Magufuli: DPP aliichezea kesi ya ''samaki wa Magufuli''

Magufuli: DPP aliichezea kesi ya ''samaki wa Magufuli''

Wakuligo

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2013
Posts
259
Reaction score
106
Rais akiongea na viongozi wa juu wa jeshi la polisi ameeleza jinsi serikali ilivyoshindwa kesi ya samaki. Eti makosa yalikuwa 19, cha ajabu DPP alipeleka moja tuu. Magufuli akalalamika kwa mwanasheria mkuu, wakapeleka tena mengine matatu na jamaa wakashinda kiulaini.

Kituko kingine, eti kuna mke wa waziri kamtukana traffic polisi wakati kitekeleza majukum yake, rais ameagiza hyo askari apandishwe cheo na pia ameshaongea na hyo waziri kumuonya.

Rais ameongea kwa uchungu mambo kibao yanayoumiza yaliyokuwa yakifanywa na baadhi ya askari wachache na kusababisha hasara kubwa kwa taifa.

Chanzo: Kipindi cha Makala ya Rais, TBC.

Rais Magufuli amemtuhumu DPP kwa kuichezea kesi inayojulikana kama kesi ya ''samaki wa Magufuli'' ili serikali ishindwe mahakamani.

Kesi hiyo ilipewa jina hilo kwa sababu washitakiwa 36 kutoka mataifa tofauti, waliokuwa wakikabiliwa na kesi hiyo walikamatwa wakati John Magufuli akiwa Waziri katika Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi na alishiriki kwa karibu katika tukio hilo.

Rais ameyasema hayo wakati alipokuwa akifungua kikao cha kazi cha makamanda wa polisi wa mikoa, mawakili wafawidhi wa serikali wa mikoa na wakuu wa upelelezi wa Mikoa.

Rais Magufuli amesema DPP aliondoa makosa 19 ambayo yangewafunga watuhumiwa na kubakiza kosa moja lakini baadaye akaamua kwenda kulalamika kwa Jaji Mkuu ambapo baadaye yaliongezwa na kuwa makosa matatu.

Rais amesema huo mchezo ulikuwa unachezwa kwenye ofisi ya DPP ili serikali ishindwe Mahakamani kwa sababu ambazo anazifahamu DPP.

Wakati wa sakata la ''samaki wa Magufuli'', Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) alikuwa ni Eliezer Feleshi ambaye August 2014 aliteuliwa na Rais Kikwete kuwa Jaji wa Mahakama Kuu. Kwa sasa Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) ni Biswalo Mganga ambaye aliteuliwa October 2014.

Rais alisema kuna kesi za mafisadi toka mwaka 2009 hazijapelekwa mahakamani lakini kesi za wezi wa kuku hazichukui muda mrefu kupelekwa mahakamani.

Rais amewambia DPP, Biswalo Mganga kujipanga vizuri ili atende haki kwa wananchi wote kwa sababu ofisi yake huondoa kesi au makosa yanayoonekana kuwafunga mafisadi.

''Ni lazima niseme ukweli ili mfahamu mwelekeo wa serikali ya sasa'' alisema.

Kesi ya samaki wa Magufuli ilisharipotiwa hapa;

Na Hapa;


VIDEO YA HOTUBA YA RAIS MAGUFULI:
Kama una Megabyte ndogo angalia kuanzia dakika ya 14:20


NOTA BENE:
Kumbe tulikuwa tunatoa lawama kwa Magufuli kuhusu serikali kushindwa hii kesi ya ''samaki wa Magufuli'' bila kufahamu hali halisi ilivyokuwa katika kutayalisha mashitaka.

Tumemkaanga sana Magufuli kwenye hili suala kumbe tatizo lilikuwa kwenye ofisi ya DPP.

Ama kweli, jambo usilolijua ni kama usiku wa giza!
 
Kuna mtu alimtukana RAISI akashikwa vepe uyo mama mke wa waziri kashikwa au sheria zetu double standard na zakifala
 
Huyo DPP alie husika na kesi ya samaki wa Ma[emoji356] ajiandae kutumbuliwa tua aiseee....
 
Mahakama zetu nazo zisiwe rigid, mabilioni yalitumika kuwahifadhi wasiharibike eti kisa kutunza ushahidi, wakati ushahidi unaweza kupigwa picha ya video
 
Hahahahaaa Magu acha kuzuga na mambo ya kesi, kama hasara umeshatupa na hatuta lisahau hili na nyumba zetu ulizogawa ovyo ovyo na Mv dar, tutapambana tuondoe kinga ya rais kushtakiwa kwenye katiba mpya,!! Nakushaur pambana mfumuko wa bei, watanzania wamechoka na comedy za majipu
 
Kuna mtu alimtukana RAISI akashikwa vepe uyo mama mke wa waziri kashikwa au sheria zetu double standard na zakifala
Thubutu! Some people are untouchable , former waziri mkuu Mizengo Pinda analijua hili. Sheria msumeno Kenya tu - The Baraza-Kerubo Village Market Incident
refers to an incident between the then Kenyan
Deputy Chief Justice Nancy Makokha Baraza
and Rebecca Kerubo who worked as a guard
at the Village Market shopping mall in Nairobi.
The incident led to the suspension and
subsequent resignation of the Deputy Chief
justice after less than one year in office.
 
Rais Magufuli amemtuhumu DPP kwa kuichezea kesi inayojulikana kama kesi ya ''samaki wa Magufuli'' ili serikali ishindwe mahakamani.

Kesi hiyo ilipewa jina hilo kwa sababu washitakiwa 36 kutoka mataifa tofauti, waliokuwa wakikabiliwa na kesi hiyo walikamatwa wakati John Magufuli akiwa Waziri katika Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi na alishiriki kwa karibu katika tukio hilo.

Rais ameyasema hayo wakati alipokuwa akifungua kikao cha kazi cha makamanda wa polisi wa mikoa, mawakili wafawidhi wa serikali wa mikoa na wakuu wa upelelezi wa Mikoa.

Rais Magufuli amesema DPP aliondoa makosa 19 ambayo yangewafunga watuhumiwa na kubakiza kosa moja lakini baadaye akaamua kwenda kulalamika kwa Jaji Mkuu ambapo baadaye yaliongezwa na kuwa makosa matatu.

Rais amesema huo mchezo ulikuwa unachezwa kwenye ofisi ya DPP ili serikali ishindwe Mahakamani kwa sababu ambazo anazifahamu DPP.

Wakati wa sakata la ''samaki wa Magufuli'', Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) alikuwa ni Eliezer Feleshi ambaye August 2014 aliteuliwa na Rais Kikwete kuwa Jaji wa Mahakama Kuu. Kwa sasa Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) ni Biswalo Mganga ambaye aliteuliwa October 2014.

Rais alisema kuna kesi za mafisadi toka mwaka 2009 hazijapelekwa mahakamani lakini kesi za wezi wa kuku hazichukui muda mrefu kupelekwa mahakamani.

Rais amewambia DPP, Biswalo Mganga kujipanga vizuri ili atende haki kwa wananchi wote kwa sababu ofisi yake huondoa kesi au makosa yanayoonekana kuwafunga mafisadi.

''Ni lazima niseme ukweli ili mfahamu mwelekeo wa serikali ya sasa'' alisema.

Kesi ya samaki wa Magufuli ilisharipotiwa hapa;
Na Hapa;

VIDEO YA HOTUBA YA RAIS MAGUFULI:
Kama una Megabyte ndogo angalia kuanzia dakika ya 14:20


NOTA BENE:
Kumbe tulikuwa tunatoa lawama kwa Magufuli kuhusu serikali kushindwa hii kesi ya ''samaki wa Magufuli'' bila kufahamu hali halisi ilivyokuwa katika kutayalisha mashitaka.

Tumemkaanga sana Magufuli kwenye hili suala kumbe tatizo lilikuwa kwenye ofisi ya DPP.

Ama kweli, jambo usilolijua ni kama usiku wa giza!
 
Magufuli is a straight foward man...he doesnt beat around the bush! Ofisi ya DPP imelalamikiwa miaka mingi sana...
Kumbe hata Rais Magufuli alishailalamikia ofisi ya DPP.

Kumbe tulishindwa kesi kwa sababu ya DDP alitaka serikali ishindwe kesi.
 
Back
Top Bottom