Madiwani wa CHADEMA Arusha wagawanyika

Madiwani wa CHADEMA Arusha wagawanyika

Ngongo,

Mkuu wangu labda kwa sababu watu wengine kama sisi hatuchangii sakata lenu ndio maana unafikiri unachokiandika kina maana. Madiwani ni wawakilishi na watekelezaji wa sera na ilani za chama kama chama kilivyowaahidi wananchi, na hawawezi kuchukua jukumu la kuingia Mufaka na CCM pasipo kuwasiliana na makao makuu ya chama ktk kupanga jinsi ya kutumia fursa walizopata...
Unachoshindwa kufahamu ni kwamba hata kabla ya muafaka wananchi walipinga hatua zozote za chama tawala kujipa vyeo vya juu ktk uongozi wa Halamashauri ya mji huo na ilifikia hadi wananchi kupoteza roho zao kupinga kile ambacho leo hawa madiwani wamekikubali.

Kwa hiyo hawa madiwani kwanza hawana ridhaa ya wananchi wala makao makuu hawana taarifa yeyote kuhusiana na makubaliano baina yao na madiwani waCCM..kisha wewe unataka kusema hili sio swala kubwa bali ni matatizo binafsi kati ya Lema na Mallah na ukaacha nje sababu hizi.. Na zaidi ya hapo unashindwa kabisa kuelewa kwamba diwani yeyote anaifanya kazi ya chama na sii yake binafsi au iliyopangwa na CCM. Na kikubwa zaidi pengine unashindwa kuelewa madaraka na mamlaka alokuwa nayo Meya ktk utendaji kazi kiasi kwamba wewe unaona hakuna tatizo kwa CDM kukubali nafasi walizopewa na CCM..

Hawa Madiwani walichokifanya hakina tofauti na Muafaka wa Zanzibar ambao Seif Hamad alikubali kuchukua rushwa la vyeo na Nnauye majuzi tu kasema tamaa yake ndio ilimponza. Tofauti iliyopo ni kwamba Seif alipata ridhaa ya Wazanzibar lakini sio ridhaa ya wanaCUF hasa wa bara. Na kwa mtaji huo Seif alikiuka sheria na taratibu za chama kwa kuunda Uzanzibar dhidi ya Ubara ndani ya chama. Bara hawakuridhia muafaka ule na matokeo yake CUF wamekosa viti bara na pengine chama ndio kinakufa bara kwa faida ndogo ya kupewa vyeo ktk wizara na taasisi ambazo hazina mamlaka ya kuleta mageuzi ambayo wananchi wa Zanzibar waliyategemea...

Hawa madiwani kwa jeuri wametoa majibu ambayo wao hawakutakiwa kabisa kuyasema tena wakiita waandishi wa magazeti kujibu maamuzi ya makao makuu. Huu ni utovu wa adabu, kukosa hekima na shukran kwa chama na wananchi waliowapa nafasi hizo..Ni jeuri ambayo tumeizoea kuiona toka CCM ambapo viongozi wabunge, madiwani na hata makatibu kata wanapopewa dhamana hizi hugeuka na kuwa wajeuri wakapenda kuheshimiwa kama Waheshimiwa na hubadilika toka mwendo, mavazi na makazi yao..

Hatutaki viongozi kama hawa! kama wanafikiria mila na desturi ya jeuri wanazowaona viongozi wa CCM wakizifanya kwa wananchi basi wakumbuke kwamba CDM ni chama cha wananchi na nguvu imepelwa wananchi ambao waliingia barabarani kwa maandamano kupinga hicho hicho walichokubali wao pasipo ridhaa ya wananchi, kisha wanatafuta wachawi toka makao makuu hali wachawi ni wao wenyewe..
 
FaizaFoxy habari za leo ndugu yangu,Kwanza umesema muafaka ulifikiwa kati ya Mbowe na Pinda.sasa unasema Mabere Nyaucho Marando kwenye ripoti yake amewasafisha Madiwani kuhusika na ushawishi kwa Rushwa. Sina uhakika na Ripoti ya Marandu kwani sijaisoma wala muafaka wa Mbowe na Pinda kwani sio Pinda wala Mbowe wamekiri huo Muafaka.Akiwa waziri wa Fedha professa Mbilinyi na Naibu wake mporogonyi walitakiwa kujiuzulu kwa kupokea rushwa ya minofu ya samaki. Ushahidi ulikuwa ni wa kimazingira.Nikiwa ni mwana CDM mwaminifu nisiyependa migogoro ndani ya Chama changu. Nina amini kabisa mazingira ya muafaka kati ya madiwani wa CDM, CCM, na TLP kulikuwa na mazingira ya rushwa, ama ya fedha, vyeo ama kuahidiwa nafasi zaidi ndani ya jiji. Ama rushwa ya kibiashara, tender nk. Kulikuwa na uharaka gani kutangazwa kwa muafaka bila kuwepo ushiriki wa kutoka cdm wilaya, mkoa?Ripoti ya marandu ndio iliyosema muafaka ni batili na wale Madiwani wanatakiwa kujiuzulu nafasi zao. Mpaka sasa hawajaiweka wazi ripoti ile kwani yale ni mambo ya ndani ya chama. Kama wamekaidi kutenda maazimio ya ripoti ni wazi watakuwa tayari na kadi za CCM mfukoni. Tutakutana kwenye uchaguzi mdogo wa madiwani Arusha na Ubunge igunga.
Kwanza unasema "sina uhakika na ripoti ya Marandu" baadae kidogo unasema "Ripoti ya marandu ndio iliyosema muafaka ni batili". Duhh, huoni kuwa huo mchakachuo tena heavy. Sasa amua moja kati ya hayo ya ripoti ya Marandu.
 
Mkandara,

Mkuu wangu napenda kukufahamisha mimi si mwakilishi wa mtu au kundi lolote.Ngongo nimtu huru hafungwi wala hafungamani na chama chochote.

Madiwani ni wawakilishi wa wananchi katika halmashauri.Diwani bila kujali katokea chama gani akishachaguliwa anawawakilisha wananchi walimchagua na waliomkataa [wengi wa wananchi si wanachama wa vyama vya siasa].Nakubaliana na wewe madiwani ni watekelezaji wa sera na ilani wa vyama.
Madiwani hawakujivika majukumu ya kuingia muafaka na CCM wala sijasikia mahali popote CHADEMA wakilalamikia hilo.Kinacholalamikiwa ni maudhui ya muafaka mkuu na si ushiriki wao kwenye muafaka.Makao makuu walikuwa na taarifa za kinachoendela na walishiriki uandaaji wa hadidu za rejea eg OCD afukuzwe kazi,Mkurugenzi wa Jiji afukuzwe kazi,Uchaguzi wa Meya urudiwe na nk au unadhani Mallah alijitungia na ikiwa alifanya kwanini tume ya Marando haikumtia hatiani ?.

Unadai madiwani kwa jeuri wametoa majibu amabyo hawakutakiwa kabisa kuyasema.Nakubalina na wewe lakini Lema na Dr Slaa walipowatuhumu kupokea mlungula pasipo ushahidi ilikuwa sahihi ?.Mkandara kama umebaini kosa la Madiwani kwanini huoni kosa la Lema na Dr Slaa ?.

Unadai hamuawataki viongozi kama hao [Madiwani]. Mimi sipendi viongozi wenye nidhamu ya uoga wasio na uwezo wa kuhoji hata haki zao za msingi.Viongozi wa ndiyo mzee/mwenyekiti ndiyo wameifikisha nchi yetu mahali pagumu.




Ngongo,

Mkuu wangu labda kwa sababu watu wengine kama sisi hatuchangii sakata lenu ndio maana unafikiri unachokiandika kina maana. Madiwani ni wawakilishi na watekelezaji wa sera na ilani za chama kama chama kilivyowaahidi wananchi, na hawawezi kuchukua jukumu la kuingia Mufaka na CCM pasipo kuwasiliana na makao makuu ya chama ktk kupanga jinsi ya kutumia fursa walizopata...
Unachoshindwa kufahamu ni kwamba hata kabla ya muafaka wananchi walipinga hatua zozote za chama tawala kujipa vyeo vya juu ktk uongozi wa Halamashauri ya mji huo na ilifikia hadi wananchi kupoteza roho zao kupinga kile ambacho leo hawa madiwani wamekikubali.

Kwa hiyo hawa madiwani kwanza hawana ridhaa ya wananchi wala makao makuu hawana taarifa yeyote kuhusiana na makubaliano baina yao na madiwani waCCM..kisha wewe unataka kusema hili sio swala kubwa bali ni matatizo binafsi kati ya Lema na Mallah na ukaacha nje sababu hizi.. Na zaidi ya hapo unashindwa kabisa kuelewa kwamba diwani yeyote anaifanya kazi ya chama na sii yake binafsi au iliyopangwa na CCM. Na kikubwa zaidi pengine unashindwa kuelewa madaraka na mamlaka alokuwa nayo Meya ktk utendaji kazi kiasi kwamba wewe unaona hakuna tatizo kwa CDM kukubali nafasi walizopewa na CCM..

Hawa Madiwani walichokifanya hakina tofauti na Muafaka wa Zanzibar ambao Seif Hamad alikubali kuchukua rushwa la vyeo na Nnauye majuzi tu kasema tamaa yake ndio ilimponza. Tofauti iliyopo ni kwamba Seif alipata ridhaa ya Wazanzibar lakini sio ridhaa ya wanaCUF hasa wa bara. Na kwa mtaji huo Seif alikiuka sheria na taratibu za chama kwa kuunda Uzanzibar dhidi ya Ubara ndani ya chama. Bara hawakuridhia muafaka ule na matokeo yake CUF wamekosa viti bara na pengine chama ndio kinakufa bara kwa faida ndogo ya kupewa vyeo ktk wizara na taasisi ambazo hazina mamlaka ya kuleta mageuzi ambayo wananchi wa Zanzibar waliyategemea...

Hawa madiwani kwa jeuri wametoa majibu ambayo wao hawakutakiwa kabisa kuyasema tena wakiita waandishi wa magazeti kujibu maamuzi ya makao makuu. Huu ni utovu wa adabu, kukosa hekima na shukran kwa chama na wananchi waliowapa nafasi hizo..Ni jeuri ambayo tumeizoea kuiona toka CCM ambapo viongozi wabunge, madiwani na hata makatibu kata wanapopewa dhamana hizi hugeuka na kuwa wajeuri wakapenda kuheshimiwa kama Waheshimiwa na hubadilika toka mwendo, mavazi na makazi yao..

Hatutaki viongozi kama hawa! kama wanafikiria mila na desturi ya jeuri wanazowaona viongozi wa CCM wakizifanya kwa wananchi basi wakumbuke kwamba CDM ni chama cha wananchi na nguvu imepelwa wananchi ambao waliingia barabarani kwa maandamano kupinga hicho hicho walichokubali wao pasipo ridhaa ya wananchi, kisha wanatafuta wachawi toka makao makuu hali wachawi ni wao wenyewe..
 
Mkandara,

Mkuu wangu napenda kukufahamisha mimi si mwakilishi wa mtu au kundi lolote.Ngongo nimtu huru hafungwi wala hafungamani na chama chochote.

Madiwani ni wawakilishi wa wananchi katika halmashauri.Diwani bila kujali katokea chama gani akishachaguliwa anawawakilisha wananchi walimchagua na waliomkataa [wengi wa wananchi si wanachama wa vyama vya siasa].Nakubaliana na wewe madiwani ni watekelezaji wa sera na ilani wa vyama.
Madiwani hawakujivika majukumu ya kuingia muafaka na CCM wala sijasikia mahali popote CHADEMA wakilalamikia hilo.Kinacholalamikiwa ni maudhui ya muafaka mkuu na si ushiriki wao kwenye muafaka.Makao makuu walikuwa na taarifa za kinachoendela na walishiriki uandaaji wa hadidu za rejea eg OCD afukuzwe kazi,Mkurugenzi wa Jiji afukuzwe kazi,Uchaguzi wa Meya urudiwe na nk au unadhani Mallah alijitungia na ikiwa alifanya kwanini tume ya Marando haikumtia hatiani ?.

Unadai madiwani kwa jeuri wametoa majibu amabyo hawakutakiwa kabisa kuyasema.Nakubalina na wewe lakini Lema na Dr Slaa walipowatuhumu kupokea mlungula pasipo ushahidi ilikuwa sahihi ?.Mkandara kama umebaini kosa la Madiwani kwanini huoni kosa la Lema na Dr Slaa ?.

Unadai hamuawataki viongozi kama hao [Madiwani]. Mimi sipendi viongozi wenye nidhamu ya uoga wasio na uwezo wa kuhoji hata haki zao za msingi.Viongozi wa ndiyo mzee/mwenyekiti ndiyo wameifikisha nchi yetu mahali pagumu.

Mkuu hapo nilipopigia mstari ndipo unapokosea..inaonyesha wazi hujui siasa na utekelezaji wake ama niseme siasa zinatumika vipi ktk ujenzi wa Taifa.. Nimekuandikia huko nyuma kuhusu kiongozi bora na vision yake ambayo inatokana na nidhamu ya maadili..nimekupa hata kanuni za chama cha CCM kuhusiana na swala hili hili...Diwani yeyote ktk utekelezaji wake inamlazimu kutekeleza ILANI za chama chake kwa sababu ndizo alizowaahidi wananchi na sii sura yake.

Kisha, hakuna mtu anazungumzia uchaguzi wa madiwani bali tunazungumzia uchaguzi ktk uongozi wa Halmashauri ya mji wa Arusha, usichanganye vitu hivi..Swala lililopo ubaoni ni MAAMUZI ya muafaka (makubaliano) waliofikia hawa madiwani baina yao na wale wa CCM ktk kugawana madaraka ya uongozi huo.. Kama kweli una uhakika makao makuu walikuwa na taarifa za maamuzi yao ktk muafaka huu ilikuwaje tena waambiwe wajiondoe ktk nyadhifa za uongozi wa Halmashauri?..

Na kama haya yote ni kweli wananchi waliafiki matokeo haya? unaweza kunambia ridhaa hiyo hawa Madiwani wameipata toka wapi na lini maana nijuavyo mimi wananchi walifanya maandamano kupinga kuchaguliwa kwa MEYA wa CCM toka mwanzo na wengine wakapoteza maisha. Je, ni lini hawa madiwani waliwauliza wananchi hadi wao kufikia maamuzi waliyofikia ktk muafaka huu..

Halafu maandalizi ya hadidu rejea ambazo unazungumzia hapo juu zilihusu matokeo (the aftermath) ya maandamano na baadhi ya wanachama wa CDM walipoteza maisha. Hii ilihusu uvunjaji wa sheria ya haki za binadamu na hakuna mahala popote panapoonyesha makao makuu waliridhia na matokeo ya uchaguzi wowote..

Kisha unajichanganya mwenyewe unaposema makao makuu walikuwa na habari ya muafaka huu, mkuu wangu lazima uelewe tunachozungumzia. Kwa mfano:- Kuwa na taarifa ya kuwepo kwa mazungumzo baina ya wajumbe wa CDM na CCM haipotezi maana ya matumaini ya msimamo wa chamai kuchukua nafasi ya ushindi.. Leo hii Obama huko Marekani anapata taabu ya kupitisha bajeti ya kupunguza madeni kwa sababu gani?.. Republican wanaendelea kusimamia kile walichowaahidi wananchi wao hata kama walishindwa Uchaguzi ktk kiti cha Urais.

Huwezi kubadilika badilika na kuanza kupitisha sera za chama kingine hata kama kiitikadi hukubaliani nazo na ndicho kinachomwangusha Obama leo kwani kuna baadhi ya sera za Republican amezikubali, i.e kukata matuymizi ktk Healthcare iende sambamba na kuongeza kodi za matajiri.. Kwa mtaji huo kapoteza baadhi ya kura za chama chake kwa sababu katoka ktk maadili ya chama kuhusiana na helathcare, wakati huo huo amekosa support ya Republican ambao hawawezi kukubali kuongezwa kodi kwa matajiri. Republican hawawezi kubadilisha msimamo wao isipokuwa washindwe kwa kura tu.
Huu ni mfano tu kukuonyesha kwamba makao makuu ya CDM walitegemea hawa madiwani watawakilisha yapi ktk muafaka huo na kuhakikisha hawapotezi haki yao kuongoza Halmashauri.

Kwa hiyo swala zima sio kuwepo kwa muafaka au mazungumzo baina ya wajumbe wa CCM na CDM kuhusiana na nafasi za uongozi wa halmshauri ila ni maamuzi ya hawa madiwani kinyume cha wananchi na chama. Makao makuu kwa kuzingatia matakwa ya wananchi bila kujali nani kaleta malalamiko hayo ndio wamefikia uamuzi wa hawa madiwani kujitoa ktk uongozi wa Halmshauri.

Madiwani wanachaguliwa na wananchi kwa SABABU na sababu zenyewe ni sera na ilani zao kwa wananchi kwani hawakuchaguliwa kutokana na sura zao..Na ni kazi ya chama kuhakikisha madiwani wanafanya kile walichowaahidi wananchi ktk utekelezaji wake...Na hapo ndipo swala zima la makosa ya hawa madiwani linapoingia.

Sawa umesema hupendi nidhamu ya woga.. lakini nidhamu ipi inayokupa wewe mamlaka ya kufanya maamuzi kinyume cha matarajio ya wakuu zako. Kumbuka kuna malengo yamewekwa na wewe umekabidhiwa kazi ya kuhakikisha malengo hayo yanapatikana kisha unaleta jeuri ya kusema wewe unajua unachokifanya hali kinakiuka maadili ya chama?.

Nidhamu ya woga haina maana ya kuwa na kiburi ila unaongozwa na sheria in their case KANUNI..Unapokwenda kinyume cha kanuni kwa madai ya kuchaguliwa na wananchi, wakubwa zako wana kila haki na sababu ya kuondoa mamlaka hayo kwako kwani sii wewe pekee unayeweza kuwahudumia wananchi kwa kufuata kanuni ulizoapa kuzitumikia. Huwezi kupingana na kanuni na ukaita huo ndio ujasiri isipokuwa ni ujinga na kukosa heshima na hekima..
 
That is my opinion you are free to have it or not..... kuwa wewe na wenzako mlitaka kuivuruga Bavicha hiyo iko wazi na wazee wakawaengueni unataka evidence zaidi ya hiyo. Kuhusu jina........jina hali discuss issue watu wanashusha nondo na majina hayahaya hivi Mzee Mwanakijiji ni jina lake halisi i think this is not a big issue. Wewe tuambie uko upande gani wa Kamati kuu au wa Malah period mengine ni spices tu.

Kuhusu upande,niko kwenye upande wa haki na nidhamu tu.

Anyways, Please be comfortable.....usiwe emotional kiasi hicho.
 
Ben na Nyakarungu najua harakati zenu toka muanzishe alliance ya kutaka kugawana vyeo Bavicha mnaonekana mnapenda sana ligi ndani ya chama chenu kwa faida ya nani sijui. Panapotokea controversial ndani ya chama huwa mnachagiza ili mnyukano ukolee zaidi, sina tatizo na ben yeye anajulikana na wengi ila nilikuwa simjui Nyakarungu hadi pale alipojitokeza kuvunja kanuni za udaktari akaweka public matokeo ya postmortem ya mauaji ya Tarime siku mbili kabla ya uchaguzi wa Bavicha nikadhani ni real kumbe zilikuwa kampeni.

Ila pamoja na harakati zenu hili la madiwani ni cha mtoto sana kwa Chadema litakwisha na madiwani watatemwa muda si mrefu if not today tomorrow na hawatakuwa na pa kukimbilia zaidi ya kuomba msamaha au kwenda wanakoona watapata msaada. Msicheze na uwezo wa kamati kuu iko pale kwa mujibu wa sheria na maamuzi yake yanaweza kutumika kama evidence na mahakama ikayakubali siyo matamshi ya magazetini na kwenye TV mwisho wa kujinukuu.



MKUU!!
Hapo juu kwenye red kumbe sio mwanachadema sasa kwa nini unatoa kauli ambazo watu watalazimika kusibiri kwa hamu hapo kwenye blue?
Narudia tena mkuu naomba uache kutoa matamko yatakayoshusha hadhi heshima ya chama, umetamka kuwa leo au kesho watakuwa wamfukuzwa je isipotokea? hata hivyo wapi mimi nimewatetea kuwa wamefanya vizuri kuungana na ccm? nachopinga mimi ni aina ya hukumu na vitisho kama nilivyoainisha pale mwanzo eneo nililoandika....''naona vita'' rudi usome hiyo coment yangu.
Sory pengine wewe ni mtu muhimu sana ndani ya chadema kwenye hatua muhimu za maamuzi ndio maana unaweka wazi bla shaka, kuwa leo au kesho watafukuzwa!!!
Kama sio, basi legeza ulimi mkuu na usitoe maneno yatakayowafanya watu wawe na hamu ya kuyasubiri, na mbaya zaidi unayatoa na deadline, eti ''kama sio leo ni kesho watakefukuzwa''
 
Wewe ndiye ulitegemewa kuwa M/kiti wa Bavicha.
Sielewi utatuzi gani ungefuata zaidi ya ule wa kamati kuu ya chama kuwataka madiwani wajiuzulu
Kama unasema kuna watu wamekufa wakati huo huo unatetea upuuzi wa mwafaka wa kugawana vyeo una maana gani kama si unafiki ni nini.
Kwa hiyo unataka Malah aendelee kuwa N/meya wakati kuna damu inamlilia.......wakati huo huo unataka Chadema wakubali nonsense hii wataficha wapi uso wao mbele ya wananchi hasa waliopata majeraha wataki wa maandamano, nina wasiwasi kama kweli wewe ni Chadema.


FEEDBACK,

Mbona unapandisha mori sana ndugu, please calm down, let's discuss the matter in a very constructive decree, but we should not seek to satisfy our thirst for freedom by drinking from the cup of bitterness and hatred, its over.
AM among the sprawl, with no peculiar side!!!
 
Vita vikali vimepamba moto magwanda ya mgambo yanawaka mto! Mimi binafsi nimeamua kukaa pembeni kwanza
 
Umaarufu wa CHadema ndio ume mpa Udiwani huyo anaye jiita Naibu Meya. Nachojiuliza hv anajua kwamba huo muafaka umejaa damu? Je, damu za waliopetea zitalipwa na nani?

Better to die fighting for freedom.... Sasa ndio maana kaambiwa kapokea rushwa....Angekuwa mstaarabu angeachia madaraka taratibu zingine zifuatwe tu.

Ubishi na ujeuri wake haujengi ila unaboamoa naona kesha jisahahu kabisa kama chama cha CDM ndio kimemfikisha hapo alipo anapaswa kukiheshimu na kauli za vingozi wake pia.

Inabidi huyo Naibu Meya apime uzito kwa hicho anachong'ang'ania.
 
daktari slaa tumia busara za kufundishwa kwenye ukatoliki. ukimsikiliza lema utaua chama chako. lema angetaka ziwe zinapigwa kila siku ili apate kisingizio. diwani anayepokea amri toka makao makuu ni kibaraka sisi wananchi hatumtaki.

Ni watu wa aina fulani tu watasikiliza ushauri toka kwako. Ni ccm pekee yenye mikakati kama yako ya uchonganishi. Ni watanzania pekee yetu tunaoongozwa na wapuuzi wasiojali nchi yao.

Dr. Slaa peke yake ameweza kuwakosesha usingizi. Kwa sasa inaelekea Lema amewakwama kooni.

JENIFA AU ZUMBU KUKU
 
Naibu Meya Estonih Mallah, mpenda amani!
Bora kufa umesima kuliko kuhishi umepiga magoti, ata ukipoteza kila kitu kwenye CDM hiyo ndio sifa ya mpambanaji


hii ni buriani chadema,mwaka 2013 haifiki ikiwa ilivyokuwa,ni story inaanza kuandikwa kuwa iliwahi kuvuma kama NCCR!
 
musione aibu kuutangazia umma kuwa mmeshindwa kuwafanya lolote "vigogo" hao. tena wamewatoa nishai kwa kuwaeleza wazi kuwa hamuna ubavu huo, sasa ni hivi,mukijaribu kuwafukuza mtakuwa mnatwanga maji kwenye kinu.tume haina muda wa kuendekeza majungu yenu na visasi vyenu vya kugombea wanawake. hakutakuwa na uchaguzi wowote na itaendelea kuwatambua kama madiwani na ubunge kama kawa, na huenda ikatoa "special viti maalum" kwao.kama unabisha rudi nyuma na ukumbuke ishu ya marando akiwa NCCR ni jinsi gani aliweza kuwa mbunge wa afrika mashariki.
 
hii ni buriani chadema,mwaka 2013 haifiki ikiwa ilivyokuwa,ni story inaanza kuandikwa kuwa iliwahi kuvuma kama nccr!

hayo ni maoni au matarajio yako, but watazame watoto yatima na wananchi wenye shida, wazee wasiokidhi gharama za matibabu.
Je unapoombea chama pinzani kife, huna mahota kwa wanyonge hawa? Nani ataikumbusha serikali inapojisahau, nasema haya nikiwa nimekwepa kukushawishi uamini kuwa cdm itachua nchi, ili uwe huru kutoa majibu juu ya hayo maswali rahisi mkuu!
 
hahahaahaaaaaa, hii ni aibu kwa slaa na mbowe alizania ni kama alivyomsurubu chacha wangwe hahahahaaaaaa magwanda kimya!
 
Magwanda wanatia huruma kwa haya, hawana la kufanya wanangoja maamuzi ya mtu mmoja tu, maana Slaa kashindwa.

Hapa pazuri kweli, akiwafukuza ina maana kakosa kiti cha Ubunge kimoja na madiwani watatu. Akiwaacha, Slaa ataonekana hafai kitu na nna uhakika hiyo ndio karata ya Mbowe kummaliza makali Slaa kwani anahisi kazidiwa umaarufu na hilo kwake mwiko.
 
Magwanda wanatia huruma kwa haya, hawana la kufanya wanangoja maamuzi ya mtu mmoja tu, maana Slaa kashindwa. Hapa pazuri kweli, akiwafukuza ina maana kakosa kiti cha Ubunge kimoja na madiwani watatu. Akiwaacha, Slaa ataonekana hafai kitu na nna uhakika hiyo ndio karata ya Mbowe kummaliza makali Slaa kwani anahisi kazidiwa umaarufu na hilo kwake mwiko.
faizafoxy kumbe bado upo, vp yahe mzma? naona bado unakomaa na cdm
 
Back
Top Bottom