Luhanjo atoa ripoti, Jairo arudishwa kazini

Luhanjo atoa ripoti, Jairo arudishwa kazini

Eti hela jamaa kachukua kweli, tena nyingi kweli, nusu ya makisio.
Ila kwakua tumekosea amount contributed, hakuna kesi
 
Eye 4 an Eye!

Sina shaka kwa sasa nchi haitawaliki JK jiuzulu sasa na PM chukua nchi ndio maana hata Prof. Ndosya ameamua kuumwa tu kwani hapa hatuna kiongozi!
 
The nice part about being a pessimist is that you are constantly being either proven right or pleasantly surprised.
Nilikua natarajia hili litatokea.

Sijastushwa hata kidogo.
Mnaotarajia miujiza itokee kwenye hii serikali ya CCM ngojeni.
 
Kusema ukweli inauma sana,
Wanajua hatutawafanya lolote,
Tumeona wa-tz wote ni kama "wangese" tu, nasi tuko kimya!!
 
Hongera Rais Luhanjo!

Nashangaa kama kweli wewe ndie ulikuwa unafundisha QM pale IFM part time unashindwa kuchua hata ukichota senti moja ya sirikali ni crime!

Huyu Rais Luhanjo ndiye alisababisha hata Katibu Mkuu Pamba afukuzwe kazi kutokana majungu ya Luhanjo ili mama Nyoni apate Ukatibu Mkuu pale Maliasili bado JK ameshindwa kuona huyu babu Luhanjo hafai katika maongozi kama rais kivuli!
 
CAG alikuwa anachunguza kukusanywa kwa izo bil moja au kuwepo kwa tuhuma za rushwa au uwepo wa barua ya kuomba mlungula wa kupitisha bajeti.

Manake Luhanjo anasema hana hatia na anasema watachunguza nani kaitoa iyo barua! Naona apa wanataka kumtisha mama shelukindo sijui?

Na akaongezea ati Jairo anaweza fungua kesi ya defarmation
Kwa upeo wangu mdogo nilidhani watachunguza uwepo wa iyo barua na matumizi ya izo ela so far!
 
Luhanjo anasema tuhuma zilikuwa za uwongo - Ina maana hakuna mchango wowote uliofanywa chini ya maagizo ya Jairo?

Anasema taasisi za Wizara hazizidi 7 na si zaidi ya 20 kama ilivyodaiwa - Hata kama ni taasisi moja je ni halali kuchanga?

Taasisi nne tu ndizo zilizochangia na zilichanga karibu TZS 500mil na si zaidi ya 1bil kama ilivyodaiwa - again ni halali kuchangisha?

REA walichangia 50mil;TANESCO walichangia 40mil; Idara ya Uhasibu ya Wizara ilitoa 150mil; Idara ya mipango ya Wizara ilitoa 278mil - za nini hizi hela? Hivi hizi Idara zilisafirisha watendaji wake wenyewe? Wameangalia kwenye vitabu vya mahesabu kwenye hizi idara?

Mwisho, loosers & winners- CCM wakiongozwa na Beatrice Shellukindo again emerges has the biggest looser in this na kuanzia sasa huyu mwanamama ataonekana kama mama chaumbea (for better for worse). As for the winner - Mr Megawatts a.k.a Ngeleja anaweza kupumua japo kwa muda kidogo maana 3 weeks ago he is looking like a dead man walking.

Hoja kwamba huu ni mchezo wa kuwapumbaza wananchi na kuzima makali ya upinzani sio sahihi kwa sababu hata kama huu mchezo ulikuwa umepangwa uwe hivyo basi kwa hakika umekuwa 'own goal'. ccm watapata shida sana tena sana na hii sarakasi ya Jairo. Inaonekana kama wamejenga 'Institutional corruption.
 
duu hii ni noma naona jailo atadai fidia kwa kumdhalilisha,serikali itamlipa na fidia juu!
 
Unajua miaka minne iliyobaki naona Tanzania itakuwa zaidi ya JEHANAM,Unajua kuna sehemu nyingi za kumbana Jairo kwanza kwa utendaji wake mbovu, pili kama mwajiriwa amewahi kuwatukana wabunge kuwa wanafanana na ZE COMEDI kwa haya tu ingetosha kumshikisha adabu.

Lakini anyway kesi ya NGEDERE ilienda kwa NYANI na haya ni maamuzi ya . tukae tukijua hizo ni rasharasha tuu Masika yenyewe bado.
 
Tunasubiri tamko la Askofu Slaa! Hivi huyu mtu yupo?
 
"Wana jf "ni kama "ze comedy". Tena ile ya "EATV"
 
Mhe Tundu Lissu, Zitto Kabwe, Halima Mdee, Chiku Abwao, Mchungaji Msigwa, Kamanda Lema, BAVICHA, UDDASA, Tanganyika Law Society, Dr Hosea, Mama Shellukindo, Deo Filinkunjombe, Ole Sendeka, Mama Malecela, hivi mmesoma na kuyatafakari maneno haya?????????????????
Hawa wote wanasign tu posho za vikao!
They are all commedians!
 
Sasa siku ile Pinda alipomuhukumu Bungeni aliposema kwamba kama angekuwa yeye ndie aliyemteua, angekuja tu bungeni siku ile kutoa taarifa kwamba alishamtimua. Leo hii sijui Pinda atatuelezaje! Au atamwangaliaje Mkweree na Jairo!

Kweli usicheze na Mkweree!
Ningekuwa pinda ningeachia ngazi leo hii ili niishi kwa haeshima kuliko kuishi kwa kujikomba na kujidhalilisha KWELI JAIRO HANA HATIA anachangisha pesa za serikali kwa risiti ipi zikaidhinishwa na nani kutumika je mkaguzi wa serikali ataziacaunt kweli tanzania jina lako ni tamu sana wageni wanakupigania hata jairo naye amekulamba kweli wewe tanzania ni mama huruma kama maharage ya mbeya
 
Yaani Luhanjo kageuka kuwa mpelelzi mkuu na wakati huo huo mahakama kuu! Sijawahi kuona dhalau kubwa kwa raia kama hii ya luhanjo. swali, kwa nini kesi ya David Jairo isingeshilishwa kwa jeshi la polisi kupeleleza?

Luhano, kumbuka , hakuna marefu yasio na ncha!
 
Jamani hawa watu wa karibu na JK akiwemo Luhanjo wana immunity kubwa ya kifisadi lakini itaisha 2015 na naomba hizi kashfa ziwekwe kwenye list ili zote zije kufufuliwa wakati mtu serious tutakayemchagua 2015 aweze kuwashughulikia. Kesi hizi na tuhuma hizi za wazi na zilizokuwa na ushahidi haziwezi kuachwa hivi hivi kwa sababu tu watu waliopewa dhamana ya kusimamia rasilimali na maadili ya nchi yetu wameamua kulindana kwa maslahi yao wenyewe na si ya taifa
mkuu unataka kusubiri mpaka 2015??
 
Hata kama ni milioni 500 hizo zilitumikaje? ni nani walilipwa na kwa ajili gani? Na je ni kawaida siku zote kwa wizara hiyo na vipi wizara nyingine?
 
waungwana hii inanichanganya na wala hainiingii akilini kwani kilichokua kinachunguzwa hasa ni nini?
1. idadi ya taasisi zilizo chini ya wizara husika.
2.pesa alizokusanya
3.dhumuni la ukusanyaji wa pesa
4.matumizi ya pesa zenyewe.
waungwana kilicho nichanganya zaidi ni kuwa sheria inasemaje juu ya uchangishaji wa pesa ktk wizara za serikali na taasisi zake.
 
Gooooshhhh!...<i>My hairs!<br />
</i>Wameogopa atafichua mengi?<br />
Nchi ya laana hii!...!<br />
Igunga mpoooo????
<br />
<br />
na 2015 watz tukifanya maamuzi kwa kutumia masaburi tumekwisha! Mwizi anapewa cheti funga yangu leo haitahesabiwa potelea mbali
 
Back
Top Bottom