Sheria ya Vyuo Vikuu inakataza Wanafunzi kujihusisha na Siasa ndani Chuo

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,119
Je, wajua Sheria ya Vyuo Vikuu ya mwaka 2005 na Kanuni za Mwaka 2013 zimepiga marufuku Wanafunzi kujihusisha na shughuli za Chama cha Siasa ndani ya Majengo ya Chuo?

Kifungu cha 57 cha Kanuni ya Vyuo Vikuu inasema "Mwanafunzi yeyote au Mfanyakazi wa Chuo Kikuu anayejihusisha katika
shughuli za Chama cha Siasa ndani ya Majengo ya Chuo Kikuu ATASHUGHULIKIWA kama ifuatavyo:-"

a. Atapewa Onyo la Kinidhamu kwa kukiuka Kifundu cha 51 cha Sheria ya Vyuo Vikuu ya mwaka 2005

b. Atasimamishwa Chuo Kikuu, akisubiri kukamilika kwa Uchunguzi wa Kinidhamu (ambao utakamilika ndani ya mwezi mmoja usimamishwaji ulipotolewa kwa Mwanafunzi au Mfanyikazi)

c. Mara baada ya Uchunguzi kukamilika, Mwanafunzi au Mfanyakazi atatokea mbele ya Kamati ya Nidhamu kujibu shitaka hilo

d. Akipatikana na hatia, kwa upande wa Mwanafunzi, atasimamishwa masomo kwa muda usiozidi MIAKA MIWILI na kwa Mfanyakazi atashughulikiwa kwa mujibu wa masharti ya Kanuni za Maadili na Nidhamu ya Wafanyakazi
 
Mbona haina meno hiyo sheria...

Wanasiasa wengi bongo haswa wa upinzani wamanzia harakati zao vyuoni...
 
Screenshot_20231029-185111.png
 
Wabongo tuache kuchanganya Ukiwa ndani ya jengo la chuo ndio huruhusiwi Kuleta alama yoyote ile ya siasa ila ukiwa nje ya chuo Hakuna anaekuzuia.. shida mnakaza mno ubongo kwenye vitu vidogo tu.
 
wabongo tuache kuchanganya Ukiwa ndani ya jengo la chuo ndio huruhusiwi Kuleta alama yoyote ile ya siasa ila ukiwa nje ya chuo Hakuna anaekuzuia.. shida mnakaza mno ubongo kwenye vitu vidogo tu.

Umenena vyema kabisa na lengo la sheria hii ilikua nikuua nguvu ya vyama vya upinzani iliyoshika kasi kwa vijana wa vyuoni.

Kumbuka siasa za vyuoni na mashuleni zilinzishwa kipindi cha tanu na ilikua ni lazima mwana chuo kuwa na kadi ya tanu.
 
Mbona machawa wa ccm wanafanya siasa ya chama chao vyuoni siku zote kama kawaida?
Au hilo katazo ni kwa wapinzani tu?!
1698596273504.png


1698595774765.png
 
Je, wajua Sheria ya Vyuo Vikuu ya mwaka 2005 na Kanuni za Mwaka 2013 zimepiga marufuku Wanafunzi kujihusisha na shughuli za Chama cha Siasa ndani ya Majengo ya Chuo?

Kifungu cha 57 cha Kanuni ya Vyuo Vikuu inasema "Mwanafunzi yeyote au Mfanyakazi wa Chuo Kikuu anayejihusisha katika
shughuli za Chama cha Siasa ndani ya Majengo ya Chuo Kikuu ATASHUGHULIKIWA kama ifuatavyo:-"

a. Atapewa Onyo la Kinidhamu kwa kukiuka Kifundu cha 51 cha Sheria ya Vyuo Vikuu ya mwaka 2005

b. Atasimamishwa Chuo Kikuu, akisubiri kukamilika kwa Uchunguzi wa Kinidhamu (ambao utakamilika ndani ya mwezi mmoja usimamishwaji ulipotolewa kwa Mwanafunzi au Mfanyikazi)

c. Mara baada ya Uchunguzi kukamilika, Mwanafunzi au Mfanyakazi atatokea mbele ya Kamati ya Nidhamu kujibu shitaka hilo

d. Akipatikana na hatia, kwa upande wa Mwanafunzi, atasimamishwa masomo kwa muda usiozidi MIAKA MIWILI na kwa Mfanyakazi atashughulikiwa kwa mujibu wa masharti ya Kanuni za Maadili na Nidhamu ya Wafanyakazi
Mbona NIT Kila siku naona shughuri tu
 
Kuna majengo na maeneo. Sheria inasema kwenye majengo ya chuo means ukiwa ndani ya vyumba vya mihadhara au ofisi ni marufuku kuonesha itikadi zako.
 
Back
Top Bottom