Madaktari wenzangu: Only "Mass resignation" itawaamsha watawala!

Wakiresign wanakomoa serikali au wagonjwa. Uchochezi mwngine hata hauna maslahi

Mkuu thinktank, wakiresign si kukomoa serikali au wananchi!Wao wameajiriwa tu lakini kuajiriwa kwao na mtumishi wako(Serikali) isiwetija ya kuteseka kwao. Ni vizuri pia kuuliza na kujaribu kuadadisi kidogo wale walio katika sekta binafsi na madaktari wa kitanzania walio nje, ni ninikilichowakimbiza huko!!

Kuna kitu tunakiita Job satisfaction, kwamba hata kama ni katika mazingira duni kikazi ukimpatia huduma mgonjwa, akipona wewe kama daktari unafurahi pia,lakini inasikitisha kuona watu wanaujuzi lakini vifaa hakuna, dawa hakunana zilizopo zimekwisha muda wake!! sasa ukiwa kama tabibu unaona bora kwenda mahali pengine ili angalau hata kama hawatajali maslahi yako kiasi uombacho mazingira ni mazuri na wagonjwa wanapona.
Inasikitisha kusoma miaka mingi na kusajiliwa katika mwaka wa saba baada ya masomo na internship na bado unashindwa kuhudumia wananchi ingawa una ujuzi.
 
hivi raha yako ni kuchochea Mgomo? sisi tumekataa maana hao madaktari na hizo T scanner hazituhusu tuacheni tuishi tunavyojua je? ni kwanini hamviachii hivyo vifaa vya humo Mahospitalini mkarudi mwakwenu?
 
Nakuunga mkono Dr. Mimi kuna kipindi nilikuwa Tarime nikamtembelea mgonjwa mmoja kwa sasa ni marahemu alikuwa na HIV. Nilikuta ndugu zake wakimuuguza bila hata gloves na wakati huyo mgonjwa alikuwa na vidonda sana na pia alikuwa akitapika sana. Roho iliniuma nikaenda kuuliza kwa manesi kama naweza kupatiwa gloves hata kwakununua. Nilipewa pair moja ya gloves kwa sh 2000 na ilibidi wale wanaomuuguza wawe wanapokezana hizo gloves. Sijui walizitumia kwa muda gani. Kwa wenzetu vitu kama gloves vinatakiwa kuwepo kila eneo lenye mgonjwa na zinatumiwa once nakutupwa. Inasikitisha sana pale viongozi wanapojifanya kama vile hayawahusu. Nadhani ni kwa sababu wao matibabu yao yako India na kwingineko. Ila Mungu yupo ipo siku watatoa hesabu ya dhamana waliyopewa kuongoza Tanzania




Ningependa kutoa pole kwa yale yaliyotokea na yanayoendeleakutokea katika nchini na nje ya nchi kuhusu sisi(madaktari).Pole kwa kumuuguzamwenzetu Ulimboka Steven(Dkt), Kushtakiwa kwa MAT, Kuhojiwa kwa Rais wetu NamalaMkopi(Dkt), Kufukuzwa kwa madaktari walio mafunzoni (Intern doctors), vitisho kwa wakuu wa idara n.k.

Mwaka huu Vyuo vikuu na shirikishi vya afya na tibavinategemea kutoa wahitimu kama ifuatavyo:

-MUHAS (150), KCMC(80), WBUCHS(50), HKMU(55), IMTU(45) naUDOM(0).
Kati ya hawa wapo wageni(foreigners) watakaorudi ktk nchizao, wapo ambao watakwenda kufanya internship katika hospitali za binafsi, nawapo wataenda kufanya kazi katika asasi zisizo za kiserikali(NGO)-kwaniinternship si lazima kufanya, ila hadi pale utakapoamua kufanya kazi katikahospitali. Kinachonishangaza serikali inasema inategemea madaktari 700 kutokavyuoni, inawatoa wapi?

MAONI:
Inawezekana katika kila jambo la nchi hii siasa(propaganda)imeingizwa, lakini si katika fani ya udaktari, hii ni fani(Profession) nainapaswa kuheshimiwa kama ilivyo. Si ajabu kiongozi kufika pale Hospitali yaTaifa na kukosa kipimo na kuambiwa kwenda Aga Khan au Regency, utamsikiaakisema “kwani havipo hapa” ukimweleza kuwa ni vibovu utasikia “wanapaswakuwakumbuka”..hii ni moja ya kauli ya kiongozi mmoja mkubwa serikalini!

-Si ajabu kumkutaSpecialist akifatilia damu kule Bloodbank,
-Si ajabu kumkuta Specialist analalamika hawezikuendelea na upasuaji kwani gloves zimembana sana(Sio saizi yake) nakushindwa kutumia vifaa vizuri,

Si ajabu kumkuta Specialist akisubiri hadi nguo za upasuajieti nguo hakuna!
Si ajabu kumkuta Specialist amejifunga shirt kichwani kamakofia, Si ajabu kumkuta specialist amevaa gauze kama mask!!
Si ajabu kumkuta Daktari amejihatarisha(being exposed) na damulakini hakuna Post Exposure Prophylaxis(PEP)

Hii ni katika hopitali ya Taifa, sasa jiulize kama hospitaliya Taifa hali ni hii, katika hospitali nyingine hali ikoje??

Kwa specialist, resident, registrar, interns wenye tabia ya kulalamika na kudaimabadiliko, ni mabadiliko yapi mnayoyadai ili hali muda wa mabadiliko hamsimamiimara katika kudai haki yenu??

Sitegemei madaktari wote kudai haki yao (kwani najua wasalitiwapo tu) lakini zaidi ya yote ni hawa wanaokuwa vuguvugu na wanafiki!!


KAMA WAZAZI/WALEZI
:

Mnawafundisha nini hawa wadogo wenu na watoto wenu, kuhusu kudai haki yako ya kikazI, “I know it is wisdom that takes courage to sit down and listen but it is the same wisdom which takes courage to stand for your right”.

KAMA VIONGOZI/WALIMU:
Unapokuwa ukipita round na wanafunzi wako(medical students,interns, registrar, residents), unajisikia nini pale wagonjwa wanapokufiakatika round, kwa sababu tu ya kukosa huduma ambayo ungeweza kutoa kwa mgonjwana kuwa chahu kwa wanafunzi wako? Wanafunzi wanakuonaje wakati ukisema, “in other countries they could have done soand so” wakati muda wa kudai hivyo vifaa na dawa hizo ndio huu? Wanafunziwako wankuonaje wewe kama specialistwakati wenzako wako katika mgomo wewe unapita round, tena wanafunzi wako wakiwana vitambulisho tu bila makoti, wewe ukiwa na koti?

KAMA WASTAAFU NAMADAKTARI BINGWA WATARAJIWA:
Wakati wadogo/watoto wetu(intern doctors) waakiwa wameachiwamzigo huu, najiuliza kwa mfano tunapokuwa katika MWR, Discussion Panel huwatunapima uwiano wa wagonjwa na treatment options:
Leo hii tukipima Option ya MASS RESIGNATION inashindikana?

-Neurosurgeons(4),
-Orthopeadicsurgeons(15),
-Pediatricians(30),
-ObGynaecologists(45),
-Physicians(60)regardless of subspeciality ie Neurolgist, Gastroenterologist,etc.
-Psychiatrist(30)-notpsychologist,
-Surgeons (40)-regardlessof subspecialty like Cardiothoracic, Plastic surgeons etc,
-Otorhinolaryngologist(20),
- Anaesthiologist 25(notanaeshetist),
-Opthamologist 30(notoptician,optometrist)…HII NI IDADI KWATANZANIA NZIMA.

Hofu kwetu kama specialists na hawa residents ni kwamba mafao, lakini tujiulize leo kama Profesa anapewa mafao ya 50,000/=Tshs kwamwezi hii ndiyo inayokufanya usigome au kuamua kuresign? Kweli?

-Cha kushangaza kuna megabrains nyingi sana za kutegemewa lakini wanaact kama hawajui hili, naamini specialists, Residents, registrar nainterns pamoja na medical students tulikuwa na APGAR SCORE ya 10 – 10!! Sasa inakuwaje microbrains ifanye hivi kwa megabrains.

If I weigh the option of mass resignation I believe it fits the puzzle, because I believe it won't take even a month for the government to call us back to the discussion table (UNDER OUR TERMS THIS TIME) , and in the mean time(I dare to believe that none of us can perish because of financial crisis).

On the other side the Government cant import other doctors,look at WHO doctor-patient ratio, every country needs one, and for those whothink they will import, ask yourself these questions from which country? Will theybe able to pay them(THIS should be above their home salary), accommodation,transport?

This is a profession(medical terminologies) and not just mere English, I bet they might needtranslators, how many? Will they pay them? Will those doctors work in thisenvironment or they have to come with medical equipments, medicine? For howlong will they have to stay here? Will they gain trust to people(rapport etc)?

Hebu tusimame pamoja katika hili, mengi yanafanyika bila mpango hukumu kusomwa mahakamani wakati huo huo, interns kufukuzwa ..sasa unajiuliza kesi ya nini kama tayari wameshafukuzwa, na Rais kuingilia madaraka ya mahakama (kutoa hukumu wakati jambo hilo hilo kukataliwa bungeni), lakini kuumizwa sana kwa Dkt,UlimbokaSteven.

PLEAD/CALL: LET US STAND TOGETHER NOW MORE THAN EVER, THIS TIME NOT IN TOTAL TOOLS DOWN BUT IN MASSRESIGNATION.
 
Wanachotakiwa kufanya madaktari ni kuwaelimisha wananchi. Wananchi ndio waishinikize serikali na viongozi wao. Katika hilo madaktari wanajitwika mzigo ambao sio wao na wala hawana uwezo wa kuubeba. Bila kuelimisha wananchi, hawawezi kujua nini kinakosekana kitaalam.
 
Wakati mwingine huwa ninapata shida sana kufikiri ni jinsi gani watanzania tulivyojawa ushabiki, ujinga, upuuziaji wa mambo ya msingi na kuunga mkono matendo maovu na zaidi ya yote kuona kila nia mbaya kwa kila jambo jema linalotokea au kutendwa!!
1.
Ushabiki(swala hili linapoangaliwa kimtazamo wa vyama, wakati ni la kitaifa)

2.
Ujinga (kuchangia mada kwa kuangalia matokeo ya jambo na si chanzo cha jambo)

3.
Upuuziaji wa mambo ya msingi (unapoita jambo lina umuhimu lakini unashindwa kulithamini au kufanya juhudi kulitatua)

4.
Huruma kwa vitendo viovu (kushabikia kuteswa kwa mtu yule yule unayemuhitaji akusaidie kuokoa maisha)

5.
Fikra mbaya (kuwa jambo lolote linalodaiwa au kuombwa lina nia mbaya na mwombwaji)



MTAZAMO:

-

USHABIKI: Jambo hili linapaswa kuangaliwa kwa umoja(kama taifa) na si ubabe, ushabiki wa vyama, elimu, wala udini kama linapotaka kuelekea( kwani kuelekea huko kunafanya watanzania wengi kuangalia lile linalokuja na si chanzo ni nini) bali kwa kutumia busara.



-
UJINGA: "Ujinga" si tusi kama hili neon lichukuliwavyo na watu wengine, ila lina maana ya kutokuwa na ufahamu. Ningeshauri wananchi wasiojua chanzo cha tatizo kujua na kuangalia nini ni chanzo (madai) cha mgomo huu wa madaktari. Lakini kama ni shida kupatikana kwa madai ya madaktari, unaweza kuyasoma hapa;



i. Kuondolewa kwa viongozi wakuu katika W/Afya kutokana na ushahidi wa uovu wao

ii. Kuboresha huduma za Afya hospitalini(ongeza vitanda, watumishi, madawa, zana za kazi)

iii. Kuwapatia watumishi wa sekta ya Afya kadi ya kijani ya Bima.

iv. Kudai posho ya kuitwa kazini kwa 5%.
v. Pendekezo la posho ya kufanya kazi katika mazingira hatarishi (30%) AU chanjo
vi. Pendekezo la posho katika mazingira magumu (30%) AU makazi.
vii. Pendekezo la mshahara kuwa mil.3.5, (sawa na ongezeko la 70%)





Katika makubaliano ya serikali na madaktari ombi la kwanza liltekelezwa(kwa ucheleweshwaji), wakati ombi la nne llikipangwa kutekelezwa kwa nusu asilimia pendekezwa hadi pale mazungumzo yatakapokwisha (ambayo haijatekelezwa hivyo ingawa ilisemwa hivyo BUNGENI). Kutokana na madai yaliyobaki kuhitaji pesa "nyingi". Serikali ilitoa tamko kuwa itashughulikia na madaktari kukubali kurudi kazini na katika bajeti ijayo ya 2013/2014 kuongezwa kwa ajili ya madai hayo muhimu.(ambayo w/Afya imezidi kupunguzwa)


Ni nani asiyejua umuhimu wa kujikinga na magonjwa(homa ya ini, UKIMWI, kifua kikuu)?leo hii daktari yule yule anayefundisha jamii jinsi ya kujikinga, anapoomba chanjo au fedha ili atafute namna ya kujikinga ni shida?!



Mazingira ya kijijini na upatikanaji wa huduma unajulikana, ni tofauti na mjini lakini pale madaktari wanapoomba posho iongezeke afike huko katika vijiji katika kutoa elimu(kwani ni moja ya kazi yake) inakuwa shida?


Si ajabu kukuta mwananchi au kiongozi akilalamika kuwa, "mnadai pesa nyingi", "wanatuelekeza kwenye maduka yao ya dawa" , "wanachukua dawa za hospitalini". "wanatuelekeza katika hospitali zao" lakini akisahau kuwa kisheria mshahara wa mwajiriwa unategemea:
*muda alioutumia akiwa shuleni (ugumu wa masomo),
*kiwango cha elimu,
*ugumu wa kazi,

*na muda wa kufanya kazi.



Na ndiyo sheria hii hii inayodai madai kama ya kuitwa kazini(call allowance)/katika fani nyingine ikiitwa "overtime" isemayo inapaswa kuwa(5%) kisheria, lakini leo ikidaiwa ni shida?



Wakati mwingine utasikia wanasema, "wanatuelekeza kwenye maduka yao ya dawa", "wanachukua dawa za hospitalini". Lakini wanachanganya na kudhani kila avaae koti jeupe hospitali au duka la dawa ni daktari!! Kama kila ambaye anafanya kazi ikulu ni Rais, muda huu unaosoma makala hii tuna marais wangapi??!



Nijuavyo mimi pale Muhimbili wodi za watoto, wakina mama mnajua hali ilivyo(wagonjwa watatu kutumia kitanda kimoja, hivyo sijui kama wagonjwa wanakuja kupata matibabu au kupeana magonjwa)! hakuna vitendea kazi wala madawa

Hivyo ndivyo ilivyo pia katika hospitali ya Bugando na pale KCMC, kule Mbeya ndio hatari zaidi.


-Leo hii mama mjamzito akija hospitali kujifungua bure(kama ilivyo katika sera) na kuambiwa akanunua pamba, analalamika anaonewa, akidhani madaktari watakula hizo pamba!


-Watoto wanakufa kwa kukosa madawa na wakiambiwa wakatafute dawa nje(kwa faida yao wenyewe kwani madawa hakuna inakuwa ni kosa)


-Ukitaka kufanyiwa upasuaji na kuambiwa hakuna damu, ndugu waje kuchangia damu au uchangie gharama, watu wanadhani madaktari wanakunywa damu! Kwani hata kama ndugu wakichangia inabidi kupimwa kutokana na magonjwa, na wakati mwingine wagonjwa hawapewi damu kutokana na damu iliyotolewa na ndugu zao ni chafu(ina magonjwa-na haitakiwi hata kumwambia mgonjwa siri hiyo).


-Unapokuta mstari mrefu wa kupigwa picha za mionzi(X-ray) na kuambiwa machine hazifanyi kazi, wananchi wanadhani ni madaktari walioharibu machine au kuipeleka hospitali binafsi. Mf Hospitali ya mkoa/rufaa TANGA. Je hospitali za wilaya zina hali gani? Vijini je?


Madai ya posho, ni pendekezo, hivyo kama serikali inapaswa kuangalia ni kwa kiasi gani inaweza kuongeza posho/mishahara na tatizo kutotokea tena na si kutumia fursa hiyo kuongeza kiasi chochote kisichokuwa na mantiki na kusema imeongezeka!! Wapi kuna shurutisho kwamba bila mil3.5 haturudi kazini, au tunatofautiana katika kusoma na kudadavua?


Lakini zaidi ni pale kunapokuwa na ushindani kati ya kundi la wasomi ambalo wananchi wenyewe ndio wanawaita, "cream of the nation' ( waliokuwa wakifanya vizuri sana darasani, hii ikiwa ina maana ya shule za sekondari, na elimu ya juu -sasa kwa umoja wao) na makundi mengine, na wananchi kudhani kundi hili halina maamuzi ya busara au kuchambua mambo ya msingi, madai, madhara, uwezekano wa utekelezaji KABLA YA MGOMO WENYEWE..(HII HAIMAANISHI HAKUNA WENYE BUSARA PIA AU UFAULU WAO HAUKUWA MZURI KWA KUNDI JINGINE isipokuwa kwa kulinganisha na kundi la hao mnaowaita hawana utu)





- UPUUZIAJI WA MAMBO YA MSINGI: Kuna msemo wa kiingereza unaosema, "Desperate times, take desperate measures" lakini kama hatua zitakazochukuliwa ni za ubabe basi ninahisi tutakuwa tunatofautiana katika kutoa maana ya neno DESPERATE. Sekta ya Afya ni muhimu kama zilivyo sekta nyingine, lakini wakati mwingine ni muhimu zaidi ya nyingine kutokana na kuhusishwa moja kwa moja na uhai wa watu. Hivyo kama ni kutokana na umuhimu huu, inapaswa kuangaliwa matatizo kama ambayo yaliyotokea na ambayo yataendelea kutokea iwapo hayatapatiwa ufumbuzi.



Leo hii wananchi wengi wanaishi na watumishi wa ndani (housegirl/boy), wengine huwa wanaonewa na kutendewa vibaya hata kama makosa yakiwa ni ya watoto wa mwajiri, lakini ndiye huyu huyu mtumishi wa ndani unayetegemea akupikie chakula!! Chakula kile kile kinachoweza kuondoa uhai wako kwa sumu ya panya inayouzwa mitaani kwa bei nafuu!!!? Inakuwaje ukimuonea hadi na yeye anapoamua liwalo na liwe huku ukimwacha apike chakula cha familia?



- KUUNGA MKONO VITENDO VIOVU: Wakati mwingine ninajiuliza hivi hawa ndio wale wale watanzania wasemao wana amani, utu na uzalendo? Inakuwaje kitendo alichofanyiwa Ulimboka Steven(Daktari) kushabikiwa namna hii? Je, hata kama ingekuwa kweli anadai mambo yasiyo na msingi angepewa stahili ile?

Yuko katika jamii (jumuiya ya madaktari), na kwa watu wengine busara zao(madaktari) inatafsiriwa kana kwamba hawana hisia. Je, wakifanya kazi kwa shingo upande, itakuwaje? Je, unadhani viongozi watakwenda hospitali za serikali au ni mwananchi yule mwenye kutoa maneno mabaya muda huu kurudi katika mikono ya wale aliowaudhi akitegemea uhai wake uwe salama?ni kweli utasalimika kwa maneno ya kejeli, na dharau anayoyatoa mwananchi?



Lakini ni kwanini mwananchi(au kama ilivyokuwa kwa kiongozi Bungeni) aseme kuwa amepata stahili yake?? Je, si serikali inapaswa kulaumiwa kwa kutotoa huduma na si mwajiriwa?



- FIKRA MBAYA: Watu wanajiuliza hivi madaktari wana utu kweli? Kweli kuacha watu wafe kwa ajili ya "maslahi" yao wenyewe? Watu waliosomeshwa bure na pesa za kodi ya wananchi? Lakini wakisahau kujiuliza madai ya msingi ni yapi na ni nani yuko katika mkataba wa kutibu wananchi wake!

Ukiwa na mtoto mnyenyekevu/muadilifu/mwenye tabia njema na ghafla akabadilika nadhani unapaswa kujiuliza wapi wewe kama mzazi/mlezi hufanyi jitihada au umeondoa nini kwake alichokuwa anakipata.

Lakini katika kujibu maswali ya wananchi (labda kutokana na kutoelewa undani wa jambo hili) Ndiyo, Madaktari tuna utu(kwani nami ni mmoja wao), na hatuwaachi wananchi wafe ila tatizo kubwa ni kutoelewa nani anapaswa kulaumiwa(kwani badala ya wananchi kutoa ushauri na njia mwelekeo wanaendelea kulumbana), hakuna mahali ilipoainishwa kuwa madaktari watawahudumia wananchi ila Serikali itatoa huduma ya Afya kupitia waajiriwa wake (Madaktari), ila wewe kama mwananchi unapaswa kuidai Serikali kwani umelipa kodi na kwa kuwaweka madarakani umeingia na mkataba na si mkataba na daktari.



Ikumbukwe kuwa madai ya madaktari yapo katika sehemu mbili. Sehemu ya kwanza ikiwa ni kutoa huduma kwa wananchi NA huduma kwa mwajiriwa(daktari) ikiwa sehemu ya pili. Inashangaza kuona kuwa wananchi wako tayari kutoona umuhimu wa sehemu ya kwanza(madawa, vitanda, vifaa vya upimaji) na kutounga mkono sehemu ya pili ya madai(kutumia nguvu, akili na uwezo wao wote kupinga PENDEKEZO la posho ikiwa kama dai moja wapo)!!

Kwa wafanyakazi, wengi(kama sio wote) kabla ya kupewa ajira mliulizwa pendekezo la mshahara wako uwe kiasi gani, na ilipoleta utata mlijadiliana na mwajiri wako, kwa wengine ilipokuwa shida mliacha nafasi hizo na kwenda sehemu nyingine. Je, utofauti huo uko wapi katika sekta ya Afya?



Kama watu wanadhani bado madaktari wanasomeshwa bure kama inavyodaiwa, wawaulize wadogo zetu walioko vyuoni HKMU,IMTU, WBUCHS, KCMC, nk. Takribani miaka miwili iliyopita wanafunzi wa IMTU waligoma kwa sababu ya ada yao kuongezwa sana, sasa sijui kusomeshwa huku kunakoongelewa kunatoka wapi!
 
Umeongea vizuri sana, ila hiyo haiwezekani kwa mind set and courage ya Mtanzania.

Ninachowashangaa nyie madr ni kimoja tu, kwanini unaanzisha kitu huwezi kukimaliza! hebu ona sasa ulimboka sijui Olimboka wa watu kaumizwa bure na rais wa mat ana kesi alafu wengine wamefukuzwa wengine wanarudi!!!!!!!

C'com guys DONT HUNT WHAT YOU CANT KILL.

YAANI MMENIBOA SAAAANA MADR, MMEGOMA MMESABABISHA UNREST ALAFU MNARUDI BILA HATA DAI MOJA KUTIMIZWA!!! SERIOUSLY!!! :redface:

Iliyobakia sasa tuwafungulie mauaji ya bila kukusudia hata wakishinda kesi watakuwa wamesota vya kutosha hadi viatu vimeisha soli halafu wanarudi kitaa kuanza kuhangaika.
 
Iliyobakia sasa tuwafungulie mauaji ya bila kukusudia hata wakishinda kesi watakuwa wamesota vya kutosha hadi viatu vimeisha soli halafu wanarudi kitaa kuanza kuhangaika.

wapi duniani uliwahi kuona/kusikia daktari anahangaika mtaani??!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
wengine wanakenua na kupump madr waache kazi kwa sababu wao wako nje huko wanao uhakika wa kutibiwa. sie wengine hata kusafiri hivi sasa twaingiwa hofu maana ukipata ajali waeza kujiozea zako na kufa a slow painful death huku ukijiona na nduguzo wakikutazama na kuanza matanga ilhali ukiwa hai. mi sijui kila mtu akianza kudai 'haki' yake sijui itakua taifa la namna gani maana nchi maskini kila mtu huona anaonewa! specialsist mzima unalalamikia gloves wewe specialist mzima unakosa ela ya kujinunulia gloves?? acheni huo ubahili! hivi mnajua sie huku maofisini tunanunua karatasi kwa pesa zetu mfukoni na vitu vingine kibao?? wakati mwengine tunasafiri kikazi bila hela na serikali inalimbikiza bila kulipa! hivi mnadhani ni nyie tu wenye matatizo!

una matatizo ya akili
 
Kosa walilolifanya madaktari ni kuwakatalia Chadema kuitisha nguvu ya umma ili kuishinikiza serikali kutekeleza madai yao. Hawana wa kumlaumu, walidhani wanaweza wenyewe. Ukweli nikuwa nchi hii ni CDM peke yake kinachoweza kuhamasisha uasi dhidi ya serikali na nguvu ya umma ikafanya kazi, wala tusidanganyane.

Makundi mengine lazima mjue hili kuwa CDM ikishirikishwa hakuna litakaloshindikana na hili hata serikali na ccm yao wanalifahamu.

Madaktari jipangeni upya safari ijayo msifanye makosa, waalimu nanyi msituletee usanii, katika harakati za ukombozi usanii na usaliti havivumiliki kamwe.

MUNGU IBARIKA TANZANIA
 
Maneno hayo ni sawa lakini kama ni dhulma ipo kwa waTZ wote. Madaktari ni sehemu ndogo ya tatizo katika nchi yetu. Kwa ujumla wake, huduma zote za jamii ni kama hamna. Hapa tutagawanyika tu kwa maoni na mitazamo tofauti. Dira ya taifa haionekani.
 
Kwa kuwa moja ya mashinikizo ya madaktari kwa serikali ni vifaa ambavyo kwa namna moja au nyingine vingetusaidia moja kwa moja sisi wananchi lakini ktk mataifa yenye uoga wa kudai haki za msingi watz namba moja. hivyo basi tatizo la madaktari ni sisi wananchi ndio tunaosababisha liwepo mpaka leo laiti kama tungeungana na madaktari kwa namna yeyote ile kama walivyo na umoja wenzetu wa misri,syria,libya muhimbili ambayo ni hsptal ya taifa watu wasingeandikiwa refelar kwenda india kupima presha tu au kupasuliwa jipu.

mkuuu! sasa wananchi tunaumwa na hatutubiwi je? tutapata wapi nguvu na uwezo wa kuungana nao. na hao walio wazima ndio wanaotuuguza je? watuache tufe na kuendelea kuumia ili waje kuungana na madoctor. kitendo cha kwenda hospitali na wao kutuambia hakuna huduma na sisi kurudi majumbani bila malumbano nao ndo tayari tushawaunga mkono ki desing yake mkuu! wao wawasubiri UN tu watawaunga mkono, si ndo sehemu sahihi walioiona kukimbilia! vikodi vyetu pia wanavyolipiwa vi mshahara wanavyo vilalamikia jaman pia si tumewaunga mkono! je?huyo dr ulimboka watu wa kawaida pia si wamewasilisha michango yao kiana mkuu!
 
Kwa kuwa moja ya mashinikizo ya madaktari kwa serikali ni vifaa ambavyo kwa namna moja au nyingine vingetusaidia moja kwa moja sisi wananchi lakini ktk mataifa yenye uoga wa kudai haki za msingi watz namba moja. hivyo basi tatizo la madaktari ni sisi wananchi ndio tunaosababisha liwepo mpaka leo laiti kama tungeungana na madaktari kwa namna yeyote ile kama walivyo na umoja wenzetu wa misri,syria,libya muhimbili ambayo ni hsptal ya taifa watu wasingeandikiwa refelar kwenda india kupima presha tu au kupasuliwa jipu.

Usifikiri watz ni wa p.u.uzi,tunafaham ma dr wanamadai mengi sana na niyamsingi lakini kamwe watz hatuwez kuandamana kwani ma dr wamekuwa wa p.u.u.z kwakuchanganya siasa kazini,wameona ili watz tuwape surpot wajidai kwamba wanatupenda sana kwa kuweka msisitizo zaidi kwenye kuboresha hosptl na kujifanya mishara sio agenda yao,ma dr sisi tumewagundua nyinyi si wazalendo kinacho wasumbua ni maslahi binafsi haya mengine ni siasa tu!
 
Nimeona nikiwa kama mtz ninae itakia nchi yangu mema niwaeleze ndugu zangu ma dr ninyi si wazalendo ila mnacheza na mind za wa tz hili ni dhahiri,katika madai yenu yote mlio nayo ambayo ni takribani kumi na mawili,mmeona ili tuwaone wazalendo mchague dai linalo gusa watz(kuboresha huduma pamoja na vifaa duni) ndio iwe agenda kuu,dr kuzungumzia kwamba anagoma kwasababu ya 3500000 hamzungumzii mkijifanya kwamba mnatupenda sana,sisi tumewafaham kwamba mnataka kutumia watz,mnataka ifike hatua tuichukie serikali na tuingie mitaani,
ila msijisumbue kwani sisi hatuwez kuandamana kwasababu zenu zakisiasa.Bwana Chitage tunakufaham vizuri kwamba wewe ni mwanasiasa mzuri tangu upo chuo.Wekeni siasa pembeni fanyeni kaz.
 
Yap umechanganua vzr sana ingawa umechanganya kidogo lakin kwa sis 2lio kwenye taaluma hii 2mekupata vzr sana.

Shida kubwa ni wa2 wengu kutokuuelewa ukwel huo, hasa wanaoish mjin coz wana options eidha kwenda Gov or Private, kwa ndg ze2 wa vijijin ndo wanaielewa shida.

Em pata picha kama Muhimbili wanalalamika mapungufu kibao, Je huko mikoan pakoje? Ngoja 2one, wanawafukuza 400 then wanategemea kupata 150, huku idad ya wagonjwa ikiongezeka, ni ujinga mtupu..!
 
Wanachotakiwa kufanya madaktari ni kuwaelimisha wananchi. Wananchi ndio waishinikize serikali na viongozi wao. Katika hilo madaktari wanajitwika mzigo ambao sio wao na wala hawana uwezo wa kuubeba. Bila kuelimisha wananchi, hawawezi kujua nini kinakosekana kitaalam.

Tena ni kweli mkuu - tena walitakiwa wafanye hivyo mapema - mgomo usingekuwa lazima. si wao na wananchi tu bali pia wangesaidiwa na vyombo vya habari na vyama ambavyo hivi sasa vinajipambanua na migomo. lakini kutanguliza migomo na kusababisha vifo - wamechemsha na kuongeza chuki dhidi yao. na declare interest ya kuwa na chuki kali kwa waliogoma na kusababisha vifo vya wa TZ wasio hatia na hasa watoto - wameshiriki kukiangamiza kizazi kijacho na Mungu aisikie laana hii.
 
Tena ni kweli mkuu - tena walitakiwa wafanye hivyo mapema - mgomo usingekuwa lazima. si wao na wananchi tu bali pia wangesaidiwa na vyombo vya habari na vyama ambavyo hivi sasa vinajipambanua na migomo. lakini kutanguliza migomo na kusababisha vifo - wamechemsha na kuongeza chuki dhidi yao. na declare interest ya kuwa na chuki kali kwa waliogoma na kusababisha vifo vya wa TZ wasio hatia na hasa watoto - wameshiriki kukiangamiza kizazi kijacho na Mungu aisikie laana hii.

Matatizo ya madakatri ni

1. wanafikiri wana akili nyingi kuliko watu wengine. Hawajui kuwa kufaulu mtihani siyo kipimo pekee cha akili

2. wanatumia mbinu za kishule kutatua migogoro ya kikazi. Hawatambui kuwa migogoro ya shule na kazini ni vitu viwili tofauti.

3. Viongozi wao wamejipa hati miliki ya kufanya maamuzi yote.

Nina uhakika madaktari wengi tu hawaungi mkono maamuzi, ila wakijaribu kusema wanafungwa mdomo kwa kutumia intimidations za namna mbalimbali.
 
Kwa hili kila mtu atafikiria lake lkn bado tukubali serikali inawajibu wa kutuboleshea mahosptal yetu mishahara hasa ya sekta ya afya <kada zote> polisi na walimu hawa ndo wana idadi kubwa yani isionekane mgonjwa anatoka hosptal ya songea anakuja muhmbili kwa huduma ambayo kabda ingepelekwa kule kwa mil 1oo tu.

Au daktar ambae ni mwajiliwa wa selikar anafanya parttym sehem flan kwa sabab mshahara anaopata serkaln aumtoshelez hii ni aibu au kuona mwalimu anakwenda shule na ubuyu au vishet kisa hana mshahara unaomtosheleza bd tunachangamoto
 
Kwa hili kila mtu atafikilia lake lkn bado tukubali serikali inawajibu wa kutuboleshea mahosptal yetu mishahara hasa ya sekta ya afya <kada zote> polisi na walimu hawa ndo wana idadi kubwa yani isionekane mgonjwa anatoka hosptal ya songea anakuja muhmbili kwa huduma ambayo kabda ingepelekwa kule kwa mil 1oo tu au daktar ambae ni mwajiliwa wa selikar anafanya parttym sehem flan kwa sabab mshahara anaopata serkaln aumtoshelez hii ni aibu au kuona mwalimu anakwenda shule na ubuyu au vishet kisa hana mshahara unaomtosheleza bd tunachangamoto
 
Back
Top Bottom