Maandamano ya Kumpinga JK Washington DC

Maandamano ya Kumpinga JK Washington DC

Status
Not open for further replies.
Wanabodi
Na pengine ningewaomba sana badala ya maandamano mwendeni Washington na agenda ya kumwambia JK achukue jukumu alokabidhiwa na wananchi kuwafikisha mahakamani waharifu wote laa sivyo wananchi watachukua jukumu hilo. hakuna sababu ya kumwadhili, kumkashifu hali yeye ndiye baba wa taifa iwe sifa kwetu...Itisheni mkutano na mumkalie kooni inatosha zaidi ya fikra za kuadhiliana hali sisi wenyewe ndio tulipandisha bar na hatujawahi kuweka cap ktk matatizo yetu..Mwisho wa uwezo wetu ktk kukabili matatizo haujulikani maanake tunapandisha tu bar.

Mkuu hapo penye red hicho kitu kilishafanyika term ya kwanza ya utawala wake. Nilikuwa washington Dc wakati huo and it was wastage of time kwasababu zifuatazo: Wauliza maswali walichaguliwa kabla ya muda hivyo wengine hatukupata nafasi yakuuliza maswali. 2. Maswali yaliyoulizwa hayakulenga moja kwa moja kwa mafisadi , ingawa yalilenga kero za wananchi, raisi hakujibu kitu kinachoeleweka zaidi yakucheka cheka tu. 3. Mahali mkutano ulipofanyika watu walikunywa pombe kabla mkutano haujaanza (nahisi nimapandikizi walifanya hivyo purposely) kwahiyo mkutano ukaonekana vurugu tupu. Why do you believe raisi wa nchi asiyesikiliza watu wake nyumbani even wabunge atawasikiliza watu walioko nje ya nchi? Kwanini raisi wa nchi anatakiwa "akaliwe kooni" kufanya kazi alizochaguliwa purposely kuzifanya? It is his responsibility to do so, miaka karibia sita hii hajifunzi, huo uvumilivu wa Watanzania sasa umepitiliza. Zaidi ya yote amekua anatoa majibu yakebehi yasioonesha kwamba even anajaribu au anajua anafanya nini. Kweli mtu huyu unamvumilia mpaka lini? When is it enough? It is up to DC people to decide, lakini kwahili wazo lako sikubaliani nalo. Najaribu kupima kipi kizito a) raisi kuabikia au b) ndugu zangu wanaokufa kila siku kwa uzembe wake na watendaji wake. Naona kama kuaibika aiibike tu. Kama kukosa wafadhili then let it be afterall hizo pesa za wafadhili hazimsaidii mwananchi wakawaida. Tukumbuke mficha maradhi humuumbua yeye mwenyewe. Tumekuwa tunaficha matatizo yetu lakini yanaendelea kutuumiza. Ni lazima raisi a-act now, hatumuombi, ni wajibu wake kufanya hivyo. Ni lazima tumueleze what we want na tuna mpa muda maalum wakuyatekeleza sio porojo za kuvua gamba nakuongezeana muda. Tumechoshwa na kamati zisizokuwa na tija, kila kitu kinaundiwa kamati watu wanakula tu pesa. Ni lazima tuelewe undani wa tatizo la umeme na nini kinafanyika nasio kusubiri mvua.
 
@Mkandara

Kwanza nitazungumzia haya maandamano ya Washingtona DC, BBinafsi nayaona ni waste of time - I dont think so mate. Maandamano huko WEST hayatazamwi kwa jicho la kupuuza kama huku.
Labda nirudie tena kusema kwamba kwa kila maamuzi tunayoyafanya muhimu zaidi ni kutazama WATU na MAZINGIRA.
wewe umesema Huko west maandamano hawayatazami hivyo? unaelewa unachokisema au unazungumza tu maanake huko west ndiko NAKOISHI..Huku maandamano yanaweza kufanywa na mtu yeyote hupinga kitu chochote na wakati wowote pasipo kuwa big deal kabisa na mara zote maandamano huwa yanapinga kitu fulani na kuonyesha kilicho bora. Unaweza andamana kutetea kuvuta bangi na hata kutembea uchi ni haki yako pia kujieleza...
Kwa mfano unaweza andamana kupinga matumizi ya gari na mafuta ya Petrol kwa kuonyesha nadhara ya gari ktk kuharibu mazingira, hewa, kuleta maradhi na kadhalika..Ni maandamano mabayo hakuna mtu atashtuka nayo ila unatumia haki yako ya kimsingi kujieleza. Sema tu kwa maandamano ya DC hakuna FFU wala mtu kupigwa virungu...
Watanzania wenzangu inabidi tufike mahala tujitazame sisi wenyewe na kujiuliza tunaifanyia nini Nchi yetu - Tunadai good governance, kwa mawazo kwa maneno na kwa vitendo. What else do you want people to do?
Your suggestion: Safu ya washauri Magogoni, wachukilie hili kama changamoto na kuanza haraka kukabiliana na mambo yanayodaiwa na wananchi. Hatua kumi huanza na moja! Wasipuuze kelele za wananchi hata kidogo, wako vijana wengi mno hawana kazi na wala hawajui kesho watakula nini let alone maisha yao yatakuwaje huko mbeleni. Na kwa population ya Tanzania vijana ndio wanaounda sehemu kubwa ya population. Ni vizuri kuchukuwa hatua za haraka....

Umeona basi Your suggestion inarudi kwa serikali na sio wewe utafanya nini zaidi ya kuandamana huko nje ya nchi! kwa nini unashindwa ku suggest kitu cha kufanya wewe kama mwananchi maanake tumelalamika toka Mwinyi, Mkapa na sasa hivi JK.. matatizo ndio yanazidi tu mwaka hadi mwaka.. why is it so special leo wewe unaandamana nchi za nje ili iweje? kwanza ni ikitendo ambacho hakitatambuliwa, hakina mvuto na labda nikwambie tu kwamba wakati wa mikutano ya UN nchi zaidi ya 20 huwa na wananchi wanaoandamana na mabango kuzipinga serikali zao. Hutokea nini zaidi? hakuna lolote unless nchi hiyo ina mahusiano mabaya ya Marekani.

Tazama sasa Marekani baada ya kuona wanashindwa Libya sasa hivi kimyaaa wamegeuza macho yao kuelekea Syria na wanawaacha wananchi vijana waliojitoa mhanga kupigana na Ghadhaff kwenye mataa. Umesikia CNN au BBC hivi karibuni wakiweka nguvu kutangaza habari za kumwondoa Ghadaffi na Libya kama zamani?...Je, umejiuliza kwa nini Marewkani na UK wamejitoa kiulainiii.. Kwa hiyo nachotaka kusema tunapeleka message to the wrong people kwa sababu Marekani na Tanzania hasa utawala wa CCM ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa..


My suggestion:- Wewe na Watanzania woote wenye kutaka mageuzi acheni tabia ya kuruka matatizo. Ni wakati wa kuya face wazungu wanasema take the bull by the horns!...na sio kutegemea Mungu, ipo siku moja sijui tumerogwa na kadhalika. Get up! stand up! Bob katwambia 20+ yrs ago.. simameni ktk mikutano na mwambie JK mbele ya wananchi wenzako kwamba ameshindwa kuongoza nchi... Acheni kuijificha nyuma ya majina bandia kama kweli nyie mnataka kuleta mabadiliko nchini. Simama na wakilisha hoja yako sehemu ambayo una hakika utapata matokeo bora zaidi na sio kuruka viunzi..
 
Wapiganaji wetu Washington DC, BIG UP sana huko wenzetu kuumwa kwenu na mashaibu yetu hapa nyumbani!!!!!!!!!!!!

Hakika mnachokifanya ni sahihi kabisa kwa mujibu wa demokrasia wa kujieleza kusikoridhisha waziwazi. Endeleeni zaidi na zaidi kujulisha ulimwengu UFISADI NA DHULUMA za CCM hadharani na kujitia bidii zaidi kuyukomboa wananchi kuondokana na utumwa wa mawazo na fikra za mwaka wa 47 kama ambavyo hili li-JWAGU linavyotaka kutuaminisha hapa jukwani.

Chonde tuendelee kupeana updates toka huko majuu.


Nyie sio wananzania, mnanunuliwa na kampuni hio ya kitajiri inayodhamini. hatutaki mfe ila kama mnataka mfe andamaneni! mnachokifanya sio cha kitanzania na mlaaniwe na mshindwe kwa jina lililo kuu.
 
Huyu nae vp?watu wengne bwana,soma ujue china imefaidika vp kwa kuwa na idad kubwa ya wananch wake wanaofanya kaz usa,nch kutofaidka n uzembe wa watendaj serikal,kwan safari za kikwete usa hakuona kuwa kuna raia wake wako uko na nch inapaswa kufaidka?
 
Nyie sio wananzania, mnanunuliwa na kampuni hio ya kitajiri inayodhamini. hatutaki mfe ila kama mnataka mfe andamaneni! mnachokifanya sio cha kitanzania na mlaaniwe na mshindwe kwa jina lililo kuu.

Kwani Sin Bin Clair alivyomnunua M k w e r e ina maana yeye sio Mtish?
 
Tutasikia na kuona mengi.Hii issue inaoenekana kuwatoa wengi kutoka huko walipo.Kuna aina flani ya watu kuamshwa na interests kuguswa.Laiti mngekuwa mnashtushwa na uamsikini wetu kama mnavyoshtushwa na hili...Lets wait and c

Mkuu jmushi1, hii ni safari ya karibu 300 toka Kikwete akamate madaraka ya nchi mwaka 2005 !. Kwa hesabu za haraka haraka hizi ni kama safari 50 kwa mwaka sawa na safari 4 kwa mwezi ikiwa na maana anasafiri kila wiki ! Kama kila safari inachukua wastani wa siku 3, ni sawa na kusema katika kila wiki yuko Ikulu tu kwa siku mbili tu kwani siku mbili zingine ni za mapumziko (Jumamosi na Jumapili). Ni wazi hizi safari za Kikwete ni mojawapo katika vitendo vya kifisadi vinavyoifilisi nchi ambavyo lazima vipigwe vita vya ndani na nje kwani kuna siku tutapigwa butwaa tutakapojua zimetugharimu kiasi gani. Nayapa big up maandamano ya kumpinga Kikwete yanayopangwa kufanyika mjini Washington !
 
@Mkandara
wewe umesema Huko west maandamano hawayatazami hivyo? unaelewa unachokisema au unazungumza tu maanake huko west ndiko NAKOISHI.. Mkandara, I know WEST perfectly well and I promise you I also know what I am talking about. Na kwa kukusadia zaidi naelewa a thing or two about the World of Politics & International Diplomacy. On the outside unaweza kuona/kufikiri kuwa maandamano kama haya yatakuwa na 'negligible' difference kwamba the State Department wont notice it. Mazungumzo ya ndani ni tofauti kabisa na public statements. Nguzo kubwa sasa hivi TZ wanashikilia when it comes to USA ni Uranium hata hivyo wamerakani hawatataka kuonekana wanawaacha 'people of Tanzania' on the dark bila kuwapa pipi. Hiyo tactic inaitwa 'social licence'. Wameanza na malaria haikubaliki - kwa hisani ya watu wa marekani, sasa tunapata mpaka viboti vya doria. Na kama kuna somo West wamejifunza kwa haraka ni kutoacha kelele za watu kawaida kama walivyoacha Egpyt. They would like to check each & every claim and meausure any potential threat against thier interests. Kwa sasa hivi wanapataka sana hapa. lets leave it there.


Huku maandamano yanaweza kufanywa na mtu yeyote hupinga kitu chochote na wakati wowote pasipo kuwa big deal kabisa na mara zote maandamano huwa yanapinga kitu fulani na kuonyesha kilicho bora. Unaweza andamana kutetea kuvuta bangi na hata kutembea uchi ni haki yako pia kujieleza... Kwa hiyo unaona malalamiko ya hao watanzania wanaotaka kuandamana yanafanana na hao wanaotaka kuvuta bangi au kutembea uchi? The WEST I know of ni kwamba kila kitu kinakuwa judged on its merit.

Kwa nini unashindwa ku suggest kitu cha kufanya wewe kama mwananchi - Nimeandika washauri wa Rais wafanyie kazi malalamiko ya wananchi. What's wrong with that? Unataka kwa mfano niwakamate watuhumiwa wa EPA niwapeleke KEKO? What excatly do you mean unaposema 'kitu cha kufanya kama mwananchi? Nalipa kodi in exchange those who collects my taxes should deliver. Hakuna umeme na hivi ninavyondika BP ambayo by the way government ni shareholder wamegoma kuuza mafuta! So, kwa maoni yako, nifungue vituo vyote vya BP kwa nguvu? Why do you think we elect leaders? Ili tuweze kuandamana? au kuna vitu wanatakiwa wafanye?

why is it so special leo wewe unaandamana nchi za nje ili iweje? - Wewe uko huko utajuaje? our national balance sheet's gone south - not a dime in the pot!

Wewe na Watanzania woote wenye kutaka mageuzi acheni tabia ya kuruka matatizo. Ni wakati wa kuya face wazungu wanasema take the bull by the horns! - I am my friend - staying 12 a day without power!

Get up! stand up! - how?

simameni ktk mikutano na mwambie JK mbele ya wananchi wenzako kwamba ameshindwa kuongoza nchi... Kumbe wanachoandaa huko Marekani ni nini? Wanaandaa mkutano-maandamo wa kumpea Pdidy au?
 
FJM, Jmushi! na Unstoppable..
Wakuu zangu itanibidi niwajibu kwa ujumla... maanake nimeachwa nyuma zaidi.. Na labda niwajuze tu kuweka mambo sawa ni kwamba hatupo hapa kubishana bali kutafuta the best solution out of this mess!. Unaweza kutokubaliana nami na ukaweka ujumbe wako na jinsi gani unaona ni bora zaidi kuandamana kuliko navyo suggest mimi. Haya ya kusema wewe unajua international diplomacy ni hadithi za elimu ya kupangiwa kwa sababu hakuna kitu kama hicho bila kutanguliza interest zako..

Marekani wanapinga mauaji Syria lakini hawasemi kitu kwa Bahrain..hakuna kitabu wala internbational diplomacy inayoweza kutafsiri hili kwa vitabu..Nakwambia tena mtaonekana wavuta bangi tu... maanadamano Tanzania yana nguvu zaidi ya kuyafanya Marekani tena hamna ushahidi. Na ndivyo kiongozi wa Canada (Harper) alishindwa kutusaidia kuhusu mikataba mibovu ya Barricks. na nchi kibao zime file mashtaka dhidi ya barricks lakini hakuna hata shitaka moja lililopelekwa mahakama za dunia - Anyway nikuache huko...

Leo asubuhi nimeingia Twitter na kuona Mh.Jk kaandika kitu ambacho kilinipa muda wa kufikiri kisha nikachanganya na za kwangu na ndio maana nimekuja na sura tofauti na ile mloizoea..Nimemsoma JK akisema hivi:- Believe in being part of the solution!..

Unajua mkuu haya ni maneno mazito sana ambayo kwa mara ya kwanza nimemsikia JK ameyaandika na ndipo nikajiweka mimi ktk chumba kimoja naye kutafuta solution..How can I be part of the solution ikiwa yeye (kwa mtazamo wangu) ndiye part of the problem to start with..Kisha nikasema well kama yeye ndiye problem what is the best approach maanake maandamano yaliyoandaliwa kisheria na Chadema mikoa yote nchini pekee imepata mushkheri mkubwa na kuleta utengano mkubwa baina yetu kwa Udini ulotoka kuzimuni.. Kwa ujumla wake hayakuweza kuzaa matunda yoyote kwa wananchi zaidi ya kuwapa umaarufu zaidi CDM pamoja na kwamba CDM na viongozi wake wamewekwa ktk picha mbaya ya Ugaidi na kadhalika (ingawa sii hoja kubwa ikiwa CDM wanajua wao sii magaidi)..

Toka tupige makelele sisi wananchi tumewezeshwa kitu gani..Hakuna.. Kisha nikajirudi na kusema wait a minute... JK kweli ndiye mbaya wetu? au sisi wananchi tulomweka madarakani ndio wabaya!.. Kwa nini tumemchagua na how can we defend utawala ambao kwa miaka zaidi ya 50 leo ni asilimia 15 tu ndio wana umeme tena wa mgao, tumezungukwa na maji ya mito na maziwa lakini hatuna maji ya kutosha majumbani, huduma za afya na elimu mbovu, kila kitu ni feki ya Uchina na India lakini bado tunaandamana kwa mabango ya ushabiki wa vyama! - nikasema hapana! - JK sio problem pekee yake bali sisi Wadanganyika ndio tulokuwa Problem na he is part of it!. Nikakumbuka ule usemi wa Field Marshall Es - ya kuwa Viongozi ni reflection yetu!

Maadam sisi wenyewe ndio tumemchagua JK mwaka tu umepita , na wala matatizo haya hayakuanza baada ya uchaguzi huu ila yalikuwepo kabla yake na wakati wake yamezidi (kitu ambacho yeye JK hakioni)..Hivyo kama kuna tatizo basi sisi Watanzania are/have been part of the problem..Na maadam hakuna mtu anayeweza kuja kutuondolea matatizo yetu ni jukumu letu sisi wenyewe kuwa sehemu ya ufumbuzi na sio kutegemea JK, CCM au Marekani.. we have to believe being part of the solution! hakuna cha mtu wa CCM wala CDM hapa ni kutafuta njia moja kwa wote...

I mean toka matatizo ya IPTL, Rada, Meremeta, ndege ya rais ya Mkapa ambayo sijui imefia wapi, Richmond, Bandari, TRA, ATC, Aiports, yote haya ni matatizo yasiyokwisha na tuliyakumbatia kwa ku raise bar ya matatizo yetu kila mwaka.. Tuliweka matumaini ktk ahadi tupu au njia za mkato toka budget zilizopitishwa hadi mwananchi kununua jenerata za umeme na mashine za kuchimba visima vya maji right in the heart of Dar es Salaam.. na hatukuoni dhiki yoyote isipokuwa fahari ya kuonyesha majenereta na matanki ya maji hata kama yalipiga makelele usiku kucha, mchana kutwa..

Vijiweni utawakuta watu wakisifia CCM na utawala wa JK kwa jazba huku matumbo yao hayana kitu.. Ndipo nakuta ya kwamba ni sisi wenyewe ndio tunampa JK wrong impression. Hakuna vipenzi wa JK wanaothubutu kumwambia kwamba mzee wangu unachemsha! mkuu wangu huko unakotupeleka siko isipokuwa huzisikia habari hizi kutoka Chadema ambao kwa imani yake anafikiri wana wivu tu.. na hapa wapambe wake wanamwambia Dr.Slaa na CDM wana wivu hawana lolote kila kitu safi..Kukaa kizani masaa 12 haiwezi kuwa unafanya maamuzi ya busara kutatua matatizo. taking the bull by the horns sio kukubali matokeo na kukaa kizani, ndio maana hunielewi.

Sasa unaweza pinga kwamba kwani huyo JK kama rais haoni hali halisi ya nchi kiasi kwamba yeye afikie kuamini anayoambiwa?.. well kuna watu wangapi Tanzania wanaamini mambo yote ni super, tena wasomi wazuri tu wakidai haya ni matatizo madogo madogo ya mpito ambayo yatapatiwa ufumbuzi soon.. Na hata kama tumeshakula miaka sita na JK lakini tumeshindwa kumaliza hata matatizo ya dharura..

Je, ktk harakati zote Sisi wananchi raia wa nchi hii tumefanikiwa kupiga hatua moja kwa maneno! - HAPANA.. Nchi inazidi kurudi nyuma na haki za wananchi zinazidi kupotea..So mbinu hii haifanyi kazi kwa sababu Mafisadi kina Rostam wanajiuzulu huku wakitucheka, EL hatajivua gamba na tunajua fika hataweza kujivua..acha hawa kuna kundi zima la wahujumu uchumi ambao wanaendeleza ufisadi wa hali ya juu nchini kiasi kwamba imefiia watu kufunga vituo vya mafuta kuiweka nchi mateka na serikali isifanye kitu..Come on now!

Jamani sichochei machafuko na wala sisemi tuingie msituni au kufanya maandamano ya vurugu kama Misri, Tunisia ili kumwondoa JK na CCM isipokuwa nachotaka ni wewe Mtanzania kufikiria njia ya kupambana na adha hizi uso kwa uso kama mlivyoweza kupambana na Vibaka wakati serikali imeshindwa kuwakamata kutokana na rushwa. Vibaka wamekwisha/pungua leo hii askari waliokuwa wakipokea rushwa hawana sehemu ya kuvuta.. Jamani haramu humfuata Mtumiaji! Ufisadi upo nchini kwa sababu sisi wenyewe tunaupenda na kuukumbatia. Viongozi wabovu wapo kwa sababu sisi wenyewe tunawakumbatia..Matendo yote haya na madudu yake yapo kwa sababu tumepoteza kitu kikubwa sana kiitwacho SHERIA na ipo kila sababu ya kuisimamisha upya by all means necessary laa sivyo tunaenda iliko Somalia..
 
Ningekua US NINGEKUWEPO, but i will be there spiritually. Make it happen
 
naunga mkono asilimia mia 100% mandamano ya amani nchini marekani......tumechoshwa na uswaiba urafiki na undugulazeshen serekalini mtoto wake anamiliki mashamba makubwa na moja ja kampuni ya uuzaji mafuta hapa nchini wakati watanzania wanalia njaa hakuna shule hosiptali hakuna madawa .....tunasema tupo teyari kufa ili kizazi chetu kije kuishi kwa rahaaa
 
mcheza sinema mmarekani, amaye pia ameshiriki harakati nyingi atahutubia maandamano yetu. imethibitishwa. wadau njooni kwa wingi
 
ili iweje? mshindwe kwa jina la yesu; msimsumbue muacheni aendelee kutatua matatizo yetu
 
Wakuu zangu itanibidi niwajibu kwa ujumla... maanake nimeachwa nyuma zaidi.. Na labda niwajuze tu kuweka mambo sawa ni kwamba hatupo hapa kubishana bali kutafuta the best solution out of this mess!. Unaweza kutokubaliana nami na ukaweka ujumbe wako na jinsi gani unaona ni bora zaidi kuandamana kuliko navyo suggest mimi. - Kwa nia nzuri kabisa nilitoa maoni yangu kwamba washauri wa Rais waangalie malalamiko ya wananchi na wayapatie ufumbuzi. Maandamano ni kitu cha mbali sana katika safu ya kudai kitu. Watu huwa wanazungumza na kuzungumza ili kupata ufumbuzi wa jambo husika. Lakini ukiona watu wenye akili timamu wanaacha shughuli zao na kuandamana barabarani basi ujue hamko kwenye page moja tena!. Na hapa ndio nasema kuna haja kabisa washauri wakawa wa wazi au niseme wakubali kuwa kuna mambo hayajakaa sawa.

Haya ya kusema wewe unajua international diplomacy ni hadithi za elimu ya kupangiwa kwa sababu hakuna kitu kama hicho bila kutanguliza interest zako.. Sijaipenda hii point hata kidogo Mkandanra na naona kama ina mtazamo hasi kwa watu wanaondamana. Kwamba hao wanaondamana hawana akili na utashi kuamua kifanya hivyo, wameelekezwa na mtu/watu/kikundi fulani kuundamana!. Nadhani ni vizuri uwe kidogo clearer hapa otherwise mtu anaweza kuichukulia hii point kama madharau kwa watanzania wenzako wanaaondamana. Ni ushauri tu ndugu yangu!

Hakuna vipenzi wa JK wanaothubutu kumwambia kwamba mzee wangu unachemsha! mkuu wangu huko unakotupeleka siko - Ni kawaida kuona viongozi wakuu wakibadilisha baadhi ya washauri baada ya muda fulani. Hii ni pamoja na kuhakikisha kuwa wanapata 'fresh ideas na pia kuhakikisha they are not out of touch. Hili ni muhimu sana kulizingatia.
 
FJM, Jmushi! na Unstoppable..
Wakuu zangu itanibidi niwajibu kwa ujumla... ..

Leo asubuhi nimeingia Twitter na kuona Mh.Jk kaandika kitu ambacho kilinipa muda wa kufikiri kisha nikachanganya na za kwangu na ndio maana nimekuja na sura tofauti na ile mloizoea..Nimemsoma JK akisema hivi:-Believe in being part of the solution!..

Unajua mkuu haya ni maneno mazito sana ambayo kwa mara ya kwanza nimemsikia JK ameyaandika na ndipo nikajiweka mimi ktk chumba kimoja naye kutafuta solution..How can I be part of the solution ikiwa yeye (kwa mtazamo wangu) ndiye part of the problem to start with..Kisha nikasema well kama yeye ndiye problem what is the best approach maanake maandamano yaliyoandaliwa kisheria na Chadema mikoa yote nchini pekee imepata mushkheri mkubwa..

napata hasira kuona kiongozi wa nchi anatumia siasa kutatua matatizo sugu ya nchi.
yeye anaposema part of solution kwa tatizo lipi?
kwa hii nchi tatizo lake ni nini?
tatizo lake sio yeye kikwete kuwa mzembe na kufanya ushwahiba hapo ikulu?
sasa tutanaweza je kuwa part of soulution sisi na yeye wakati yeye ndio tatizo
TANZANIA HAINA TATIZO LOLOTE ZAIDI ya kikwete
  • sera tunazo
  • mali ghafu tunazo
  • Ardhi tunayo
  • maliasili tunazo
  • wataalamu wapo
  • technology zipo (siku hizi unaweza kuingia mkataba kutumia technology ya mtu mwingine)
tatizo ni uongozi hasa kikwete na Pinda hawana kila kukicha wanatafuta udanganyifu ila watu watulie wao waendelee kuisha madarakani, naposema kuisha madarakani nina maana hanisha hakuna wanachofanya kama viongozi hawa ni sanamu ya uongozi,
na ndio maana maandamano yanakua njia
sahihi kwa sababu kikwete ni tatizo na anajua yeye ni tatizo ila ni mwenye moyo mgumu kugeuka sasa nchi inaangamia
sio muda kuna makubwa yatatokea hapa nchi kama watu wataendelea kucheka na uongozi wa usanii
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom