Lwakatare afutiwa mashtaka ya Ugaidi

Lwakatare afutiwa mashtaka ya Ugaidi

mnatakakuendelea na matamko,maendamano,migomo,sumu,kugawa namba za watu, wizi wa wake za watu,matumizi mabaya ya ruzuku na misuguano isiyoisha .r.i.p.chadema

WALLAH leo umedata kimtindo.
 
Mahakama Kuu ya Tanzania imefuta mashtaka yote ya ugaidi yaliyokuwa yanamkabili Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa CHADEMA Wilfed Lwakatare.

Taarifa kutoka Mahakama Kuu zinasema Mahakama Kuu imebakiza shitaka moja tu, la utekaji ambalo kimsingi ni Jinai na lina dhamana.

Taarifa zaidi zinasema ni shangwe kuu kutoka kwa wafuasi wa CHADEMA walioko mahakamani na Familia ya Lwakatare.Baadhi ya wafuasi wa CHADEMA waliohojiwa wamesema huu ni ushindi mkubwa dhidi ya udhalimu.

Mwanafamilia mmoja wa Lwakatare huku akibubujikwa machozi akasema mkono wa Mungu umeonekana dhidi ya shetani mtoa roho za watu.

Katika kesi hii Lwakatare anawakilishwa na Jopo la mawakili nguli watano ambao ni Mabere Marando,Tundu Lissu,Professor Abdallah Safari,Peter Kibatala na Naronyo Kicheere.

kuitana magaidi,sijui chama cha magaidi na propaganda mfu nyingine kama hizo kutakimaliza ccm ambacho kinakufa taratibu kabla ya wakati wake,uzushi uzushi tu na siasa za majitaka bila kujibu hoja za msingi za kwani tuko hapa tulipo kwa miaka zaidi ya 50 ya uhuru na kuigeuza cdm ndio hoja yao au ndio tatizo linalowakabili watanzania kunatuongezea umaarufu na kuzidi kuwachinjia wao baharini.
 
Hivi kale ka-ushahidi kedekede ka mbinguni from Mwigulu hakakufikishwa mbele ya jaji? Yaani mtu kutoka povu lote bungeni na viapo juu bado jaji anakuona b.w.e.g.e....duh. Mwigulu, kale ka-treni kwa kwenda mbinguni bado hakajaondoka bado, bado una nafasi ya kudandia lifti ukatoe kale ka-ushahidi dhidi ya Lwakatare.
 
Tumeiona video lwakatare akipanga ugaidi, akipanga kulisha mtu sumu, akipanga kumteka mtu..hasafishiki yule ni gaidi tu
 
Hizi mahakama siku hizi hovyo kabisa, hazitendi haki ikaonekana imetendeka..wanahongwa vipesa kidogo tu hoi
 
Hii ni sawa kugeuza karatasi upande wa pili, ambapo rangi inabaki ile ile
 
Tatizo la Proffesionals ( DPP ) Kufanya kazi kwa kufuata Ngoma za Wanasiasa mwisho wake ni aibu
 
Duh pole sana Ben Saanane natumaini utapata nufuu na kupona haraka lakini pia usijekuta neno la Rais mtarajiwa toka Kigoma lishaanza kufanyakazi.
Asante sana mkuu Ngongo.Mwenyezi Mungu anaendelea kuniponya,yeye ni Mungu wa rehema.
 
Last edited by a moderator:
Mungu mwema kwa watakatifu kama Lwakatare..Ludovick sijui akaishi wapi.kama si watu kumuua na mapanga basi ni kumroga kwa waganga.
 
Lwakatare amefutiwa mashitaka yote ya ugaiidi na judge wa mahakama kuu.
Amebakiwa na shitaka moja tu linalohusu madai.

Mimi naona sasa hii serikali inaenda pabaya,kwan huwa inapenda kuchafua wanasiasa kwa kuwapeleka kotini huku wakijua hasa hawatashinda na hawana ushaidi wowote!!na kinachendelea nikulipa watu gharama za kesi tu zinazoanzia mamilion!!najiuliza huu mfuko wakulipa washindi wa kessy zinatoka wapi??mifukoni mwao au benki ya tanzania ambayo ni kodi ya mwananchi kwa ajili ya maendeleo ya nchi?

nachowashauri wajue Tanza ya sasa siyo ile ya miaka iliyopita ya kusikiliza redio kwa mjumbe!!tumechoka na habari zao!hamna jipya kila siku maneno yaleyale!:angry:
 
Hizi mahakama siku hizi hovyo kabisa, hazitendi haki ikaonekana imetendeka..wanahongwa vipesa kidogo tu hoi

mahakama ni nzuri pale inapotenda haki kwa ccm na propoganda zake.
 
Back
Top Bottom