Maandamano ya Kumpinga JK Washington DC

Maandamano ya Kumpinga JK Washington DC

Status
Not open for further replies.
Kazi ya Raisi ni Kutafuta Nje! Yaani kuomba omba kina Richmond waje eeh! Mabalozi na waziri husika kazi zao nini Rojeo!
 
Labda mkuu ungenieleza kosa langu ni lipi? wewe umesema humjui, mimi nimekurahisishia umjuwe sasa unaniuliza vipi mimi maswali hayo? kwani wewe huwezi kumuuliza yeye mwenyewe direct? kuna wakati busara kidogo inatosha.

What's your point? Someone is trying to help us solve our problems, the least we can do is welcome them! You dont have to see the glass as half empty all the time.

@ Saigon. Huyu Lisa stori yake naifahamu..lakini hukunielewa maana ya swali langu..je, watanzania wangapi wanamfahamu? Kama uliona nilivyomquote mtoa mada, nadhani husingesema maneno uliyosema!!!

@Seacliff. So if someone is trying to solve our problems, are we supposed to be a** kissers?!? I have a doubt that you have a matonya mentality. no one from outside Tanzania can be able to solve our problems for sure...we are the only ones to solve our problems mazee. Who did solve their problems?! Did we? If no, why then are you willing to welcome them solve our problems?!


 
@ Saigon. Huyu Lisa stori yake naifahamu..lakini hukunielewa maana ya swali langu..je, watanzania wangapi wanamfahamu? Kama uliona nilivyomquote mtoa mada, nadhani husingesema maneno uliyosema!!!

@Seacliff. So if someone is trying to solve our problems, are we supposed to be a** kissers?!? I have a doubt that you have a matonya mentality. no one from outside Tanzania can be able to solve our problems for sure...we are the only ones to solve our problems mazee. Who did solve their problems?! Did we? If no, why then are you willing to welcome them solve our problems?!

mzee hivi vita dhidi ya mafisadi lazima vipiganwe nje na ndani pia..! vipi unakumbuka mazimbu na dakawa/ wapigania uhuru wa africa ya kusini?
kama tuliweza kuwaweka hawa wapigania uhuru wa africa ya kusini hapa ..na kwa kiasi fulani waliweza kuongeza msukumo wa kujikomboa kutoka utawala wa makaburi ,, sioni ni kwanini watanzania walioko nje pamoja na marafiki zao wasijaribu kufanya kitu hichohicho kupigana na ufisadi unaolitafuna taifa letu!! tafakari!
 
@ Saigon. Huyu Lisa stori yake naifahamu..lakini hukunielewa maana ya swali langu..je, watanzania wangapi wanamfahamu? Kama uliona nilivyomquote mtoa mada, nadhani husingesema maneno uliyosema!!!

@Seacliff. So if someone is trying to solve our problems, are we supposed to be a** kissers?!? I have a doubt that you have a matonya mentality. no one from outside Tanzania can be able to solve our problems for sure...we are the only ones to solve our problems mazee. Who did solve their problems?! Did we? If no, why then are you willing to welcome them solve our problems?!
swali dogo...ni kwanini huwa mnachukua misaada mingi kutoka kwa hawa jamaa bila kujiuliza wenyewe wanasaidiwa na nani ila linapokuja suala la wenyewe kutusaidia kupinga ufisadi na uonevu mnauliza maswali mengi sana? .....si unaona serikali yetu ilivyowapotezea waingereza kwenye issue ya radar ..lakini issue ilipofika kwenye mavuno serikali ikaanza kudandia...tafakari!
 
Nyie sio watanzania , nyie ni wamarekani , shughulikieni kwanza matatizo ya uchumi ya nchi yenu. Hamuoni nchi yenu inavyo didimia sasa

Hii mambo ya kutumia Avatar za watu ni issue ..niliposoma hiyo koment nikawaza haaa hivi mheshimiwa Slaa anaweza kuongea hii maneno kweli

lakini baada ya kusoma ktkt ya mistari nimegundua unahitaji kubadili avatar GB
 
Acheni hizo.kwani JK amewafanya nini?Amekuta mfumo mbovu,cha kufanya ni kupambana na mfumo sio mtu kama JK
 
Nyie sio wananzania, mnanunuliwa na kampuni hio ya kitajiri inayodhamini. hatutaki mfe ila kama mnataka mfe andamaneni! mnachokifanya sio cha kitanzania na mlaaniwe na mshindwe kwa jina lililo kuu.
 
Tutasikia na kuona mengi.Hii issue inaoenekana kuwatoa wengi kutoka huko walipo.Kuna aina flani ya watu kuamshwa na interests kuguswa.Laiti mngekuwa mnashtushwa na uamsikini wetu kama mnavyoshtushwa na hili...Lets wait and c
 
Ingekuwa inawezekana mngempopoa japo kwa mayai viza abaki na huo uvundo. Inatia hasira sana Rais wa nchi anashindwa kushughulikia mambo ya msingi yanayohusu wananchi wake na badala yake anabaki kujichekesha na kujipendekeza kwa mafisadi na wezi wa mali za umma pekee
 
Nakwambia hivyo vya kata ni vya zamani, nimekuwekea ushahidi kuwa sasa ni vya kaya, hukupenda? nivipambe nini na huo ndio ukweli? au huupendi? Unanchekesha!

Na UDOM kikiisha kuwa ni chuo kikubwa South of Sahara! si madogo hayo kijana. Na pale kuwa ndio kituo kikubwa cha elearning in East Africa. Soon kijana, hiyo ni ahadi ya Bill Gates, swahiba yake mkubwa JMK.

Aaaahaa!!! Naona nicheke tu inatosha. Tunaongelea mambo ya msingi wewe unatuletea habari za misaada ya Bill Gates, fikra dhaifu sana na tegemezi. Hey madam!! We are talking about Tanzania and its people, exploiting our opportunities and resources, building our capacity and stepping foward as a nation and NOT LIPPING BILL GATES' SOLES FOR A FEW US CENTS, Wake up!! Lakini sio kosa lako ni swala kiakili zaidi, hata Baba wa Taifa Mzee wetu Nyerere amewahi kusema ukiona mtu anaogelea udini, ukabila mwogope kama ukoma. Uko maeneo hayo hauwezi kuongea zaidi ya akili yako kwa lugha nyingine ukiwa mkoma una limited capacity hauwezi kukimbia kama utakavyo labda ukibebwa.
 
Nyie sio wananzania, mnanunuliwa na kampuni hio ya kitajiri inayodhamini. hatutaki mfe ila kama mnataka mfe andamaneni! mnachokifanya sio cha kitanzania na mlaaniwe na mshindwe kwa jina lililo kuu.


Ushindwe wewe na ukimbizi wako, unategemea upendeleo wa mafisadi na serikali legelege. Nyie si ndo mmezoea kununua nua watu hadi kadi za kura za watanzania masikini. Hopeless!!
 
Wanabodi,
Imenibidi kuchukua njia tofauti ya kuufikisha ujumbe wangu kwa wananchi. Na moja ya kazi yangu kubwa itakuwa kupambana na mawazoz ambayo kila siku yanategemea serikali yake itamfanyia nini wakati yeye mwenyewe hafikirii lolote la kuifanyia serikali yake. Haiwezekani ukapewa maisha bora on a silver plate na wala hizi habari za kulalamika tuu haziwezi kutupeleka popote pia maamuzi yoyote yasiyoweza kujenga hayawezi kupongezwa.


Kwanza nitazungumzia haya maandamano ya Washingtona DC, BBinafsi nayaona ni waste of time kwa sababu kinachofanyika ni kutoelewa mahusiano baina ya serikali ya Marekani na Tanzania na nini msimamo wa Marekani kuhusiana na Tanzania. Maandamano kama haya ni sawa na Palestine waandamane dhidi ya Israel ingawa case hazifanani.

Pili wakati mwingine tunapopanga jambo la kufanya ni vizuri pia kutazama athari zinazoweza kujitokeza. Tusiwe kama waaarabu ambao wanaona haki yao kujitoa mhanga na kujilipua mabomu nchi za watu ili kupelekea ujumbe unaohusu nchi zao. Na matokeo yake ndio wanaitwa Terrorist na hakuna tafsiri nyingine ya kuwapongeza hata kidogo.

Hivyo tupo ktk wakati wa kujaribu kujenga mahusiano baina ya Watanzania wa ndani na nje hivyo kufanya maandamano haya DC sidhani kaa yataweza kutusaidia zaidi ya kuonyesha utovu wa heshima kwa rais ambaye ni mwaka jana tu amechaguliwa na wananchi walio wengi tena basi yawezekana wote mnaoandamana hamkupiga hata kura..

Kitu kimoja tu ni kwamba wakati nchi za wenzetu hu raise bar ktk mafanikio sisi hupandisha bar ktk matatizo. Ni sawa maamuzi ya kuruka matatizo kila bar inavyopanda ndivyo tunavyipanga kuyaruka utafikiri mashindano ya kuruka juu..Sasa cha ajabu tulifika mahala ambapo ndio mwisho wa uwezo wa binadamu kuvumilia matatizo. Kama ni kuruka basi tulifikisha bar kwenye mita tatu ambapo hakuna binadamu anaweza kuruka kwa nguvu zake mwenyewe..Watanzania ndio kwanza tukatafuta njia ya kuruka juu na mti (polls)..

Ni wazuri sana wa kutafuta njia za kukabiliana na matatizo hivyo sasa hivi kila mtu anaruka na mti matatizo na kwa bahati mbaya upande wa pili hakuna confort thing cha kuangukia kama godoro.. Kila siku wanakufa watu, wanavunjika mbavu, miguu na kadhalika kutokana na matatizo haya ya kuruka highjump na miti bila kujua upande wapili hakuna sehemu nzuri ya kutua..isipokuwa sisi Wadanganyika tunachokiona n urefu wa bar ya matatizo na tutaweza vipi kuruka matatizo hayo kwenda upande wa pili..


This is not good, Watanzania wenzangu inabidi tufike mahala tujitazame sisi wenyewe na kujiuliza tunaifanyia nini Nchi yetu. Kama wewe ni fisadi ama jirani yako ni fisadi basi tuchukue maamuzi magumu..nakumbuka wizi wa vibaka nchini umepungua sii kutokana na ukali wa sheria ya serikali bali maamuzi ya wananchi wenyewe kuhakikisha wizi wa vibaka unakwisha. Watu walifikia kuchukua madaraka mikononi mwao wakiwashika vibaka huwachoma moto.. siombei hili na wala silipongezi isipokuwa mahala ambapo serikali ilishindwa wananchi walichukua maamuzi magumu.. Leo hii vibaka wamepungua, mtu unaweza kwenda kariakoo na pochi lako mfukoni ukakatiza mitaa ya Kongo na chain ya dhahabu..

haya yote hayakuwa maamuzi ya serikali isipokuwa wananchi wenyewe kukomesha wizi na karaha za vibaka. sasa basi imefika mahala Ufisadi umekuwa sugu na hauwezi kupatiwa dawa na serikali. wananchi wenyewe chukueni jukumu la kuwafuata Mafisadi na kuwaambia ACHA unachokifanya!.. Kama kiongozi wa serikali mwambieni ACHA UFISADI au laa wananchi tunachukua jukumu wenyewe...

Na pengine ningewaomba sana badala ya maandamano mwendeni Washington na agenda ya kumwambia JK achukue jukumu alokabidhiwa na wananchi kuwafikisha mahakamani waharifu wote laa sivyo wananchi watachukua jukumu hilo. hakuna sababu ya kumwadhili, kumkashifu hali yeye ndiye baba wa taifa iwe sifa kwetu...Itisheni mkutano na mumkalie kooni inatosha zaidi ya fikra za kuadhiliana hali sisi wenyewe ndio tulipandisha bar na hatujawahi kuweka cap ktk matatizo yetu..Mwisho wa uwezo wetu ktk kukabili matatizo haujulikani maanake tunapandisha tu bar.
 
Sasa Nyerere kama sio mdini kwanini anapigiwa debe awe mtakatifu? ana utakatifu upi? mtu aliyetesa watu bila mfano.


My God!!! What a nonsense head!! "Sasa Nyerere kama sio mdini kwanini anapigiwa debe awe mtakatifu? ana utakatifu upi?" .. This is purely a catholic denominational principal, na ni dhehebu la Roman pekee lenye utaratibu wao huo wa kuwatangaza watu watakatifu, hii ni kanuni yao na sio kwamba Nyerere ndo wakwanza kufanyiwa mchakato kama huo, na si lazima mtu atangazwe Mtakatifu ndio maana kuna mchakato na una vigezo vyake. Lakini kilichonisikitisha zaidi ni jinsi unavyojidhihirisha dhaifu mno kiufahamu japo haounekani hivyo kwa nje. Hivi hili swala la utaratibu wa Waroma kuamua kumtanganza mtu wao mtakatifu linahusiana vipi ni udini unaousema. Kama wangekuwa na mamlaka ya kutangaza yeyote yule awe mwislam, msabato, mlokole, mlutheran, mwanglican n.k hapo tungesema kuna udini lakini wanahusika na watu wao tu kwa utaratibu waliojiwekea na wala hawaitaji serikali kulitambua kikatiba au kwa sheria yoyote ile, sasa hapo kuna udini gani. Nimesha kwambia unatuchosha kukufundisha a, e, i, o,u. Epu kazana kidogo basi angalau tuanze na Baba, Mama, Dada, vinginevyo utadumaa.
 
Kwanza nitazungumzia haya maandamano ya Washingtona DC, BBinafsi nayaona ni waste of time kwa sababu kinachofanyika ni kutoelewa mahusiano baina ya serikali ya Marekani na Tanzania na nini msimamo wa Marekani kuhusiana na Tanzania. Maandamano kama haya ni sawa na Palestine waandamane dhidi ya Israel ingawa case hazifanani.


.

Shukran mkuu umeona hilo.. tumejaribu kuwaambia ... lakini hawaelewi .. jibu wanalokupa "UMETUMWA WEYE"
 
This is one of the strongest message and we support u guys, this is expressing ourselves, wasting time ?! Noooo way, I think JK will park it and not travel
 
@Mkandara

Kwanza nitazungumzia haya maandamano ya Washingtona DC, BBinafsi nayaona ni waste of time - I dont think so mate. Maandamano huko WEST hayatazamwi kwa jicho la kupuuza kama huku.

Watanzania wenzangu inabidi tufike mahala tujitazame sisi wenyewe na kujiuliza tunaifanyia nini Nchi yetu - Tunadai good governance, kwa mawazo kwa maneno na kwa vitendo. What else do you want people to do?

My suggestion: Safu ya washauri Magogoni, wachukilie hili kama changamoto na kuanza haraka kukabiliana na mambo yanayodaiwa na wananchi. Hatua kumi huanza na moja! Wasipuuze kelele za wananchi hata kidogo, wako vijana wengi mno hawana kazi na wala hawajui kesho watakula nini let alone maisha yao yatakuwaje huko mbeleni. Na kwa population ya Tanzania vijana ndio wanaounda sehemu kubwa ya population. Ni vizuri kuchukuwa hatua za haraka.
 
Mining Company zote za Tanzania ni za Wamarekani!
Marekani urafiki wake ni wa Maslahi Tanzania ni shamba lake la kuvuna, endeleeni kujidanganya na porojo zenu
 
Wanabodi,
Imenibidi kuchukua njia tofauti ya kuufikisha ujumbe wangu kwa wananchi. Na moja ya kazi yangu kubwa itakuwa kupambana na mawazoz ambayo kila siku yanategemea serikali yake itamfanyia nini wakati yeye mwenyewe hafikirii lolote la kuifanyia serikali yake. Haiwezekani ukapewa maisha bora on a silver plate na wala hizi habari za kulalamika tuu haziwezi kutupeleka popote pia maamuzi yoyote yasiyoweza kujenga hayawezi kupongezwa.


Kwanza nitazungumzia haya maandamano ya Washingtona DC, BBinafsi nayaona ni waste of time kwa sababu kinachofanyika ni kutoelewa mahusiano baina ya serikali ya Marekani na Tanzania na nini msimamo wa Marekani kuhusiana na Tanzania. Maandamano kama haya ni sawa na Palestine waandamane dhidi ya Israel ingawa case hazifanani.

Pili wakati mwingine tunapopanga jambo la kufanya ni vizuri pia kutazama athari zinazoweza kujitokeza. Tusiwe kama waaarabu ambao wanaona haki yao kujitoa mhanga na kujilipua mabomu nchi za watu ili kupelekea ujumbe unaohusu nchi zao. Na matokeo yake ndio wanaitwa Terrorist na hakuna tafsiri nyingine ya kuwapongeza hata kidogo.

Hivyo tupo ktk wakati wa kujaribu kujenga mahusiano baina ya Watanzania wa ndani na nje hivyo kufanya maandamano haya DC sidhani kaa yataweza kutusaidia zaidi ya kuonyesha utovu wa heshima kwa rais ambaye ni mwaka jana tu amechaguliwa na wananchi walio wengi tena basi yawezekana wote mnaoandamana hamkupiga hata kura..

Kitu kimoja tu ni kwamba wakati nchi za wenzetu hu raise bar ktk mafanikio sisi hupandisha bar ktk matatizo. Ni sawa maamuzi ya kuruka matatizo kila bar inavyopanda ndivyo tunavyipanga kuyaruka utafikiri mashindano ya kuruka juu..Sasa cha ajabu tulifika mahala ambapo ndio mwisho wa uwezo wa binadamu kuvumilia matatizo. Kama ni kuruka basi tulifikisha bar kwenye mita tatu ambapo hakuna binadamu anaweza kuruka kwa nguvu zake mwenyewe..Watanzania ndio kwanza tukatafuta njia ya kuruka juu na mti (polls)..

Ni wazuri sana wa kutafuta njia za kukabiliana na matatizo hivyo sasa hivi kila mtu anaruka na mti matatizo na kwa bahati mbaya upande wa pili hakuna confort ya kuangukia godolo.. Kila siku wanakufa, wanavunjika mbavu, miguu na kadhalika kutokana na matatizo haya ya kuruka highjump na miti bila kujua upande wapili hakuna sehemu nzuri ya kutua..isipokuwa sisi Wadanganyika tunachokiona n urefu wa bar ya matatizo na tutaweza vipi kuruka matatizo hayo kwenda upande wa pili..


This is not good, Watanzania wenzangu inabidi tufike mahala tujitazame sisi wenyewe na kujiuliza tunaifanyia nini Nchi yetu. Kama wewe ni fisadi ama jirani yako ni fisadi basi tuchukue maamuzi magumu..nakumbuka wizi wa vibaka nchini umepungua sii kutokana na ukali wa sheria ya serikali bali maamuzi ya wananchi wenyewe kuhakikisha wizi wa vibaka unakwisha. Watu walifikia kuchukua madaraka mikononi mwao wakiwashika vibaka huwachoma moto.. siombei hili na wala silipongezi isipokuwa mahala ambapo serikali ilishindwa wananchi walichukua maamuzi magumu.. Leo hii vibaka wamepungua, mtu unaweza kwenda kariakoo na pochi lako mfukoni ukakatiza mitaa ya Kongo na chain ya dhahabu..

haya yote hayakuwa maamuzi ya serikali isipokuwa wananchi wenyewe kukomesha wizi na karaha za vibaka. sasa basi imefika mahala Ufisadi umekuwa sugu na hauwezi kupatiwa dawa na serikali. wananchi wenyewe chukueni jukumu la kuwafuata Mafisadi na kuwaambia ACHA unachokifanya!.. Kama kiongozi wa serikali mwambieni ACHA UFISADI au laa wananchi tunachukua jukumu wenyewe...

Na pengine ningewaomba sana badala ya maandamano mwendeni Washington na agenda ya kumwambia JK achukue jukumu alokabidhiwa na wananchi kuwafikisha mahakamani waharifu wote laa sivyo wananchi watachukua jukumu hilo. hakuna sababu ya kumwadhili, kumkashifu hali yeye ndiye baba wa taifa iwe sifa kwetu...Itisheni mkutano na mumkalie kooni inatosha zaidi ya fikra za kuadhiliana hali sisi wenyewe ndio tulipandisha bar na hatujawahi kuweka cap ktk matatizo yetu..Mwisho wa uwezo wetu ktk kukabili matatizo haujulikani maanake tunapandisha tu bar.
Ndugu yangu Mzee Mkandara,heshma mbele.Nimeipenda post yako hii,(zingatia bold)lakini sikubaliani na mengi ulioyasema ili kujustify shinikizo ama hoja kwamba wenye mwelekeo wa maandamano waache kufanya hivyo.

Pengine kuna sababu nyingine(nadhani zipo)nzito kidogo zaidi,hata hivyo bado zinaweza kuwa disputable.Hilo la kudhalilishwa first off sikubaliani nalo.

Kama serikali ina mamlaka na mihimili kama mahakama,polisi na bunge.Basi ni lazima yawepo maswali pale inapokuja kutokuwajibika ama kutokuwajibishwa kwa wahujumu uchumi na mafisadi kwa ujumla.Wananachi walioko Tanzania wana shida nyingi sana na pia zinapelekea wao kuwa wepesi wa kusahau.

Kwa upande mwingine,wameshaona kuwa kama habari za magazeti ni soap opera.Kashfa za ufisadi zikija wanapiga tu domo na muda si mrefu werevu (mafisadi)wanaowajuwa wana tune to a diffrent music.(idara ya habari imetekwa).Unasikia story inabadilishwa na wadaganyika wanajump on to the band wagon.Humu ndani tunatakiwa tuwe tofauti.

Mtanzania ambaye amekuwa exposed ie walioko nje ni tofauti sana na wale ambao hawakufanya hivyo.(wanaorudi na kutowajali wananchi wana mioyo ya ajabu)Kwa namna dunia ilivyo kwasasa,mawasiliano yamekuwa rahisi sana,mfano ni tweeter,FB,na hata hii JF.Walioko nje hata kama hawajarudi nyumbani siku za karibuni,bado wanawasiliana na ndugu zao kwa karibu sana na wanahisi kama na wao wako huko kwasababu ni familia.Wanaelezwa shida dada zao,mama zao,shangazi zao,wajomba zao nk wanazopitia kila kukicha kuanzia umeme,mafuta usafiri nk,matatizo ni mengi,achilia mbali wasiojuwa watakula nini siku inayofuata.And so therefore they symphathise with fellow Tanzanians ie family members na hata citizens kwa ujumla.

Serikali kwa upande wake ni ya kulaumiwa badala ya kuwalaumu wananchi kwasababu ina vitendea kazi vya kulishugulikia hili suala.Laiti kama wangetumia nguvu za jeshi la polisi kuwakamata mafisadi badala ya kuuwa raia wasiokuwa na hatia na kujaribu kuwatisha wenye kuibua ufisadi.Laiti kama jeshi la wananchi/jeshi la kujenga Taifa wangekuwa wanashughulishwa na ujenzi wa Taifa kama infrastructures ie madaraja,road constructions nk,na si wenye vyeo vya juu kula mishahara baada ya kupelekwa nje vitani ama MEREMETA.Laiti kama mahakama hizo zingewahukumu mafisadi kwa haki.Laiti kama taasisi ya kuzuia rushwa ingekuwa inafanya kazi yake kiukweli badala ya usanii tunaouona.Laiti kama wabunge wa magamba wangeacha kulala bungeni na kuamka kuendelea kulipwa.Ama kutetea hoja bila kujali maslahi ya Taifa.Hayo si utumishi wa umma.Na rais yuko kimya,tunasikia yeye anasafiri tu.Laiti kama bunge hilo lingekuwa linatumika kupitisha mikataba yenye tija kwa Taifa...What is our priorities?Najiuliza kila mara,what would it take for them to listen?Hilo ndilo la kujuliza.

Unless uniwekee sababu nzito za kuwapinga wenye kutaka kuandamana.Basi ndipo nitakubalina na wewe mkuu.

Nantanguliza shukran,na pia nategemea kuendelea na mjadala huu mzito ambao unaonekana umeamsha wengi.
Pia nakubaliana na pendekezo kuwa apelekewe agenda ya kuchukua jukumu alilokabidhiwa na wananchi kuwapelekea watuhumuiwa wa ufisadi mahakamani.However hilo lingekuwa la maana kama kungeonekana dalili za yeye kuwashughulikia.

Nionavyo mimi ni michanga ya macho tu every now and then.Tulijadili sana humu kuhusu EPA nk,hadi sasa naona usanii tu na hatujui kiasi kilichorudishwa na ni wapi pesa hizo zinatumika,je ni kwa manufa ya wananchi kama alivyo ahidi?Kama ni kweli hataki kudhalilishwa(mana maisha ya watanzania wengi ni ya kiudhalilishaji)Basi kabla hajatia timu ajibu maswali akiwa huko huko,then ninaweza kuunga mkono hatua ya tofauti na agenda za tofauti,shida ninayoona mimi hapa ni kwamba wananchi hawasikilizwi.
 
Mining Company zote za Tanzania ni za Wamarekani!
Marekani urafiki wake ni wa Maslahi Tanzania ni shamba lake la kuvuna, endeleeni kujidanganya na porojo zenu

Sasa wewe unataka kutuambia nini? Aliyewamilikisha hao wamarekani hizo dhahabu zetu si huyu Baba yenu Kikwete? Au hujui siri ya George Bush kuja kukaa hapa Tanzania kwa siku nne kitu amabacho si cha kawaida kwa Rais wa Marekani hasa wa Republican, Huyo Kipenzi chenu JK akikaa miezi miwili bila kwenda Marekani anasikia kizungu zungu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom