Madereva wa mikoani, tabia na utaratibu wa kupaki mabasi sehemu ya chakula chenye bei juu mnaumiza abiria wenye kipato kidogo

Dah niliudhika sana Ally's kutoka Dar-kwenda Mwanza...badala ya kupaki dodoma mjini kwenye hotel/migahawa mizuri .wameenda kulipaki basi karibu na bahi...vyakula vimepoa na vibaya kinoma.

Ok kutoka hapo ineenda kusimama tena nje ya mji wa Singida..chakula kibaya na bei kubwa vile vile..
 
Ukifanya uchunguzi utagundua pia kwamba Madereva wenyewe hawali kwenye hotel hizo huwa wanalipwa hela tu , wao wanakula sehemu maalum , wana wapishi maalum humo njiani huwaletea msosi kwenye maeneo wanayoahidiana
Hii itakua kweli mkuu, Maana akisha simamisha basi tu, humuoni tena, zaidi ya konda. Mara ya kwanza nilikua nahisi labda kuna vyumba special wanakaa.
 
Hii serikali haijali wananchi hata kidogo, ni wizi kama wizi mwingine kuuza sahani ya chakula, wali boko boko 8000
Ulitaka serikali ipange bei ya chakula?Halafu mpige kelele tena kwamba ni ya kidikteta?Supply and demand ndio inaamua bei ya bidhaa.Uchumi wa kupangiana bei sio mzuri.Bei ni mapatano ya muuzaji na muuziwa.Ukiona haikufai acha.Muuzaji atateremsha bei kwa sababu ya demand ndogo.
 
Serikali yetu - mamlaka husika tunaomba mtusaidie sisi wanyonge na hii tabia ya madereva inayozidi kushamiri kila kukicha, hasa kwa wale ndugu zetu wanaosafiri mikoa ya mbali wanapata tabu sana kuhusu masuala ya chakula.

• Dar - - mwanza
• Dar - - mbeya
• Dar - - kigoma
• Dar -- Arusha
• Dar -- Ruvuma

Kuna tabia na utaratibu wa mabasi walio jiwekea bila kuhofia abiria wao, sio rafiki kabisa, wanapaki mabasi yao sehemu ya chakula bei zao ziko juu sana bila kujali abiria mifukoni mwao/kipato walicho nacho. Karibia vituo vyote wanavyo paki hawa madereva unakuta Chakula cha bei ya chini ni kuazia elfu Tsh7000/- hadi elfu Tsh8000/- na kuendelea, na ukiangalia hicho chakula hakina hadhi ya kuuzwa bei kwa hiyo, alafu chakula kinakuwa ni kidogo ikiwa mtakua watu wawili hamuwezi kushiba.

Jana nilikuwa natoka Dar kuja Mbeya tulipofika sehemu ya chakula, niliongozana na mama mmoja mwenye watoto wa 3 alivyo ambiwa chakula bei ya mwisho ni elfu Tsh7000 alikuwa mnyonge sana, na kiasi alichokuwa nacho taslimu alikuwa na elfu Tsh5000 tu, ikambidi anunue soda na biscuit, roho iliniuma sana.

1. Madereva mnadhani kila mtu anapesa ya kununulia hicho chakula cha bei ya juu?

2. Au sehemu mnazopaki kwa ajili ya watu kula ni za viongozi wa ngazi za juu huko serikalin?


Ombi langu kwa Serikali tunaomba mtoe tamko/sheria kwa mabasi yote, yawe yanasimama kwenye mji ulio na huduma kamilifu ili abiria wote wapate huduma stahiki
Hya malalamiko huwa yanaletwa hapa mara kwa mara. Tatizo watanzania ni manyumbu yanapenda kulalamika bila kuchukuwa hatua. Tungekuwa tunakomaa wakati wa uchaguzi kulinda kura hawa watawala wasingetuchezea namna hii.
 
Sawa kabisa siku tulipita chalinze pale kulia tukaona tukale kidogo maana tulitoka mtwara.
Aisee naagiza kuku kienyeji chips likaletwa bonge la paja.
Mmh kula kidogo likanishinda ladha.
Nikaja kuambiwa badae ni yale mandege Tai yana miguu mirefu hivi ndo nimeuziwa.
Hizi ni story za vijiweni. Hivi wewe unadhani kuna mtu mwenye uwezo wa kukamata ndege wengi mpaka afikie hatua ya kuuza nyama yao? Au humjui tai wewe? Wanapatikana kwa wingi kiasi hicho?
 
Dah niliudhika sana Ally's kutoka Dar-kwenda Mwanza...badala ya kupaki dodoma mjini kwenye hotel/migahawa mizuri .wameenda kulipaki basi karibu na bahi...vyakula vimepoa na vibaya kinoma.

Ok kutoka hapo ineenda kusimama tena nje ya mji wa Singida..chakula kibaya na bei kubwa vile vile..
Hao ni majambazi,Dom mngekula poa tu,Manyoni hamkosi msosi uhakika pale,Singida town popote mikuku ,nyama iko bwerere.
 
Beba chakula chako kutoka kwenu,
Mabasi hayawezi kupeleka watu kwa mama ntile kusiko hata na vyoo vya kujisaidia abiria.
Mbona zamani mabasi yalikuwa yanasimama stendi na stendi kulikuwa na hotel nzuri na zenye vyakula vizuri? Kwanza kulikuwa hakuna mama ntilie wa kuuzia wasafiri vyakula. Serikali leo ikiamuru magari kusimama stendi, nakuhakikishia watu wataweka hoteli nzuri sana.
 
Back
Top Bottom