Maafisa Polisi wawanyanyasa Waandishi wa Habari waliokuwa wakiripoti maandamano katika makaburi ya Langata

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Jul 24, 2021
576
1,625

Tukio hilo limetokea wakati waandishi wa habari wakirekodi tukio la wafanyakazi wa makaburi ya Langata kugoma wakilalamika kucheleweshewa mishahara yao, ambapo polisi waliwataka waandishi wa habari waondoke kutoka eneo la tukio.

Shughuli za mazishi zilisitishwa katika makaburi hayo, baada yawafanyakazi hao kugoma sababu ya kutolipwa mishara yao ya miezi 5.

Afisa wa polisi wa kike aliyerekodiwa kwenye tukio hilo akiwanyanyasa waandishi hao kwa kuwasukuma mwandishi na mpiga picha wakiwa wanaripoti tukio hilo amekosolewa vikali na Wakenya.

Mmoja wa wandishi wa habari aliyefanyiwa tukio hilo kutoka Citizen TV, Mary Mouki amesema tofauti kati ya polisi na wao ilizuka baada ya waandishi wa habari kuhoji hatua ya polisi kurusha mabomu ya machozi kwa waombolezaji ambapo wawili walijeruhiwa katika tukio hilo.

Citizen TV
 
Hao ni polisi wangapi waliohusika na tukio hilo, hadi uanze kuhoji demokrasia? Bado Kenya demokrasia iko juu sana kuliko hapa kwetu ambapo hata ukiimba tu unashughulikiwa!
 
Back
Top Bottom