Madaktari wenzangu: Only "Mass resignation" itawaamsha watawala!

Madaktari wenzangu: Only "Mass resignation" itawaamsha watawala!

Madaktari kugomea kutibu wagonjwa ni sawa na uuaji. Hawa ni wauaji tu. Nawaomba wajifunze kuhusu ulimboka: Je kama Ulimboka asingetibiwa angepona? Na wagonjwa ni hivyo wajue kuwa wameua watu wengi sana. Wameua sana

Kenge,mbuz,bata mzinga,kuku we, Dagaa wabichi,kibua,nyani,ngedere,kuku la kizungu we unafugwa mawazo mpaka akili,s******e we.
 
We vipi? Tuje tukupe kichapo heavy halafu upelekwe hospitali ukute kuna mgomo usitibiwe we utajisikiaje? Au umeugua serious ukakimbizwa hospital ukakuta mgomo we hali hiyo unaichukuliaje? Unajua kushabikia mgomo kunasababishwa na kuwa na afya njema? Ungekuwa mgonjwa umelazwa halafu hupati huduma yoyote! Jamani,madai yao ya vifaa ni sahihi lakini mgomo hapana! Kwani tusio na uwezo wa kwenda private ndio tunaoumia! Hili sio suala la kushabikia hata kidogo.

Bornivila unaweza kufikiri suluhu ya muda mfupi au ya muda mrefu. strategic thinking huwaza juu ya mafanikio katika muda mrefu, Unaweza kukosa viatu na wali leo ukawekeza kwa ajili ya faida utakayopata miaka kumi baadaye. uzuri hapo kuna kitu kinaitwa time value na risk unazochukua. Vyote hulipwa katika miaka 10 hiyp. Leo unasema juu ya maumivu ya kichapo cha mtu mmoja leo, lakini siku ukienda hospitali ya Tz ukapata huduma kama zile za Apollo India utawashukuru sana madaktari kuwa waliitetea huduma ya afya ya mtanzania kwa gharama kubwa!!!
 
Aliyesema Madaktari ni wabinafsi alikuwa sahihi. Kama wangetaka dhamira yao ya kudai kuboreshwa kwa huduma za afya kwa kuboresha mazingira ya utoaji huduma, wangewashirikisha watumishi wote wa sekta ya afya, mapambano ya madai yao kwa serikali yangepata mashiko sana. Bila shaka serikali ingesalimu amri. Kwa hili jamaa wa serikali tuliyonayo ni lazima watawachezea sana
 
Umeichoka amani wewe unataka machafuko amia basi kwenye hizop nchi ulizozitaja.

amani inahusikaje hapa?!machafuko yamekujaje hapa? huu ndio wimbo tuliokaririshwa Amani, amani..amani..halafu unakufa kwa magonjwa yanayoweza kutibika kabisa ila unashindwa kusimamia eti unalinda amani!!! aliyekukaririsha huo wimbo hajui hizo shida!!
na suala la kwenda nje..ni kutokana na kukatishwa tamaa tu, wapo wengi tu wapo hospitali binafsi..yaani ratio ya daktari mmoja kwa zaidi ya wananchi 35,000 na serikali yako inazidi kuzidisha upungufu kwa kufukuza wengine na wewe unasema hiyo ni amani?! kweli upeo wetu ni mkubwa kweli!!
 
Matatizo ya madakatri ni

1. wanafikiri wana akili nyingi kuliko watu wengine. Hawajui kuwa kufaulu mtihani siyo kipimo pekee cha akili

2. wanatumia mbinu za kishule kutatua migogoro ya kikazi. Hawatambui kuwa migogoro ya shule na kazini ni vitu viwili tofauti.

3. Viongozi wao wamejipa hati miliki ya kufanya maamuzi yote.

Nina uhakika madaktari wengi tu hawaungi mkono maamuzi, ila wakijaribu kusema wanafungwa mdomo kwa kutumia intimidations za namna mbalimbali.

hayo ni yako maoni na wako mtazamo tu mkuu!
 
Doctors kazeni kamba ukombozi hauji kwa manyaso bali kwa haki ninaimani mtafanikiwa yaani taaluma yenu inalipa na si Tanzania tu hata nje ya nchi msibweteke na serikali kichaa ambayo haina utu kwa wananchi wake bali matumbo yao
 
amani inahusikaje hapa?!machafuko yamekujaje hapa? huu ndio wimbo tuliokaririshwa Amani, amani..amani..halafu unakufa kwa magonjwa yanayoweza kutibika kabisa ila unashindwa kusimamia eti unalinda amani!!! aliyekukaririsha huo wimbo hajui hizo shida!!
na suala la kwenda nje..ni kutokana na kukatishwa tamaa tu, wapo wengi tu wapo hospitali binafsi..yaani ratio ya daktari mmoja kwa zaidi ya wananchi 35,000 na serikali yako inazidi kuzidisha upungufu kwa kufukuza wengine na wewe unasema hiyo ni amani?! kweli upeo wetu ni mkubwa kweli!!

Basi waendelee kugoma na wewe unayetaka ndugu zetu wafe mahospitali uwaunge mkono sasa watu wakifa hivyo vifaa unavyosema vitatumiwa na nani??? au wewe upo nahututi ukapelekwa hospital ukakuta kuna mgomo wa madaktari? utafurahi ndiyo yanayowakuta ndugu zetu.
 
Madaktari wa Tanzania wanagoma wanawaacha wagonjwa wakikata roho ili walipe maslahi yao...kama kazi ya udakatari aina maslahi badili kazi ingia kwenye siasa.
 
MADAKTARI MMEFANYA MAMUZI MAGUM, NDIO INITIAL STAGE ZA UKOMBOZ!TATZO WATZ NI TOFAUTI NA WALIBYA,WAMISRI,WA2NISIA etc CC WAOGA TENA SANA,2NAPENDA HAKI ILA HA2PO TAYARI KUIPGANIA!TAIFA LITAKOMBOLEWA NA WELEVU(MAJASIRI),WAJINGA(WAOGA) WATASHUHUDIA MAFANKIO
 
Madaktari wa Tanzania wanagoma wanawaacha wagonjwa wakikata roho ili walipe maslahi yao...kama kazi ya udakatari aina maslahi badili kazi ingia kwenye siasa.

Waache mara ngapi??? wameshaacha na wengine mmeshawaachisha. Ngoja mle joto ya jiwe.
Hata wao wana haki ya kukaa kupiga soga kwenye net kama nyie na watalipwa vizuri kama nyie kuliko kushinda wanafanya kazi hatarishi kwenye mazingira magumu kwa kipato kidogo.
Mama, baba, mjomba, shangazi na watoto wako ndio watapata taabu. Subiri kidogo tu. Kwani wote utawapeleka india???
 
Yataka ujasiri! Sina hakika kama wote mko pamoja kiasi hicho " hatuko huru ila tuna nidham ya uwoga.


The talk is cheap....Dr Catherine Mung'ong'o keshaonyesha njia, who is next??.............NOBODY!
 
Asante mtaalam kwa uchambuzi makini, inatia moyo tunao wataalam!

Tulikofikia hakuna mshindi, si serikali si wataalam wetu madaktari, si wananchi, si yeyote mpenda maendeleo na amani. Tulipofikia pia tutakosa rafiki wa kutusaidia iwe mawazo au hali.

ili kuwa katika hali salama, tunapaswa kuangalia mbele sana: Suala hili lisiwe la madaktari peke yao. Hili ni suala la taifa zima, linagusa maisha ya kila mtu anaeishi Tz, mwenyeji kwa mgeni. Nina maoni makuu mawili: 1. Wanasheria watupe upembuzi yakinifu juu ya haki ya afya na jinsi inavyopaswa kutolewa kufuatia TZ kuwa mwanachama wa WHO na wanachama wa mikataba mingine inayohusu haki ya afya na nyanja zake zote. Ndani ya baadhi ya hii mikataba kama ule wa haki za kitamaduni na uchumi (the Internationla covenant on economic and socila rights - 1966) ambamo haki ya kufanya kazi inaweza kuhusishwa na haki ya afya inatajwa; kifungu cha 7 cha mkataba huu kinahusu haki ya kufanya kazi na mazingira bora kazini; kifungu hiki kinazungumzia serikali zote wanachama ( TZ ilikuwa miongoni mwa wanachama wa kwanza kabisa kuridhia na kusaini mkataba huu wakati huo - 1966 - Mwl JKN akikabiliana na suala la kukopa kwa ajili ya huduma za jamii - elimu, afya nk.)

kifungu kinafafanua mazingira bora kuwa ni pamoja na mafao stahiki kwa kila aina ya kazi...hapa tujiulize kama mshahara wa dr ni stahiki yake ikilinganishwa na taaluma na sekta zigine ambazo hazizalishi lakini ni muhimu sana?? ...(7) (ii) kiwango cha maisha kinachoridhisha kwake na familia yake...decent living for them and their families....(b) safe and healthy working conditions...kifungu cha 8 kikitambua haki za wafanyakazi kuwa na vyama vyao kutetea na kusimimia masilahi yao...hiki kimeainishwa kwa upana sana...kifungu cha 12 kinawahusu madaktari zaidi kuwa serikali zote wanachama kutambua haki ya kila mtu kufurahia kiwango cha juu cha afya ya mwili na ubongo ( ...the right of everyone to the enjoyment of the highest attainable standard of physical and mental health...) 12(2) state should take steps to achieve "full realization" of this right...and this to inlcude the follwing:

reduction of stillbirth- rate....; (d) creation of conditions which would assure to all medical service and medical attention in the event of sickness....yaani haturuhusiwi kukubali hali ya mgonjwa kukosa huduma kama mwanachama wa mkataba huu....nk

TZ imeridhia mkataba huu bila reservation - bila maeneo ambayo tunadhani hatuwezi kuyakidhi.. na hata kama tungefanya hivyo...bado tungebanwa na vifungu vingine ambavyo vinaainisha wajibu wa serikali katika mfumo huu ambao ni kuhakikisha haki ya mgonjwa na ya dakatari, nurse na wengine inalindwa...

katika mfumo huu serikali inafanya kazi na madktari kupitia chama chao kujua njia sahihi za uendeshaji na usimamizi wa utaratibu huu; wanasheria wakisaidia kuweka mambo katika mtazamo wa haki na usalama wa pande zote: HAKUNA MSHINDI AU ANAYESHINDWA....

KATIKA hili tunakubaliana ( huu ni mchakato mkubwa wa kitaifa ukihusisha bunge nk)...kiasi cha pato la taifa na jinsi tunavyoligawa kwa nyanja mbali mbali...tukilindwa na sheria ya usawa usio bagua mtu au kundi hata katika mgawanyo wa mapato kwa njia ya mishahara....usawa na kutobaguliwa ( the principle of non discrimiantion and equality of all types) ni moja ya misingi mikuu ya umoja wa mataifa na wanachama wake wote - TZ ni mojawapo na mpaka tumetoa naibu Katibu Mkuu wa umoja huu - tuko mbele sana katika masuala haya...

katika mtazamo huu athari kwa raia wasioweza kulipia matibabu aghali inalindwa ...nia ikiwa kuhakikisha watu wote wanapata matibabu stahiki kwa kila ugonjwa - ikibidi mtu kutibiwa nje iwe ni kwa matakwa yake na uwezo wake - wengi wa hawa huwa wafanyabiashara wakubwa -

kwa hiyo kama kuna kesi mahakama yoyote itaangalia mambo haya na usawia wake na haki itaonekana kutendeka maana mahakama itasaidia pande zote: serikali kusimamia wajibu wake na madaktari kusimamia haki zilizo za msingi kwao. Wananchi tutafaidika na muafaka wa hawa wawili...mahakama na bunge vikiwa katikati....kuhakikisha uwiano sahihi wa masuala yote...

Maoni ya 2: yote ya juu yanawezekana tukikubali kusikilizana, kuzungumzana kama ambavyo mchakato ulikuwa umeanza...kwa hiyo ninawaomba madaktari wafanye kazi na wanasheria kuliweka hili katika mtazamo huu na kuhakikisha uratibu makini wakati wa majadiliano. pili katika hili ni kwa serikali kukubali kw mara nyingine kuzungumza na madaktari, pengine na wadau wengine - kubwa likiwa kuweka misingi itakayosimamia mustakabali wa nchi kwa namna ambayo inajengea maeleano katika masuala ya msingi.

Kufuata mikatba ya kimataifa na ya ndani kupitia katiba na sheria zingine...kuna mapana ambayo sijayaweka hapa ambayo serikali inayajua vizuri na ninaamini yakiletwa katika meza ya majadiliano yanaweza kuinua taifa letu kuliko kulididimiza kama inavyotaka kutokea sasa.

raia wa leo wanauwezo kujua mapana na wigo za majadiliano haya: mwisho wa siku wataona ni madaktari na serikali waliowasaliti na si mmoja kati yao!! Kwa hiyo pande hizi mbili zikae pamoja na kufikia muafaka wa namna sahihi ya kufikia muafaka katika hili...la sivyo kwetu raia sauti zetu zinalalama na kusema "....tumewakosea nini (serkali na madakatari) kutughilibu kiasi hili??? Mbona mnatuumiza??

ninaamini na kuomba kuwa hekima ya Mungu ipitayo zote itaongoza na kutangulia pande hizi mbili kufikia makubaliano. Tz tumetatua migogoro mingi ulimwenguni na tunaheshimika sana na majirani na watoka mbali - sasa ni wakati wa kujiganga na migogoro yetu ya ndani. isikilizeni sauti wa wanawake na watoto, wazee, wenye ulemavu wa aina nyingi, wenye mapenzi mema na nchi yetu. Tunawategemea, Tunategemea hekima yenu kulifikisha taifa mahali stahiki. AMINA.

Maoni mazuri sana sana sana sana.
Shida inakuja tu kwamba serikali inaingilia na mahakama na kutoa maamuzi. Hapa ndipo mahakama zetu zimepoteza sifa yake. Inaelekea mahakama imekosa sifa za kuaminika tena
.
 
Siku moja nilikuwa naongea na jamaa mmoja toka Ulaya, aliniuliza hivi "Hivi kwa nini Tanzania wananchi hawawezi kuungana kupinga dhuluma mnayotendewa na serikali yenu?" kweli nilikosa jibu sahihi, ila nilichomwambia "Serikali ya Tanzania inatumia udini na vyombo vya habari kudanganya wananchi"
  • Dini inatumika pale ambapo inawezekana (Mfano CUF tuliambiwa ni cha kiislamu na walileta mavisu kuua wananchi, kumbe ni uongo, na hapo wakristu hawakukiunga mkono, na ikitokea CUF kaitisha umoja wowote basi atapata tu Islam kwa sababu christian watasema nyie wadini, na hapo umoja haupo, serikali itapeta.
  • Vyombo vya habari vinatumika kukanusha yayoiandama serikali (mfano suala la Dr Ulimboka na madakitari kwa ujumla) hapo wananchi wanadanganywa eti hawa jamaa wanadai eti tuwalipe msharaha mkubwa (tena kwa kutaja kiasi ili na wenye mshahara mdogo wawaonee donge ili wawapinge, na hapo wananchi wanaaminishwa kuwa serikali imefanya juhudi ila madakitari ndiyo tatizo.
Mkuu wangu Ndivyo Tulivyo na hakika ktk swala la CUF sidhani kama kuna mtu hapa haamini kwamba ni chama cha Kiislaam tena. Walisingiziwa wakaamini nasi tukaamini na sasa kimekuwa hivyo. Nachoogopa ni Chadema nao walisingiziwa baadhi yetu wakaamini na isije fikia nao wana Chadema wakaamini. Hivyo ndivyo Tulivyo ktk kuamini tunayoambiwa.

Lakini pamoja na yote haya ni vizuri kufahamu kwamba kila kitu kina sababu zake..Wazanzibar wamegombania saana kile wanachoamini ni haki yao lakini wamepuuzwa kwa miaka hadi imefikia watu kuunda UAMSHO chombo ambacho kinachukua maamuzi ya kuchoma makanisa kama silaha ya kuishinikiza serikali. Madaktari nao wamegoma kama njia ya kuishinikiza serikali isifuate matakwa yao..

Jamani, jamani ni muhimu sana kuelewa who we a dealing with. Ni serikali dhalimu isioyojali hata wafe wananchi wote as long as they stay in power hawatajali kitu. Kati ya sinema nazozipenda sana ni ile ya The Usual Suspect, mkanda huu upo ktk list ya sinema zenye ujumbe mkubwa sana kuhusu uwezo wa binadamu. Katika sinema hii kuna mtu anaitwa Kaizer Soze huyu jamaa aliwekwa kati na majambazi waliomsihka mwanaye na mama yake mzazi ambaye ni mkewe kama Hostage, ili afanye wanavyotaka wao. Kaizer Soze kwa kuwaonyesha hao jamaa nani mwanamme (jasiri) aliwaua mwanaye na mama yake (mkewe) yeye mwenyewe mbele yao na kisha kuwaambia sasa ni imabakia vita baina yake na wao..

Angalia hekima ya sinema hii, unaweza kuona kwa nini Kaizer Soze asikubali matwaka ya hao jamaa lakini on the other hand kwa nini wale watu wawachukue mwanaye na mkewe kama Hostages?...Hivyo, makosa hayawezi kuondolewa na makosa mengine tunajiongezea machungu. Madaktari, mna kila sababu ya ktk madai yenu na ya msingi sana tu isipokuwa maandalizi na maamuzi mlofikia haya ndio tunayoshindwa kuafikiana nayo. Wote tunajua udhaifu wa serikali hii na nadhani zipo njia znzuri zaidi za kupambana nayo..Ni sisi wote kuungana hasa Watumishi wa Umma bila kubagua na kufanya maandamano ni migomo kwa silimia isiyozidi 40..

Tunajua serikali haitatishika sana kutokana na kwamba kuna watu wengi sana hawana kazi leo na wanasubiri nafasi kama hizi kuonyesha Unafiki wao lakini pia wananchi kwa umoja wetu tunaweza kabisa kuishinikiza serikali kupunguza matumizi yake yote ya anasa toka Bungeni, mahakama na serikali maana hakuna sababu kabisa kwa serikali kutumia fungu kubwa la bajeti kwa matumizi ya kawaida ambayo hayahusu utoaji huduma kwa wananchi moja kwa moja. Tupigeni vita sote kwa pamoja matumizi mabaya ya serikali na tuiadhibu serikali maana hili sio swala la Chadema CUF au TLP..
 
Madaktari wa Tanzania wanagoma wanawaacha wagonjwa wakikata roho ili walipe maslahi yao...kama kazi ya udakatari aina maslahi badili kazi ingia kwenye siasa.

Siasa nayo ni kazi? Wacha dharau ya taaluma za udaktari. Kiilaza ndio asiyejua maana ya udaktari.
 
Kenge,mbuz,bata mzinga,kuku we, Dagaa wabichi,kibua,nyani,ngedere,kuku la kizungu we unafugwa mawazo mpaka akili,s******e we.

Matusi kwa huyo mlaniwa hayatoshi mimi nasema anayewalaumu madaktari amelaniwa kwa kuwa hajui ukweli na ukweli hawezi kuupata kwa sababu anafikiri kwa kutumia masaburi. Serikali ina wajibu kutlinda raia wake kwa vita njaa na kuhakiisha tuna afya njema sasa unapomlaumu daktari kagoma unakuwa mwendawazimu kwa sababu ni serikali inatakiwa kuhakikisha daktari hagomi lakini kwa wenye matope kichwani wote wamewaandama ma drs mimi nasema MADAKTARI MSITISHWE KAZENI BUTI MBUNGE FORM IV BILA KOZI YOYOTE MSHAHARA MLIMA DR PESA HAKUNA KWA NINI??????????!!!!!!!!
 
Mkuu wangu Ndivyo Tulivyo na hakika ktk swala la CUF sidhani kama kuna mtu hapa haamini kwamba ni chama cha Kiislaam tena. Walisingiziwa wakaamini nasi tukaamini na sasa kimekuwa hivyo. Nachoogopa ni Chadema nao walisingiziwa baadhi yetu wakaamini na isije fikia nao wana Chadema wakaamini. Hivyo ndivyo Tulivyo ktk kuamini tunayoambiwa.

Lakini pamoja na yote haya ni vizuri kufahamu kwamba kila kitu kina sababu zake..Wazanzibar wamegombania saana kile wanachoamini ni haki yao lakini wamepuuzwa kwa miaka hadi imefikia watu kuunda UAMSHO chombo ambacho kinachukua maamuzi ya kuchoma makanisa kama silaha ya kuishinikiza serikali. Madaktari nao wamegoma kama njia ya kuishinikiza serikali isifuate matakwa yao..

Jamani, jamani ni muhimu sana kuelewa who we a dealing with. Ni serikali dhalimu isioyojali hata wafe wananchi wote as long as they stay in power hawatajali kitu. Kati ya sinema nazozipenda sana ni ile ya The Usual Suspect, mkanda huu upo ktk list ya sinema zenye ujumbe mkubwa sana kuhusu uwezo wa binadamu. Katika sinema hii kuna mtu anaitwa Kaizer Soze huyu jamaa aliwekwa kati na majambazi waliomsihka mwanaye na mama yake mzazi ambaye ni mkewe kama Hostage, ili afanye wanavyotaka wao. Kaizer Soze kwa kuwaonyesha hao jamaa nani mwanamme (jasiri) aliwaua mwanaye na mama yake (mkewe) yeye mwenyewe mbele yao na kisha kuwaambia sasa ni imabakia vita baina yake na wao..

Angalia hekima ya sinema hii, unaweza kuona kwa nini Kaizer Soze asikubali matwaka ya hao jamaa lakini on the other hand kwa nini wale watu wawachukue mwanaye na mkewe kama Hostages?...Hivyo, makosa hayawezi kuondolewa na makosa mengine tunajiongezea machungu. Madaktari, mna kila sababu ya ktk madai yenu na ya msingi sana tu isipokuwa maandalizi na maamuzi mlofikia haya ndio tunayoshindwa kuafikiana nayo. Wote tunajua udhaifu wa serikali hii na nadhani zipo njia znzuri zaidi za kupambana nayo..Ni sisi wote kuungana hasa Watumishi wa Umma bila kubagua na kufanya maandamano ni migomo kwa silimia isiyozidi 40..

Tunajua serikali haitatishika sana kutokana na kwamba kuna watu wengi sana hawana kazi leo na wanasubiri nafasi kama hizi kuonyesha Unafiki wao lakini pia wananchi kwa umoja wetu tunaweza kabisa kuishinikiza serikali kupunguza matumizi yake yote ya anasa toka Bungeni, mahakama na serikali maana hakuna sababu kabisa kwa serikali kutumia fungu kubwa la bajeti kwa matumizi ya kawaida ambayo hayahusu utoaji huduma kwa wananchi moja kwa moja. Tupigeni vita sote kwa pamoja matumizi mabaya ya serikali na tuiadhibu serikali maana hili sio swala la Chadema CUF au TLP..

Mkuu mawazo ni mazuri sana lakini hilo haliwezekanio tz hakuna ushirikiano wa wafanyakazi na ndani ya wafanyakazi hao kuna system at work kwa hiyo mobilization ni ngumu sana bora hivyo walivyofanya ujumbe umefika japo kwa ghrama ya watz wenzao ilikuwa hakuna namna nyingine ya kufikisha ujumbe ispokuwa mgomo
 
Back
Top Bottom