Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 877
- 4,105
JPM alipoona Mwendokasi Madereva wanadai maslahi alikwenda kuchukua vijana serikalini na JKT akawapa kazi za ulinzi, kukata tiketi,ufundi na udereva. Walioletwa kwa sababu wanawekwa bila sifa wameendelea kujifunza kazi taratibu lakini wakiwa na msongo mkubwa wa mawazo kuhusu lini watapata nafasi ya kulalamika na kutema nyongo?
Hali hiyo ya msongo wa mawazo imekuwa kubwa kiasi kwamba wakaazi wa DAR wanadai hawa jamaa wanaweza kusimamisha gari kituo likiwa limejaa na wakapakia abiria hata kupitia milango isiyotakiwa bila kujali usalama wao.
Leo nimeona pia Dreva mmoja mwenye msongo wa mawazo clip inasambaa ikionyesha alivyovuka vituo bila kusimama huku akiendesha kama vile kabeba magunia.
Kampuni hii ina garage lakini sidhani kama tumewahi kuona tangazo la kutaka kuajiri mafundi.....jiulize mafundi wa kampuni wanapatikanaje? Lakini pia jiulize garage ya kampuni kubwa kama hii ipo wapi? Jiulize kwanini magari yaliyopaki ni mengi kuliko yanayotembea? Usalama wa abiria upo wapi kama hali ipo hivi? Tunasubiri hawa madereva waue abiria ndipo tujirekebishe?
Mhe. Mchengelwa kabla yakusubiri kuletewa mwekezaji na magari mapya pls zungumza na hawa wachache waliopo wakushauri ili unapokwenda kukabidhi Mradi kwa wawekezaji binafsi ujue mikataba iwe na terms gani.
Lakini pia kaa na hawa ndugu uwaulize kama bado wangetamani kufanya kazi na Mradi huu au wapo tayari kurudi kwenye ofisi zao za awali uajiri watu wenye shida na kazi? Haiwezekani watu wanatafuta kazi then Dreva anatishia abiria kwamba wafanye wafanyavyo hiyo siyo ajira yake.
Nakusalimuni
Pia soma
- Dereva wa Basi la Mwendokasi adaiwa kuwapitiliza Vituo Abiria baada ya kukasirishwa
Hali hiyo ya msongo wa mawazo imekuwa kubwa kiasi kwamba wakaazi wa DAR wanadai hawa jamaa wanaweza kusimamisha gari kituo likiwa limejaa na wakapakia abiria hata kupitia milango isiyotakiwa bila kujali usalama wao.
Leo nimeona pia Dreva mmoja mwenye msongo wa mawazo clip inasambaa ikionyesha alivyovuka vituo bila kusimama huku akiendesha kama vile kabeba magunia.
Kampuni hii ina garage lakini sidhani kama tumewahi kuona tangazo la kutaka kuajiri mafundi.....jiulize mafundi wa kampuni wanapatikanaje? Lakini pia jiulize garage ya kampuni kubwa kama hii ipo wapi? Jiulize kwanini magari yaliyopaki ni mengi kuliko yanayotembea? Usalama wa abiria upo wapi kama hali ipo hivi? Tunasubiri hawa madereva waue abiria ndipo tujirekebishe?
Mhe. Mchengelwa kabla yakusubiri kuletewa mwekezaji na magari mapya pls zungumza na hawa wachache waliopo wakushauri ili unapokwenda kukabidhi Mradi kwa wawekezaji binafsi ujue mikataba iwe na terms gani.
Lakini pia kaa na hawa ndugu uwaulize kama bado wangetamani kufanya kazi na Mradi huu au wapo tayari kurudi kwenye ofisi zao za awali uajiri watu wenye shida na kazi? Haiwezekani watu wanatafuta kazi then Dreva anatishia abiria kwamba wafanye wafanyavyo hiyo siyo ajira yake.
Nakusalimuni
Pia soma
- Dereva wa Basi la Mwendokasi adaiwa kuwapitiliza Vituo Abiria baada ya kukasirishwa