ambayo hayaliingizi taifa kwenye hasara. Vipi kuhusu sukari? Nani kasababisha emefeli? Msiongozwe na ushabiki. Lazima Muwe mnatumia akili zenu

daa nimecheka kweli yaani pamoja na utumbo wako huo unaonuka kila mahali halafu unajiita GT ?
 
Sasa kama muda ulikwisha hawezi kuniaminisha mm great thinker kuwa eti sijui nani alifanya ashindwe kesi. Labda ni njia ya kujisafisha ili aonekane anamaamuzi mazuri ambayo hayaliingizi taifa kwenye hasara. Vipi kuhusu sukari? Nani kasababisha emefeli? Msiongozwe na ushabiki. Lazima Muwe mnatumia akili zenu
Unajiaunajiaibsha humu, rudi Labour.
Tunaongelea Samaki unakuja na Sukari, hujioni una mapungufu?
 
NI DPP tu hawa jamaa wengi wajeshi la polisi ni kama hivyo majanga serikali inahitaji kujituma hasa
 
Uandishi wa habari wa bongo ni shida. Hauna kujiongeza hata kidogo. Mwandishi hajatoa hata ufafanuzi nani alikuwa DPP wakati wa kesi ya samaki na kwa sasa yuko wapi. Ninavyojua mimi, moja ya viongozi wa mwanzo kutumbuliwa na Magufuli alikuwa DPP, hivyo hayupo tena yule wa samaki wa Magufuli. Sasa waandishi walitakiwa waje na majina-yupi wa zamani, yupi wa sasa.
 
Rais Magufuli amemtuhumu DPP kwa kuichezea kesi inayojulikana kama kesi ya ''samaki wa Magufuli'' ili serikali ishindwe mahakamani.

Kesi hiyo ilipewa jina hilo kwa sababu washitakiwa 36 kutoka mataifa tofauti, waliokuwa wakikabiliwa na kesi hiyo walikamatwa wakati John Magufuli akiwa katika Waziri katika Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi na alishiriki kwa karibu katika tukio hilo.

Rais ameyasema hayo wakati alipokuwa akifungua kikao cha kazi cha makamanda wa polisi wa mikoa, mawakili wafawidhi wa serikali wa mikoa na wakuu wa upelelezi wa Mikoa.

Rais Magufuli amesema DPP aliondoa makosa 19 ambayo yangewafunga watuhumiwa na kubakiza kosa moja lakini baadaye akaamua kwenda kulalamika kwa Jaji Mkuu ambapo baadaye yaliongezwa na kuwa makosa matatu.

Rais amesema huo mchezo ulikuwa unachezwa kwenye ofisi ya DPP ili serikali ishindwe Mahakamani kwa sababu ambazo anazifahamu DPP.

Wakati wa sakata la ''samaki wa Magufuli'', Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) alikuwa ni Eliezer Feleshi ambaye August 2014 aliteuliwa na Rais Kikwete kuwa Jaji wa Mahakama Kuu. Kwa sasa Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) ni Biswalo Mganga ambaye aliteuliwa October 2014.

Rais alisema kuna kesi za mafisadi toka mwaka 2009 hazijapelekwa mahakamani lakini kesi za wezi wa kuku hazichukui muda mrefu kupelekwa mahakamani.

Rais amewambia DPP, Biswalo Mganga kujipanga vizuri ili atende haki kwa wananchi wote kwa sababu ofisi yake huondoa kesi au makosa yanayoonekana kuwafunga mafisadi.

''Ni lazima niseme ukweli ili mfahamu mwelekeo wa serikali ya sasa'' alisema.

Kesi ya samaki wa Magufuli ilisharipotiwa hapa;

Na Hapa;


VIDEO YA HOTUBA YA RAIS MAGUFULI:


NOTA BENE:
Kumbe tulikuwa tunatoa lawama kwa Magufuli kuhusu serikali kushindwa hii kesi ya ''samaki wa Magufuli'' bila kufahamu hali halisi ilivyokuwa katika kutayalisha mashitaka.

Tumemkaanga sana Magufuli kwenye hili suala kumbe tatizo lilikuwa kwenye ofisi ya DPP.

Ama kweli, jambo usilolijua ni kama usiku wa giza!

Hili ni ukweli mtupu,DPP Feleshi...alishiriki kikamilifu kuharibu ushahidi.
 
Nadhani humfahamu vizuri Jaji Dkt Feleshi wewe, kama kunamwanasheria muadilifu hata mmoja alobakia hapa Tanzania basi ni Feleshi, niliwahi kusema hapa natamani sana Feleshi angefanya kazi na Magufuli akiwa kama DPP nchi ingenyooka hii, kama unajua Ikulu ilikuwa inamuingilia then unatoa wapi ujasiri wa kumtuhumu Feleshi?
Tuhuma za Rais Magufuli ni nzito hasa ikichukuliwa zimetolewa na kiongozi mkuu wa nchi na Amiri Jeshi Mkuu.

Kwa nini Jaji Feleshi hakusema ukweli kwa Waziri Magufuli hata kama kulikuwa na shinikizo kwenye kesi?
 
Magufuli is a straight foward man...he doesnt beat around the bush! Ofisi ya DPP imelalamikiwa miaka mingi sana...
Nimenuna kupita maelezo kwa insight hii!yaani kumbe machi madogo walikuwa wananyea debe for sure ila ndio figisu za mamlaka tu zimewatoa
 
Tuhuma za Rais Magufuli ni nzito hasa ikichukuliwa zimetolewa na kiongozi mkuu wa nchi na Amiri Jeshi Mkuu.

Kwa nini Jaji Feleshi hakusema ukweli kwa Waziri Magufuli hata kama kulikuwa na shinikizo kwenye kesi?
Hakuwa akiwajibika kwake, hivi hili nalo ni la kumlaumu DPP? sio kazi ya DPP kukusanya ushahidi, yule ni mtaalamu wa kisheria naamini aliona serikali ikianguka mahakamani lakini kutokana na shinikizo la waziri ikalazimika kumlizisha na ndo maana hata hayo mashitaka aloongeza baada ya kushinikizwa na CJ (kwa mujibu wa JPM) yalishindwa kuthibitika mahakamani, wapelelezi wetu ni jipu na hii ni sehemu ambayo Jaji Feleshi anapaswa kupongezwa baada ya kuleta mabadiliko makubwa ya kuwaondoa maaskali polisi mahakamani ili wajikite kwenye ukusanyaji wa ushahidi pekee na sio kuendesha mashtaka, ni busala sasa JPM kuuliza nini kilitokea kuliko kurusha madongo tu tena kwa mtu muhimu kama yule.
 
Mtoa post unaamini vp kama huo ni ukweli?
Vp kwani ni mara ya kwanza ngosha kushindwa kesi?
 
Rais Magufuli amemtuhumu DPP kwa kuichezea kesi inayojulikana kama kesi ya ''samaki wa Magufuli'' ili serikali ishindwe mahakamani.

Kesi hiyo ilipewa jina hilo kwa sababu washitakiwa 36 kutoka mataifa tofauti, waliokuwa wakikabiliwa na kesi hiyo walikamatwa wakati John Magufuli akiwa katika Waziri katika Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi na alishiriki kwa karibu katika tukio hilo.

Rais ameyasema hayo wakati alipokuwa akifungua kikao cha kazi cha makamanda wa polisi wa mikoa, mawakili wafawidhi wa serikali wa mikoa na wakuu wa upelelezi wa Mikoa.

Rais Magufuli amesema DPP aliondoa makosa 19 ambayo yangewafunga watuhumiwa na kubakiza kosa moja lakini baadaye akaamua kwenda kulalamika kwa Jaji Mkuu ambapo baadaye yaliongezwa na kuwa makosa matatu.

Rais amesema huo mchezo ulikuwa unachezwa kwenye ofisi ya DPP ili serikali ishindwe Mahakamani kwa sababu ambazo anazifahamu DPP.

Wakati wa sakata la ''samaki wa Magufuli'', Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) alikuwa ni Eliezer Feleshi ambaye August 2014 aliteuliwa na Rais Kikwete kuwa Jaji wa Mahakama Kuu. Kwa sasa Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) ni Biswalo Mganga ambaye aliteuliwa October 2014.

Rais alisema kuna kesi za mafisadi toka mwaka 2009 hazijapelekwa mahakamani lakini kesi za wezi wa kuku hazichukui muda mrefu kupelekwa mahakamani.

Rais amewambia DPP, Biswalo Mganga kujipanga vizuri ili atende haki kwa wananchi wote kwa sababu ofisi yake huondoa kesi au makosa yanayoonekana kuwafunga mafisadi.

''Ni lazima niseme ukweli ili mfahamu mwelekeo wa serikali ya sasa'' alisema.

Kesi ya samaki wa Magufuli ilisharipotiwa hapa;

Na Hapa;


VIDEO YA HOTUBA YA RAIS MAGUFULI:
Kama una Megabyte ndogo angalia kuanzia dakika ya 14:20


NOTA BENE:
Kumbe tulikuwa tunatoa lawama kwa Magufuli kuhusu serikali kushindwa hii kesi ya ''samaki wa Magufuli'' bila kufahamu hali halisi ilivyokuwa katika kutayalisha mashitaka.

Tumemkaanga sana Magufuli kwenye hili suala kumbe tatizo lilikuwa kwenye ofisi ya DPP.

Ama kweli, jambo usilolijua ni kama usiku wa giza!

Sasa kama Mashtaka hayana mashiko unalazimishaje kushinda kesi?

Halafu kilichompeleka kwa Jaji Mkuu ni nini? Haoni kama alikuwa ana influence decision za Mahakama wakati yeye sio mwanasheria?

Tangu lini mlalamikaji akaenda kwa Jaji Mkuu kulalamika badala ya kukata rufaa kisheria?

Alikuwa wapi kukata rufaa, mpaka leo kawa Rais anatulalamikia sisi wananchi?
 
Ana bahati kwa kuwa ni Jaji vinginevyo angekuwa tayari katumbuliwa!!
DPP ni kama Jaji, sio rahisi kumtumbua, pia ukifikia hatua ya kumtumbua mtu kama Feleshi basi jitafakari mala mbilimbili.

Uliza mwanasheria yeyote wa serikali atakueleza boss wao huyo wa zamani ni mtu wa aina gani, Feleshi ni mwadilifu na mchapa kazi hasa, licha ya kuwa boss lakini kila siku ukitoa jpili lazima saa kumi na moja alfajiri yumo ofisini na anaondoka saa mbili usiku, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, hakuna mtu angethubutu kumpa rushwa Feleshi maana hata huo ujasiri sijui unaupata wapi.

Hii ni kama tu ile issue ya UDA watu walimsema sana humu eti alihongwa ndo maana akaiondoa kesi mahakamani baada ya watu kuelezwa nini kilitokea ndo wakaona kumbe si mtu wa kuwa compromised na ndo wakagundua Hossea alikuwa mtu wa aina gani.
 
Magufuli is a straight foward man...he doesnt beat around the bush! Ofisi ya DPP imelalamikiwa miaka mingi sana...
Ni kweli na naamini kabisa alilosema magufuli. Dpp amelinda sana watu wenye nazo angali wahalifu wadogo wakiwa ndio pekee wanaumia. Ofisi ya Dpp ni jipu la muda mrefu.
 
Back
Top Bottom