Mkandara thanks for your informative post. Labda nianze na hiyo quote hapo juu, inabeba ujumbe mzito ni kweli lakini; it also depends on who is saying or using that phrase. Kama ni JK huo ujumbe/msemo hauna maana yeyote zaidi ya propaganda. Kwenye maisha tunakutana na watu wanaotupa wosia/advice tofauti. Wengine watapokea ule ujumbe na kuandika mahali au kuutunza mahali kwa kumbukumbu; wengine wataandika mahali lakini wataenda further than that; wataufanyia kazi (put the words into action). Sasa haya maandishi ya JK kwenye face book hayana tofauti na mtu aliyeandika advice nzuri akaweka mahali (frame it and hang on the wall) kwaajili ya kumbukumbu bila kuufanyia kazi. Kwanini nasema hivi:
1)JK anataka sisi tuwe part of the soln lakini yeye ni part of the problem. Nitatoa mifano ku-support ninachosema hapa. JK anahimiza watanzania hasa watanzania nje ya nchi wawekeze nyumbani (good idea). Lakini mimi nimefanya kazi nje ya nchi kwa jitihada zangu nakuja TZ kuanzisha biashara ya hotel; kwanza natakiwa kila ninapopita e.g.kuomba leseni etc niache 10%. Nikilalamika na kutoa taarifa TAKUKURU nobody cares. Kumbuka biashara yangu sio kwa faida yangu pekee lakini pia ndugu zangu watafaidika kupata kazi, na pia serikali itajiongeza mapato (that is me being part of the soln to TZ poverty). Pamoja na kupambana stage za mwanzo kuweza kusimamisha biashara yangu, bado nakuja kugundua mimi kama mwekezaji wa ndani nalipa tax wakati mwekezaji wa nje anakwepa tax. Nikilalamika na kuripoti sifiki mahali kwanini: mwekezaji anauhusiano/urafiki wakaribu zaidi huko magogoni kuliko mimi mtu wa kawaida. Nikiwa nafikiria nifanye nini kuhusu hili; then inaibuka tatizo lingine (uhaba wa umeme). Kutokana na hilo nalazimika kuwa na genereta stand by ili biashara yangu iendelee. Nikiwa nasubiri wabunge waje na kitu concrete kuhusu soln ya umeme kwaku-mbana Ngeleja, ndio inakuja hii trend ya Jairo style. Kuongeza pain kwenye kidonda nakuja kueleweshwa kwamba hakuna wakuweza kuwaadhibu watu kama Jairo kwasababu ndio "mtindo uliopo" and so the only order to clean this mess has to come from Mr. President himself.Kutokana na hayo na mengine mengi naomba nieleweshwe who is part of the problem and who is part of the soln.
a) JK kufumbia macho ufisadi is it part of the soln or part of the problem? Unamuhamasishaje mwananchi kuwekeza au hata kujitolea kwenye community wakati anajua wazi mafisadi wana-benefit at others expense?
b) How can JK and all of us expect Waalimu, Madaktari, Mapolisi wawe part of the soln wakati hatujali mchango wao? Kama tungewajali tunge-limit spending (cut down safari zisizo za lazima, posho, ziba mianya yote ya watu wanaokwepa kodi including haya makampuni yanayobadilisha majina kila baada ya miaka 5 etc) ilituwalipe watu hawa mshahara unaostahili. I mean njia zakuongeza government revenue ziko nyingi lakini watendaji hatuna (JK & Co are definately not playing their part).
c) Unam-convince vipi mtu atii mamlaka vyombo vya sheria e.g. mahakama wakati wewe unachagua incompetent judges (majaji wa vodafasta) ambao hata hiyo sheria yenyewe hawajaijua vizuri leave alone practice that much? Kweli unategemea ni play part yangu kwakuamini nitapata haki yangu from someone who does not know what she/he is doing? I can play my part to report thieves, corrupted leaders etc; but I also need the government to do their part, not only bringing them to justice but also provide fair justice (Refer Issue ya Chenge; waingereza wamefanya almost half of the work in their investigation but look at what JK and his people are doing!!!? And the list goes on and on.
Ni ukweli usiopingika wananchi wengi wa TZ wana nia yakufanya mazuri kwaajili ya nchi lakini siku zinavyozidi kwenda wanakata tamaa. Haitusaidii kuangalia utawala wa Nyerere, Mwinyi, Mkapa ulikuwaje kama wengine wanavyo-justify hii mess. Why; Because tumeshapita huko; tunachotakiwa sasa nikujifunza where we went wrong and then move forward. However, we can not move forward under JK leadership in this manner. Me and you + others agree something drastic has to happen, and the question is; what is the best approach to bring those changes before it is too late? Life is what is coming and not what was.
Me and you + others agree something drastic has to happen, and the question is; what is the best approach to bring those changes before it is too late? Life is what is coming and not what was...Thank U mkuu wangu kwanza kwa ku acknowledge kwamba tatizo ni Kikwete. Hilo moja maana sii watanzania wote wanaamini hivyo. Pili mimi nasema tatizo sio Kikwete peke yake hata sisi Watanzania ni TATIZO..Kwa hiyo hapa tunapata sura mbili ambazo ni tatizo na kwa ujumla wake ndio tunaijenga sarafu moja ya Utanzania..Yeye JK kama reflection yetu sisi sote ni TATIZO kama tulivyo TATIZO sisi wenyewe.. Umenipata hapo mkuu wangu.. Na tukianza na kuamini hivyo tu, nadhani utakuwa mwanzo mzuri wa kutafuta ufumbuzi..
Mkuu wangu maelezo yako yoote hapo juu kuhusiana na mapungufu ya JK na ukaorodhesha mchango wako pamoja na raia wengine ambao wamejaribu pasipo mafanikio kulijenga taifa letu lakini yalipuuzwa na utawala wa JK.. Hayo yote mkuu wangu, ni mchango ambao ulikuwa WAJIBU wa kila raia, kila mtanzania ktk hali ya kawaida ktk ujenzi wa Taifa katika Kujikimu na mahitaji yetu ya kawaida... Yaani ili tuendelee tulitakiwa kufanya kadha wa kadha na rais alitakiwa kutoa fursa hizi na zile na kama angekuwa HIVYO tusingekuwa hapa tulipofika, lakini haikuwa hivyo!..JK hakuwa rubani au niseme dereva mzuri, na sisi abiria hatukupata nafasi ya mchango wetu kuingia ktk grid la maendeleo ya kitaifa kwa sababu za kisiasa zaidi (hizo nguvu mpya, ari mpya, na madudu yake) ndio maana tumefika hapa tulipo..
Kwa bahati mbaya yeye JK haoni tatizo lake na sidhani kama atakubaliana na uloyaandika hapo juu, lakini pia ni bahati mbaya nyingine hata wewe na Watanzania wengi hawakubaliani na maelezo yangu kwamba wao pia ni sehemu ya tatizo.. Upeo wa kifira wa JK na wa Watanzania wengi hatuna tofauti kabisa na ndio maana kiuchumi MAHITAJI yamegeuka kuwa MATATIZO. Ukosefu wa umeme haukuanza na Ngeleja wala Jairo, tulijua toka JK akiingia madarakani na kwa bahati mbaya EL alitwambia ataleta mvua za kisayansi na JK leo anasema Hiyo ni kazi ya Mungu..sasa unategemea kitu gani kwa viongozi ambao ndio walikuwa wa kwanza kukimbilia Loliondo kupata kikombe cha babu ikiwa na maana wana magonjwa sugu na hatuyafahamu.. hawa watu wanaamini kweli uchawi zaidi ya sayansi kwa hivyo unapowapa madaraka unategemea wafanye miujiza gani?
Kwa hiyo mchango wako sii hoja tena, uzembe wa JK sii hoja tena kwa sababu hatuwezi kwenda popote tukitumia mifano ya nyuma ambayo ilishindikana na tumefika hapa tulipo leo. Lakini maadam tumejua kwamba tumekwama na sababu ya kukwama ni kwamba sisi wenyewe ndio sababu WE ARE PART OF THE PROBLEM (including JK mwenyewe) hivyo basi to be part of the solution - we got to be responsible/accountable.. Kwanza tukubali na kutambua kwamba sisi sote ni sehemu ya tatizo, kisha tuache ushabiki wa vyama, makundi nakadhalika ndipo tunapoweza kuchambua vizuri mbinu nzuri za kufanya..
Mkuu wangu tumekwama kiuchumi, tumekwama kwa kila hali bora ya kimaisha.. Hivyo basi kwa kutazama hali halisi ya leo hapa tulipokwama, ndipo tunapotakiwa kuja na strategy nyingine kabisa ya kujikwamua toka hapa tulipokwama.. Kama vile gari lililokwama ktk tope, huwezi kuendelea kukanyaga mafuta ili kutumia nguvu zaidi ya farasi kulikwamua toka ktk tope wakati abiria wamekaa ndani ya viti wakichungulia nje.. Kuamini kwamba lilokwama ni gari hivyo ni kazi ya dereva na wenye gari kujikwamua ni mawazo mgando ambayo yatatushindisha porini...Pia kuamini na kutegemea nguvu za farasi za gari letu ni maamuzi mabaya kwani kila tunapokanyaga mafuta zaidi ndivyo gari linavyozidi kuzama ndani ya tope..Kwa mwerevu hataendelea kukanyaga mafuta bali kutazama mahusiano ya hapo tulipo, tope, uzito wa gari na mzigo, kukwama na kadhalika ili kufiikia maamuzi ya kujikwamua, hivyo hata nyenzo za matumizi zinazohitajika zitakuwa tofauti na zile za kawaida ktk safari..
Na ili kujiondoa hapo tulipo tunatakiwa kuja na mipango mipya na sii kuanza kulaumiana jinsi gani dereva hakusikia warning zetu. Na wala sii swala la kumtazama na kumzomea dereva, kondakta au fundi isipokuwa hii ni kazi mpya ya kujikwamua toka ktk tope ili tupate kuendelea na safari!..Kujikwamua huko hakuna ujuzi wa mtu mmoja kuendesha gari na wala sii dhamana ya mtu mmoja kwani tusiposaidiana ndio tumelala porini. Na kibaya zaidi Kibongobongo ikishindikana kabisa, madereva wanaweza kutuacha hapo porini wakaenda kulala mahotelini, wewe na mimi tulokwama msituni kazi ipo kwetu.
Na itanishangaza sana ikiwa vijana wa UVCCM watapingana nami hali ni wao waliotuacha mataani kwa kufanya kapeni kubwa ya kumrudisha JK madarakani 2010.. Naweza kabisa kusema UVCCM pamoja na umoja wa Wanawake ndio umecheza turufu kubwa ktk uchaguzi mkuu kuliko hao wazee asilia kila Malecela, Msekwa, Mwinyi na kadhalika..Pale tulipokuwa na nafasi ya kumwondoa JK wao hawakuona lakini ni rahisi leo kwao kuona makosa ya JK baada ya...sijui kama ni kampeni against JK au kweli UVCCM wamepania kufanya mabadiliko kwa manuifaa ya wananchi au ya chama..Hasa pale wanapotaka kuandaa maanadamano nchi za nje..Kwa nini yasifanyike nyumbani, ikiwa mara ya kwanza UVCCM kumpiga vita rais na mwenyekiti wa chama chao..
Sasa turudi ktk maandamano, ningeomba mtu hata mmoja aje hapa aniambie hayo maandamano mnategemea ku accomplish kitu gani? nini malengo ya maandamano hayo na ujumbe gani utakaotawala zaidi ya kuwaonyesha ulimwengu jinsi Ridhwan sijui tajiri na kadhalika. Halafu kibaya zaidi ni kwamba maamndamano haya yanatayarishwa na mtu anayedai kuwa Mwana UVCCM hali hii haijawahi tokea nyumbani hata siku moja UVCCM kufanya maandamano dhidi ya kiongozi wao wenyewe.
Sasa ingekuwa bora zaidi kwa hali zote za kimalengo maandamano haya kufanyika Tanzania kuliko Marekani kwa sababu haijawa utamaduni wa Mtanzania kumpinga rais kwa maandamano nyumbani wakati hapo Marekani maandamano kama haya ni sehemu ya maisha yao ya kila siku.. Naweza kusema kila siku, kila saa kuna maandamano sehemu fulani ya Marekani.. Ni halki ya kimsingi kwa wananchi wake ktk kuufikisha ujumbe wao kwa wahusika iwe serikali, shirika au taasisi yeyote.. Wananchi wana uhuru wa kufanya hivyo hata kama kundi la watu hao wanaona Ufisadi ni haki yao.. Ufisadi sio uhujumu uchumi na wakaandamana kuupamba Ufisadi.
Mwisho mkuu wangu, JK kachagua viongozi woote dhaifu na hatukufanya lolote kupinga chaguzi hizo hata kama analindwa na sheria kwa sababu mawaziri wote na wanasheria wa Mkapa na JK wengi wao walikuwa wakijulikana kwamba hawafai, wana scandals kabla hata hawajachaguliwa..Ni watu wanaojulikana kuendesha ufisadi kabla hawajawa mawaziri lakini tumewapa heshima zote za kitaifa muda wote..Tulitegemea kuvuna kitu gani haswa. Mimi nambieni tu hayo maandamano ya DC tunategemea kufanikisha kipi?.. Kama ni ujumbe jamani CUF wamefanya sana, Chadema wamefanya sana tena hadi mauaji yametokea lakini umesikia nani katusiiliza. mauaji yote toka Bulyanhulu, Pemba, Tarime, Arusha yote yako recorded ktk vyombo vya kimataifa lakini wamefanya nini - NOTHING!!..
Kifupi Kukata mzizi wa fitna dawa ya matatizo yetu ipo kwetu sisi wenyewe na nitasema tena JK ni sehemu ya Matatizo<Soluhisho..akiwa kama rais na Mtanzania..