Madaktari wenzangu: Only "Mass resignation" itawaamsha watawala!

Madaktari wenzangu: Only "Mass resignation" itawaamsha watawala!

Doctors let's meet tomorrow at the announced venue for afore mentioned agenda, and let everyone pass by the ATM before attending, for our usual contributions.
 
Wewe mr. Mhasibu yaani jana nilisaini hela yangu ya nauli sh. 10,000/= kumbe nilipotoka ukaongeza 4 mbele ikasomeka 410,000 hiyo 'cha juu' unaenda kununua karatasi kweli?
duh, was this suppose to be a joke, maana sioni kaa inahusu au inachekesha.
kaz kwelikweli..
 
1. Kwa vile WTZ wachache wamekubali kukanyagwa kichwani na MAFISADI - ndio unataka na madaktari wawe hivyo?
hata ningetaka, nisingeweza.
2. Wewe unalipwa shilingi ngapi ambazo unaweza hadi kununua karatasi za ofisi yako??? Au ndio nyie W..I wa nchi hii?
Of koz as a scientist siezi kushindwa kununua karatasi za 10K ili ku-print kazi zangu, i won't stoop that low.
3. Wananchi/Wagonjwa wa Tanzania sio mali ya madaktari - ni mali ya Serikali so Serikali ifanye wajibu wake.
which is all well, lakini sheria ni msumeno. masikio daima hayazidi kichwa, nchi hii ni maskini, it is NOT USA kwamba individualism is a way of life. Mtarudi tu kuipigiamagoti sirikali..mtakuja!
 
We vipi? Tuje tukupe kichapo heavy halafu upelekwe hospitali ukute kuna mgomo usitibiwe we utajisikiaje? Au umeugua serious ukakimbizwa hospital ukakuta mgomo we hali hiyo unaichukuliaje? Unajua kushabikia mgomo kunasababishwa na kuwa na afya njema? Ungekuwa mgonjwa umelazwa halafu hupati huduma yoyote! Jamani,madai yao ya vifaa ni sahihi lakini mgomo hapana! Kwani tusio na uwezo wa kwenda private ndio tunaoumia! Hili sio suala la kushabikia hata kidogo.

Nimeangalia itv taarifa leo na kuona wagonjwa wanabebwa na ndugu zao kwenda private kufanya vipimo kisha kurudi mhimbili na ujue kwa mfano kipimo cha CT scan pale hospitali ya regency ni 282000 wakati ilipokuwepo mhimbili gharama ilishuka hadi 50000......Kwa hiyo wewe furaha yako ni kumzungusha mgonjwa kupata vipimo private wakati vingeweza kupatikana hospitali za serikali? nina mashaka na uwezo wako wa kufikiri!!!
Kwa taarifa yako, watu wapuuzi kama wewe mmechangia kuondoa mgomo kwenye vyombo vya habari (ambao ndo unaisumbua serikali) mmehamishia mgomo mahospitalini ( ambako serikali haijali kinachoendelea huko) matokeo yake wananchi wasio na hatia wanateseka sana na kwa taarifa yako si ajabu vifo vinavyotokea sasa vikazidi vile vya kipindi cha mgomo bahati mbaya wasiasa wahuni kama wewe hawavitangazi.
udaktari ni profession huwezi kuilinganisha na siasa na zamu hii mtajua kutofautisha siasa na taaluma!
 
Nadhani ni vizuri ukafahamu kama kweli ma Dr si wazalendo ukilinganisha na makundi mengine, pia mazingira wanayosoma hao madaktari wetu je yanawajengea uzalendo? Mwaka ulopita tumeshuhudia wanachuo wa IMTU wakisuguana na Uongozi wao kwa sababu ya ada kubwa wengi wao wakishindwa kuendelea na masomo, wanaoendelea ni kwa kujinyima sana, wewe unadhani watazirudishaje hizi? Elimu ya watu kujigharamia ni hovyo kabisa kwani haitakuwa na manufaa kwa wananchi kamwe. wapo wamesoma kwa kugharamiwa na serikali bure kabisa mpaka nauli unapewa lakini uzalendo ukowapi zaidi ya kujiongezea mishahara mjengoni tena bila upinzani kama wanaoupata hawa ndugu zetu madaktari. Uzalendo huanzia kwa viongozi/watawala kwa kuwa mfano kwa watu wake. Nakumbuka uzalendo wa Mwl Julius K. Nyerere- baba wa taifa amewahi kupunguza mshahara wake kufuatia maoni ya wananchi(Wanafunzi wa UD). Ni kweli ilikuwa nchi ya kijamaa wakati huo. Sina uhakika sana na mfumo tuliopo ila kwa maoni yangu si wakijamaa. "Think big"
 
Nimeona nikiwa kama mtz ninae itakia nchi yangu mema niwaeleze ndugu zangu ma dr ninyi si wazalendo ila mnacheza na mind za wa tz hili ni dhahiri,katika madai yenu yote mlio nayo ambayo ni takribani kumi na mawili,mmeona ili tuwaone wazalendo mchague dai linalo gusa watz(kuboresha huduma pamoja na vifaa duni) ndio iwe agenda kuu,dr kuzungumzia kwamba anagoma kwasababu ya 3500000 hamzungumzii mkijifanya kwamba mnatupenda sana,sisi tumewafaham kwamba mnataka kutumia watz,mnataka ifike hatua tuichukie serikali na tuingie mitaani,
ila msijisumbue kwani sisi hatuwez kuandamana kwasababu zenu zakisiasa.Bwana Chitage tunakufaham vizuri kwamba wewe ni mwanasiasa mzuri tangu upo chuo.Wekeni siasa pembeni fanyeni kaz.

Nadhani ni vizuri ukafahamu kama kweli ma Dr si wazalendo ukilinganisha na makundi mengine, pia mazingira wanayosoma hao madaktari wetu je yanawajengea uzalendo? Mwaka ulopita tumeshuhudia wanachuo wa IMTU wakisuguana na Uongozi wao kwa sababu ya ada kubwa wengi wao wakishindwa kuendelea na masomo, wanaoendelea ni kwa kujinyima sana, wewe unadhani watazirudishaje hizi? Elimu ya watu kujigharamia ni hovyo kabisa kwani haitakuwa na manufaa kwa wananchi kamwe. wapo wamesoma kwa kugharamiwa na serikali bure kabisa mpaka nauli unapewa lakini uzalendo ukowapi zaidi ya kujiongezea mishahara mjengoni tena bila upinzani kama wanaoupata hawa ndugu zetu madaktari. Uzalendo huanzia kwa viongozi/watawala kwa kuwa mfano kwa watu wake. Nakumbuka uzalendo wa Mwl Julius K. Nyerere- baba wa taifa amewahi kupunguza mshahara wake kufuatia maoni ya wananchi(Wanafunzi wa UD). Ni kweli ilikuwa nchi ya kijamaa wakati huo. Sina uhakika sana na mfumo tuliopo ila kwa maoni yangu si wakijamaa. "Think big"
 
Viongozi wetu wanajilimbikizia mali nyingi, halafu huduma za afya zinadorora, na si afya tu kaulize taasisi nyingine zinapata kiasi gani kwa matumizi ya kawaida. Serikali hii imeshashindwa kutambua wajibu wake, na hawana utu hata kidogo. Ni walafi kupindikia, ulafi huu ndio umetufikisha hapa. sasa wanaanza udictator. Patachafuka hapa na wote tutaumia.

E Mungu okoa hili Taifa, Hawa vingozi wakumbuke walipotoka.
 
Nape mnakuja na ID nyingii hivi jiulize kwanini hao vigogo kila siku wako India ulishawai kujiuliza na ukapata jibu. We na dhaifu wako mmekalia mshahara mshahara ndio wana haki
 
Sasa mambo yamewageukia wanatafuta huruma na sapoti kutoka kwa watanzania, wakubali tu kuwa wameshindwa wajipange upya.
 
Huu uzalendo unaohubiriwa tu kwa madaktari?
Liwalo na liwe!
 
Madaktari kugomea kutibu wagonjwa ni sawa na uuaji. Hawa ni wauaji tu. Nawaomba wajifunze kuhusu ulimboka: Je kama Ulimboka asingetibiwa angepona? Na wagonjwa ni hivyo wajue kuwa wameua watu wengi sana. Wameua sana
 
Ulimboka amepelekwa SA kwasababu TZ pamoja na kuwepo madaktari lakini viendea kazi vya kisasa havipo. Ndiyo maana tabaka la juu linaenda kutibiwa nje ya nchi kwenye vifaa vya kisasa! (Vitendea kazi ni baadhi ya madai ya madr.)
 
Madaktari kugomea kutibu wagonjwa ni sawa na uuaji. Hawa ni wauaji tu. Nawaomba wajifunze kuhusu ulimboka: Je kama Ulimboka asingetibiwa angepona? Na wagonjwa ni hivyo wajue kuwa wameua watu wengi sana. Wameua sana

hamna jipya hapa
 
Akili zako zinakutosha mwenyewe,haziwezi kumsaidia hata mtoto wa chekechea!!!
 
Back
Top Bottom