Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,606
- 29,754
Ukweli usemwe
Mwalimu Julias Kambarage Nyerere aliwahi kusema kuwa katika uongozi wake yapo mambo mazuri alifanya na pia yapo ya kipuuzi ambayo alifanya. Akaendelea kusema anashangaa wanaomfuatia wanayaacha yenye tija na kuendeleza yale mabaya yake.
Katika mambo ya kipuuzi aliyoyafanya mojawapo ni lile la kuipeleka nchi kwenye Umoja wa nchi huru za Afrika (OAU) ambayo sasa inaitwa Umoja wa Afrika (AU) bila kuzingatia utashi na maamuzi ya wananchi.
Ikumbukwe kipindi hiko, Mwalimu alikuwa anaungwa mkono hata na watoto wadogo hivyo angepeleka jambo la kujiunga na jumuia za kikanda wangepiga kura na kumbukumbu ingebaki. Lakini maamuzi yake aliyoyafanya kwa niaba ya Taifa zima hayakuzingatia utashi wa nchi na kiukweli hata Katiba yetu hairuhusu jambo hilo. Katiba ipo kimya kama ilivyonyamazishwa na waliyoiandika.
Sambamba na hilo, uamuzi wa kuunganisha Tanganyika na Zanzibar ni mufilis endapo utaratibu haukufuatwa. Sidhani kama wananchi enzi hizo waliulizwa na kuridhia kupitia kura kabla ya Nyerere na Karume kuungana. Leo tuna muungano unaolindwa kwa mtutu wa bunduki na wizi wa kura. Muungano ambao viongozi wanaapa kuulinda kwa sababu una maslahi kwao na si kwa wananchi.
NINI KIFANYIKE
Mzee wa Msoga aliwahi kusema kwenye kikao cha wakuu wa nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki kuwa, kabla ya kupata Rais mmoja wa Jumhiya ni sharti wananchi waulizwe kwanza.
Pamoja na mapungufu kadha wa kadha yanayozungumzwa dhidi ya JK, lakini hili la kurudi kwa wananchi kupata ridhaa ni jambo ambalo hakuna rais wa Afrila aliwahi siyo kusema tu, bali hata kuliwaza.
Nashauri, serikali ianze mchakato wa kura za maoni kuhusu sisi kujiunga jumuiya zote za kikanda yaani
AU (African Union)
SADC (Southern African Developing Countries)
EAC (East African Comunity)
ADB
OIC (YKWIM)
Na zingine ambazo wametupeleka huko kama misukule.
Bunge lisitumike kama mhuri wa kufanya maamuzi yanayohitaji utashi wa wananchi ambao ndiyo wenye nchi
Kinyume na hapo, hizo jumuiya zina manufaa makubwa kwa viongozi badala ya kunufaisha nchi.
CC: Gwappo Mwakatobe FaizaFoxy zitto junior Pascal Mayalla Erythrocyte Mzee Kigogo Retired raraa reree Extrovert Mdude_Nyagali Depal Mamndenyi Joannah Mzee Mwanakijiji funzadume Mshana Jr Bujibuji Simba Nyamaume
Mwalimu Julias Kambarage Nyerere aliwahi kusema kuwa katika uongozi wake yapo mambo mazuri alifanya na pia yapo ya kipuuzi ambayo alifanya. Akaendelea kusema anashangaa wanaomfuatia wanayaacha yenye tija na kuendeleza yale mabaya yake.
Katika mambo ya kipuuzi aliyoyafanya mojawapo ni lile la kuipeleka nchi kwenye Umoja wa nchi huru za Afrika (OAU) ambayo sasa inaitwa Umoja wa Afrika (AU) bila kuzingatia utashi na maamuzi ya wananchi.
Ikumbukwe kipindi hiko, Mwalimu alikuwa anaungwa mkono hata na watoto wadogo hivyo angepeleka jambo la kujiunga na jumuia za kikanda wangepiga kura na kumbukumbu ingebaki. Lakini maamuzi yake aliyoyafanya kwa niaba ya Taifa zima hayakuzingatia utashi wa nchi na kiukweli hata Katiba yetu hairuhusu jambo hilo. Katiba ipo kimya kama ilivyonyamazishwa na waliyoiandika.
Sambamba na hilo, uamuzi wa kuunganisha Tanganyika na Zanzibar ni mufilis endapo utaratibu haukufuatwa. Sidhani kama wananchi enzi hizo waliulizwa na kuridhia kupitia kura kabla ya Nyerere na Karume kuungana. Leo tuna muungano unaolindwa kwa mtutu wa bunduki na wizi wa kura. Muungano ambao viongozi wanaapa kuulinda kwa sababu una maslahi kwao na si kwa wananchi.
NINI KIFANYIKE
Mzee wa Msoga aliwahi kusema kwenye kikao cha wakuu wa nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki kuwa, kabla ya kupata Rais mmoja wa Jumhiya ni sharti wananchi waulizwe kwanza.
Pamoja na mapungufu kadha wa kadha yanayozungumzwa dhidi ya JK, lakini hili la kurudi kwa wananchi kupata ridhaa ni jambo ambalo hakuna rais wa Afrila aliwahi siyo kusema tu, bali hata kuliwaza.
Nashauri, serikali ianze mchakato wa kura za maoni kuhusu sisi kujiunga jumuiya zote za kikanda yaani
AU (African Union)
SADC (Southern African Developing Countries)
EAC (East African Comunity)
ADB
OIC (YKWIM)
Na zingine ambazo wametupeleka huko kama misukule.
Bunge lisitumike kama mhuri wa kufanya maamuzi yanayohitaji utashi wa wananchi ambao ndiyo wenye nchi
Kinyume na hapo, hizo jumuiya zina manufaa makubwa kwa viongozi badala ya kunufaisha nchi.
CC: Gwappo Mwakatobe FaizaFoxy zitto junior Pascal Mayalla Erythrocyte Mzee Kigogo Retired raraa reree Extrovert Mdude_Nyagali Depal Mamndenyi Joannah Mzee Mwanakijiji funzadume Mshana Jr Bujibuji Simba Nyamaume